Ni ngumu kuamini utajiri wa hawa wachungaji unatokana na SADAKA pekee

Ni ngumu kuamini utajiri wa hawa wachungaji unatokana na SADAKA pekee

Kinumbo

JF-Expert Member
Joined
Dec 8, 2019
Posts
3,039
Reaction score
5,560
Tanzania hii kila uchwao ma pastor wanaibuka na kuwa wengi zaidi, wengi wakihubiri habari za Mwenyezi Mungu. Wametokea kuwashawishi watu wengi kuwafuata ama kuwa nao katika makanisa yao. Asilimia kubwa ya hao ma pastor wamekuwa na utajiri mkubwa mno kupitia makanisa yao.

Baadhi ya hao ma pastor ni kama, pastor Tony Kapola, pastor Dale, pastor Boniface Mwamposa, pastor GeorDavie na wengine wengi. Hawa ma pastor wamekuwa na umaarufu pamoja na utajiri mkubwa mno kupitia hizo shughuli zao za kichungaji. Wanaishi maisha expensive sana, kiasi kwamba unabaki unajiuliza ni u pastor tu ama kuna mambo mengine.

Napata mashaka kwa ile misafara yao ya magari ya gharama ni SADAKA pekee imefanya vile? Wanasukuma ma G Wagon, BMW, Benz za maana na nyinginezo nyingi za bei mbaya. Ni kweli Tanzania hii waumini wao wanatoa kiasi kile, inatia mashaka sana.

Inakuwa ngumu kuamini.
 
Kwa mfumo wa Katoliki mfano sadaka ya Jpili kwa makanisa ya mjini na sehemu mambo safi, jumla hufika mil 5 kwa Jpili moja. Hapo nazungumzia Parokia moja. Wastani ni mil 3.5. Hapo ni ibada 3 hadi 4. Sasa hawa wa ibada moja, tena sehemu za kukodi kama kwenye hayo majengo ambapo wanalipa kodi, tena na aina ya waumini walio nao ni ngumu kuamini kuwa ni sadaka tu.
Labda kidogo Mwamposa maana yeye ni mjasiriamali pia. Anauza "injili" na viambato vyake
 
Watu wana mambo yao nyuma ya hayo makanisa, wanapiga mishe zao kimya kimya. Kwenye uma inaonekana wao ni viongozi wa kidini kumbe wana michezo yao. Sadaka tu haiwezi fanya wajenge majumba ya kifahari na waendesha magari expensive kiasi kile.

Watu wana mambo yao nyuma ya hayo wanayo fanya wazi, we elewa hivyo tu. Sio wao tu kwa sasa asilimia kubwa hapa nchi michezo mingi ya ajabu ajabu inaendelea chini chini na kimya kimya. Ukitaka kuamini hilo fuatilia kwa sasa hapa nchini magari tena ya bei kubwa yananunuliwa sana, we unahisi kuna nini?
 
Money laundering inaweza hata ikawa kutoka kwa watu wa nchi zingine kabisa
Au hata mzigo wa Unga umeuzwa hela zinatakatishwa kwa hawa jamaa
 
Naamini kuna michezo inaendelea nyuma ya pazia maana zile G Wagon hununui kwa sadaka.
Money laundering inaweza hata ikawa kutoka kwa watu wa nchi zingine kabisa
Au hata mzigo wa Unga umeuzwa hela zinatakatishwa kwa hawa jamaa
 
Back
Top Bottom