Jackal Malinza
Member
- Aug 28, 2013
- 33
- 4
Kiukweli jamani ninaumia sana na huu mfumo wa elimu yetu maana umekuwa ukiendeshwa kiutashi wa wanasiasa, embu angalia kipindi Mungai alipokuwa waziri alifuta biashara na kuunganisha Physics with Chemistry, yaani kila waziri akija anatambulisha kitu chake, halafu swala la shule za kata hivi kweli walifanya uchunguzi yakinifu kabla ya kuanzisha kweli au tulikulupuka coz unakuta shule hazina vifaa na watoto wanakaa chini je kweli hapo tumefanikiwa? halafu swala la mtaala kuangalia maswala ya nje wakati hayomataifa hayasomi chochote kuhusu sisi y sisi tuwasome kuhusu wao? Embu jamani tufunguke kwa maoni hivi unaona nini kifanyike turejeshe hadhi ya elimu yetu maana sasa hivi mtu anamaliza chuo hawezi kuanzisha mradi wake anangojea kuajiriwa, je ndo tumelaaniwa au tumekosea wapi?