Ni raha sana kuwa CCM

Ni raha sana kuwa CCM

My Son drink water

JF-Expert Member
Joined
Nov 30, 2016
Posts
4,932
Reaction score
13,306
Ukiwa mwana CCM utaishi kwa Raha sana, maana yake ni kwamba, hutaweza kuhisi maumivu yoyote ya maisha.

Kila baya kwako litakuwa ni zuri tu, na kila zuri kwako ni zuri tu, kifupi ni kwamba hakunaga stress ukiwa mwana CCM.

Bidhaa zikipanda Bei kwako ni sawa tu, ukishinda na njaa pia ni sawa tu,ukiugua ukakosa huduma ya matibabu ni sawa tu.
Ukikosa ajira ni sawa tu.

Ukionewa na Police ni sawa tu, ndani ya CCM viongozi wote ni watakatifu hakunaga mwenye Dhambi au kasoro yoyote.

Ndo maana Jenerali Ulimwengu amechimbwa mkwara wa kufa mtu kwa kulikosoa Bunge ambalo Spika wake ni mwana CCM na wabunge wote ni wana CCM.

Kosa la Jenerali Ulimwengu ni kwanini anawakosoa watu ambao huwa hawakosei?

Mungu hana kasoro na ukimkosoa utakuwa salama, lakini ukiikosoa CCM hutakuwa salama.

Jamani ni Raha iliyoje kuwa mwana CCM?
 
Ndio maana Mimi sihami CCM japo wamenivunjia kibanda changu cha umachinga. Yaani hakuna lilionipa raha kama hili. CCM sio ya kila mtu ni kwa ajili yetu wenye akili furani hivi.
 
CCM ni ufunguo wa maisha upinzani ni kufuli.
Kuthibitisha wale walioondoka kwenye ufunnuo wa Maisha baada ya kwenda huko kwenye kufuli ,wamerudi mbio tena kwa kasi ya ajabu tulipowailiza mbona mmerudi huwaga wanajibu mtu kwao.
 
Back
Top Bottom