Ni rahisi mwanamke kukuacha ikiwa>.......

Ni rahisi mwanamke kukuacha ikiwa>.......

kitalolo

JF-Expert Member
Joined
Dec 4, 2006
Posts
1,827
Reaction score
708
Nimesikia kuwa ikiwa ulioa mwanamke na ukamkuta tuseme ni mdada tu wa nyumbani hana kazi na elimu yake ni yawaida ikatokea baada ya kuwa kwenye mahusiano au ndoa ukaamua kuendeleza kielimu pengine hata kumwezesha kupata kazi eti wazee wanasema kuna uwezekano mkubwa wa demu huyo kuachana na wewe kwavile pengine mlipoazna mahusiano aliona kutokana na levo yake wewe ndio unayemstahili sasa akipanda chata atataka kuwa na wa levo ya juu zaidi kwahiyo uwezekano wa yeye kutoka nje ya ndoa unakuwa mkubwa zaidi au hata kuachana maana sasa anakuona kama vile uko matawi ya chini na yeye yuko matawi ya juu. pia kuna usemi kuwa mwanamke ataona kuwa kwavile wewe umeamua kumwendeleza kielimu ni sawa na unamdhgarau na unamwona kama sio msomi au humpendi tena mbaya zaidi ni wanasema ni wakati wa kumtongoza demu au wakati wa uchumba ukamwahidi vitu kama kusomeswa na mengineyo kama hayo eti anaweza kukubali au kuingia kwenye ndoa kwavile tu anajua atasomeshwa na mambo mengine kama hayo. je kuna ukweli wowote katika hili na kama ni kweli je nini kafanyike?
 
Mkuu Kitalolo (Ngitalolo????) hebu weka paragraphs basi ndugu yangu ili tusome kwa raha zetu...
 
Kubadilika ni hulka ya mtu sioni ukweli wa jambo hilo.
Siku zote me husema panapo upendo hamna matatizo unless mmeoana kwa sababu nyinginezo.
 
Kitalolo unasomesha?Kubadilika kwa mtu ni tabia binafsi ya mtu hizo factor nyingine hata zikiwepo kama mtu mtulivu ni mtulivu tu na kama ni mcharuko basi twende kazi
 
Kitalolo unasomesha?Kubadilika kwa mtu ni tabia binafsi ya mtu hizo factor nyingine hata zikiwepo kama mtu mtulivu ni mtulivu tu na kama ni mcharuko basi twende kazi
ndio nasomesha sasa wananitisha kuwa ntajaachika mkuu wa kurambaramba
 
waweza achika ndiyo. Nina mifano kadhaa ya watu waliotendwa baada ya kuwasomesha watu wao. Ila usikate tamaa. Daima katika maisha ni ku-risk. Unaweze achika au pengine usiachike. Yategemea tabia ya mtu. Ila uwe tayari kwa lolote. Tenda wema.... nenda zako.
 
waweza achika ndiyo. Nina mifano kadhaa ya watu waliotendwa baada ya kuwasomesha watu wao. Ila usikate tamaa. Daima katika maisha ni ku-risk. Unaweze achika au pengine usiachike. Yategemea tabia ya mtu. Ila uwe tayari kwa lolote. Tenda wema.... nenda zako.

sasa ukiweke data kuonyesha kwa asilimia unafikiri inaangukia wapi zaidi kuacha au kuendelea kuwa pamoja baada ya kusomesha?
 
hili laweza kutokea kwani wapo wanaobadilika baada ya kusaidiwa...ni kuomba Mungu usikumbane na binti wa dizaini hiyo.
 
Hiyo inatokea mara nyingi. Ni kwamba unapompeleka shule unamjengea ufahamu/uelewa, unamuingiza katika mazingira mapya na huko anakutana na watu tofauti tofauti, anajifunza mambo mengi tofauti kutokana na hiyo exposure. Ni katika kipindi hicho ndipo anaweza kujijua aina gani ya mwanaume angependa kuwa nae kwasababu tayari ameshainteract na watu kwahyo anawaelewa vizuri zaidi kuliko mwanzo. Kidogo kidogo anaanza kulinganisha mahusiano yenu na mahusiano ya rafiki au watu wake wa karibu. Anaweza kuhisi kuna vitu ana miss au mahusiano yenu yana mapungufu. Ikitokea hvyo ni rahisi kukuacha na kwenda anapoona ni pazuri zaidi.
Hata wale wanaokuwa na wapenzi ambao wapo secondary mfano form1, probability ya kuwa wote hadi amemaliza chuo huwa ni ndogo.
Hiyo isikuwe wasiwasi maana watu wanatofautiana.
 
Hiyo inatokea mara nyingi. Ni kwamba unapompeleka shule unamjengea ufahamu/uelewa, unamuingiza katika mazingira mapya na huko anakutana na watu tofauti tofauti, anajifunza mambo mengi tofauti kutokana na hiyo exposure. Ni katika kipindi hicho ndipo anaweza kujijua aina gani ya mwanaume angependa kuwa nae kwasababu tayari ameshainteract na watu kwahyo anawaelewa vizuri zaidi kuliko mwanzo. Kidogo kidogo anaanza kulinganisha mahusiano yenu na mahusiano ya rafiki au watu wake wa karibu. Anaweza kuhisi kuna vitu ana miss au mahusiano yenu yana mapungufu. Ikitokea hvyo ni rahisi kukuacha na kwenda anapoona ni pazuri zaidi.Hata wale wanaokuwa na wapenzi ambao wapo secondary mfano form1, probability ya kuwa wote hadi amemaliza chuo huwa ni ndogo. Hiyo isikuwe wasiwasi maana watu wanatofautiana.
Bi shosti umenena vema mpaka mwenyewe nimekukubali, maelezo yako ni ya ukweli aisee!
 
si wanawake wote .. ingawa haya yaliwahi kumkuta ndugu yangu ... yule msichana bila aibu alimuacha solemba alipomaliza kusomeshwa na kupata kazi ya ualimu... akapata jamaa hukohuko shule anapofundisha
 
si wanawake wote .. ingawa haya yaliwahi kumkuta ndugu yangu ... yule msichana bila aibu alimuacha solemba alipomaliza kusomeshwa na kupata kazi ya ualimu... akapata jamaa hukohuko shule anapofundisha


unaona sasa?
 
Na hata hapa kwenye utetezi wako baaado unachapia....pole kwa majukumuanya way turud kwenye mada,haya mambo yapo sana mdau tena sana,nina mifano lukuki,mmoja ulimtokea ndugu yangu az my bro.........ni kwamba yeye alikuwa na kabinti,kale kadem alianza nako uhusiano tangu kapo primary,kalipofaulu baba akakataa kukasomesha jamaa akakapeleka Kilakala,then fom for kaka faulu jamaa akamuunganishia advance kilakala tena,mtoto akaenda SUA,jamaa akawa anamhudumia kama kawaida,mtoto akaua shahada ya kwanza,akaua ya pili,akamchakachua jamaa na kumuuliza anadai kias gani apewe???????bint sasa yupo na maisha yake........TAFAKARI
niko bise nisaidie kuedit.maana nimbanwa sana hapa ofisini nikaamua kuandika chapchap
 
Hiyo inatokea mara nyingi. Ni kwamba unapompeleka shule unamjengea ufahamu/uelewa, unamuingiza katika mazingira mapya na huko anakutana na watu tofauti tofauti, anajifunza mambo mengi tofauti kutokana na hiyo exposure. Ni katika kipindi hicho ndipo anaweza kujijua aina gani ya mwanaume angependa kuwa nae kwasababu tayari ameshainteract na watu kwahyo anawaelewa vizuri zaidi kuliko mwanzo. Kidogo kidogo anaanza kulinganisha mahusiano yenu na mahusiano ya rafiki au watu wake wa karibu. Anaweza kuhisi kuna vitu ana miss au mahusiano yenu yana mapungufu. Ikitokea hvyo ni rahisi kukuacha na kwenda anapoona ni pazuri zaidi.
Hata wale wanaokuwa na wapenzi ambao wapo secondary mfano form1, probability ya kuwa wote hadi amemaliza chuo huwa ni ndogo.
Hiyo isikuwe wasiwasi maana watu wanatofautiana.

well said
 
kama yuko busy sana kapataje muda wa kusoma hiyo comment
 
Ni kweli mara nyingi hilo hotokea .Mimi nimeshashuhudia mara mbili.
 
Ni kweli baadhi yao hubadilika hii ni moja ya sifa.ila vilevile inategemea na upeo wake huyo demu au mke.wapo wanaona maisha ni dili wengine huwa na mtazamo wa kuridhika uliyenaye.asante
 
Kwa tafiti nyingi na ukweli tukiangalia maisha halisia hiyo kitu ni kweli kabisa,wanawake wengi waliosomeshwa na kutafutiwa kazi na waume zao huwa hawadumu pamoja katika maisha,nasema ni kweli maana mie mwenyewe imenikuta
 
Back
Top Bottom