Tatizo la yanga ni kuanzia uongozi kocha hadi mashabiki.
Uongozi umesajili wachezaji kwa kukurupuka. Timu haiko balanced kiufundi. Kuna wachewaji namba 4 zaidi ya watano ally ally, ally sonso, dante, lamire nk wakati natural full backs namba 2 n 3 ni wawili tu boxer n macelo na huyo marcelo analetwa dk za mwisho baada ya gadiel kusaini simba wakawa na aibu timu haina left back wakaletewa na mwigulu toka singida. Same story mbele kuna namba 10 zaidi ya wa nne wakati namba 9 targetman hamna. Hiyo molinga hakuna mchezaji mule. Mchezaji hata kama hana match fitness akigusa mpira unajua mguuni kuna jambo.
Kocha. Zahera nae akijua timu imesajiliwa ni almost mpya alitakiwa awahi preseason awajue wachezaji wake. Badala yake kaja dk za mwisho. Ligi inaannza hawajui wachezaji wake. Pili.zahera anatumia nguvu nyingi kuwaaminisha watu molinga ni mchezaji huku akiwa hana match fitness kama anavyodai. anawaacha wengine jukwani ambao wako.fit zaidi yake. Tatu waliweka kambi mwanza kujiandaa na zesco lakini cha ajabu akampanga molinga game zote wakati akijua hawezi kumtumia mechi dhidi ya zesco. Kwanini hakuwatumia kina balinya kalengo katika kuwaandaa game na zesco.