crome20
JF-Expert Member
- Feb 5, 2010
- 1,193
- 810
Kumekuwa na utaratibu wa bodi ya mikopo kutumia kigezo cha mwanafunzi ambaye amesoma shule za private kukosa sifa ya kupata mkopo wa bodi kwa ajili ya High learning Institution. Mimi napingana na dhana hii kwa sababu zifuatazo Mosi. Kwanza kumpeleka mtoto shule ya private sio kuwa mzazi ana uwezo kifedha, maana wengi wetu tunateseka na mikopo angalau mtoto apate msingi wa elimu bora. Ni wazi kuwa kiwango cha elimu cha shule nyingi za serikali ni duni hivyo kulazimika baadhi ya wazazi kutafuta njia mbadala. Pili. ikumbukwe kuwa mpaka mtoto anafika muda wa kwenda chuo, jua pia mzazi vyanzo vya mapato hasa kwa wafanyakazi vyaweza kuwa vimeisha, mfano kukaribia kustaafu, hivyo ni wakati wa serikali kumpokea mzazi kwani alimsomesha kwa gharama si kwa faida binafsi bali awe msaada kwa Taifa Zima. Tatu ni jukumu la serikali kuhakikisha watu wanapata elimu bora, hivyo kumnyima mkopo ni sawa na kumwadhibu badala ya kumshukuru mzazi kwa kuisaidia serikali maana kama watoto woote ambao wako private wakirudishwa shule za serikali ni wazi kuwa itakuwa balaa tupu maana wasingetosha katika majengo machache na duni yaliyopo. Ukitaka kutenda haki ni lazima ujiridhishe kuwa mzazi bado anao uwezo uleule, hana majumu mengine ya kusomesha, hana project kubwa inayotumia kipato chake kama vile ujenzi, ugonjwa n.k