Ni sahihi kusema " nitakufunga leo" huku wewe si mchezaji wa timu husika?

Bonde la Baraka

JF-Expert Member
Joined
Sep 22, 2016
Posts
4,580
Reaction score
7,943
Wadau labda kwa kuwa mimi si mpenzi wa mpira wa miguu kivile, nashangaa kuwakuta vijana wenzangu wakibishana kwa kauli kama hii, "nakufunga leo huniambii kitu mimi" huku timu anayoitetea hana hisa wala ubia nayo , hana kadi ya uanachama, hajawahi kumwona live hata mchezaji mmoja licha ya kwenye video na magazetini ,timu iko nchi za wazungu ambao wengi wanatuona kama unshapped mind persons sisi weusi, yeye si kocha mkuu wa timu, si mhasibu wa timu, si mfadhili wa timu ,si mpishi wa timu ,yaani hana nafasi yoyote katika timu husika.
Is this right?
 
Uzuri umeshasema we sio mpenzi wa mpira kivile.
 
Mkuu hujui nguvu ya shabiki.? Hata ivyo hujui haya mambo.
Waachie wenyewe
 
Mkuu hujui nguvu ya shabiki.? Hata ivyo hujui haya mambo.
Waachie wenyewe
Kweli ngoja nitulie. Niliwaona vijana jioni hii wanaitana mbwa , mara ngedere nyie hauniwezi, nakufunga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…