Ni sawa kurudia dozi ile ile mara mbili mfululizo?

Ziltan

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2011
Posts
2,672
Reaction score
6,880
Salaam.

Mrs. wangu ametumia Dozi ya Azethromyzin vidonge 30 (2x3). Ni kwa ajili ya fungus na kutoa uchafu mweupe unaomtoka.

Sasa tangu ameanza imeonesha matumaini fulani lakini aliambiwa akimaliza arudie tena dozi hiyohiyo hata mara 3.

Je, ni sawa kurudia dozi hiyo?

Asanteni.
 
Mkuu azithromycin ni antibiotic na si anti fungal mbona?

Ila kama bado uchafu unatoka na amemaliza dawa rudinaye hospital wajaribu kufanya vipimo tena.
Utumiaji wa mda mrefu wa madawa husababisha usugu wa dawa.
 
U.T.I
Ukitaka kuikomesha tumia Ngongwa saba asubuhi na anywe maji Lita moja kabla yakula chochote kwa mda wa Siku saba
Kama imekomaa ni siku 14 ukifanikiwa lete mrejesho.
 
Hiyo sio dawa ya fungus ni ya kuuwa vimelea aina ya bacteria,kwa dalili hizo za uchafu mweupe ukeni yawaza kuwa fungus ila je anawashwa ukeni?ushauri nenda hospitali na si duka la dawa maana nahisi hiyo dawa umepewa na mtu baki si daktari au mtoa huduma za afya mweny uweledi
 
Kubadilisha dawa ni njia nzuri kupata tiba ya haraka, kuna dawa unaweza tumia miaka nenda rudi usipate nafuu
Ila kama dozi ya mwanzo imemtiba basi aendelee nayo, hususani kwa gonjwa kama hilo maana huwa linahitaji dozi mara mbili ili kumaliza kabisa, pia msishiriki tendo mpaka apone pia huwa wanashauri hata mwenza wake atumia hata kama mzima ili usije muambukiza
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…