Ni tabia mbaya,jitahidi uiache.

ndayilagije

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2016
Posts
7,491
Reaction score
8,304
Katika maisha kuna mambo mengi yanachosha na kushangaza pia.yanaleta ukakasi.
_Mtu kakuamini anakueleza tatizo lake,kama hujui jinsi ya kumsaidia/kumshauri mwambie ukweli tu,usianze kumweleleza shida zako. Tatueni kero yake ikiisha muanzishe utatuzi wa kero yako.
_Uko ndani ya usafiri wa umma,kuna wasafiri wa kila aina wenye matatizo/mafikra kibao unazungumza ujinga mwanzo mwisho.Tulia kidogo acha watu wawaze wanayowaza.
_Umeenda kwenye msiba/harusi au kusanyiko lolote lile unawasiliana kwa simu kwa msauti mkuuuubwa!watu wote wanakata shingo kukushangaa wewe wala hujishtukii.
_Umeenda ofisi ya umma badala ya kueleza shida iliyokupeleka hapo,unalaumu mtoa huduma uliyekutana naye hapo juzi!Mimi nikusaidieje sasa!
_Umbea na usengenyi ni pacha wa mtu mweusi,haukwepeki!jaribu basi kutosengenya hadharani ya nini kujiongezea maadui?
_Jirani kajitutumua kanunua kigari chake,kama hutaki kumpongeza si ufanye tu kama hujaona!siyo unaanza kwanza gari yenyewe ya mkopo halafu mbayaaa!wewe unayo.
_Umenunua homthieta nyumbani kwako,unagonga mziki kama ukumbini...fungulia kwa mahitaji yako bhana.!
_Mama yako anahali mbaya hapo kwenu kisiju tu,nyumba inavuja,hata soler hana ni mzee na ni mgonjwa,lakini hapo kwako Kinondoni unafanya sherehe na marafiki kila wiki!!!!!
Ni tabia mbaya!
 
Hii tabia ya kusahau wazazi wengi wanayo sana tena wengine hata watoto wao watembelee wazee wao.
 
Hii tabia ya kusahau wazazi wengi wanayo sana tena wengine hata watoto wao watembelee wazee wao.
Ni tabia mbaya mkuu. Utashindwa kuwapeleka watoto kwa wazazi wako kwasababu hujapeleka vitanda vizuri,hakuna choo na hata chakula ni shida.
 
Tabia za walimwengu ndo tulivyo ni kukemea au kufanya yako tuu
Mengine ni magumu sana kukemea mkuu,huwezi ingilia uhuru wa mtu na hasa unapoona kabisa kuwa hajitambui inabidi umvumilie tu. Hajavunja sheria yoyote ile. Lakini bado ni tabia mbaya.
 
Mengine ni magumu sana kukemea mkuu,huwezi ingilia uhuru wa mtu na hasa unapoona kabisa kuwa hajitambui inabidi umvumilie tu. Hajavunja sheria yoyote ile. Lakini bado ni tabia mbaya.
Ni kweli ndio vile nimesema ukishindwa kukemea bas unaamua tu kufanya yako( kukaa kimya)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…