Desprospero
JF-Expert Member
- Feb 1, 2023
- 1,015
- 2,493
Wapigadili, walafi, mafisadi na matapeli wana akili sana. Kila kiongozi anayeingia madarakani humkalia kikao na kujua wapi anawashwa ili wamkune hapo hapo!
Hakuna Rais aliyewahi kuwa na mapenzi na watu wake Kwa hapa Tanzania kama Julius Nyerere lakini hatukuwahi kusikia akiitwa "Rais wetu mpendwa". Mwinyi hakuitwa "Rais wetu mpendwa". Mkapa ndiye kabisaa hakuhitaji sifa hiyo. Hata Jakaya na ubishoo wake hakuitwa Rais wetu mpendwa.
Kwa mara ya kwanza tumesikia Amiri Jeshi akiitwa mpendwa ni Awamu ya 5 ya Magufuli (mwendakuzimu) na muasisi wa sifa hiyo ni Paulo Makonda then Mawaziri wakafuata.
Awamu ya 6 kauli hii imepamba moto lakini inatolewa na wateule wa Rais tu na si vinginevyo. Hata Marekani, Rashia, Kenya, Uingereza, Brazili, Equador nk hatujawahi kusikia Mkuu wa Nchi akiitwa "Our Beloved President", aibu.
Kauli hii ina Siri kubwa ya utapeli wa kisiasa. Ni lugha ya ulaghai, wizi, woga, hofu na kujiweka karibu na Mamlaka kuficha upigani uliojificha. Hii ni lugha ya Sanaa ya mahusiano yadiyo na afya. Imagine Majaliwa anamwita SSH mpendwa, Tulia Ackson anamwita mpendwa, CDF na IGP nao wamwite mpendwa, hivi wajukuu zake, wanaye, mumewe wamwiteje?
Rais ogopa na ukatae kuitwa Rais mpendwa. Behind the phrase kuna kuna ajenda ya kukupaka mafuta kwa mgongo wa chupa usione maovu Yao. Kataa tena hadharani kama Nyerere alivyokataa kuitwa mheshimiwa akataka aitwe Ndugu. Ni kwa vipi unaweza kumwajibisha anayekuitwa mpendwa?
Lakini kama na wewe unafurahi kuitwa mpendwa basi tumejua wapigadili wamefanikiwa 100% maana tunaambiwa Kwa Sasa Kuna mashindano baina na kati ya wateule wako nani akaunti yake inasoma B's na mzembe gani akaunti yake inasoma Ms. Wawili miongoni mwao wameshagonga Ts. Hallelujah!
Hakuna Rais aliyewahi kuwa na mapenzi na watu wake Kwa hapa Tanzania kama Julius Nyerere lakini hatukuwahi kusikia akiitwa "Rais wetu mpendwa". Mwinyi hakuitwa "Rais wetu mpendwa". Mkapa ndiye kabisaa hakuhitaji sifa hiyo. Hata Jakaya na ubishoo wake hakuitwa Rais wetu mpendwa.
Kwa mara ya kwanza tumesikia Amiri Jeshi akiitwa mpendwa ni Awamu ya 5 ya Magufuli (mwendakuzimu) na muasisi wa sifa hiyo ni Paulo Makonda then Mawaziri wakafuata.
Awamu ya 6 kauli hii imepamba moto lakini inatolewa na wateule wa Rais tu na si vinginevyo. Hata Marekani, Rashia, Kenya, Uingereza, Brazili, Equador nk hatujawahi kusikia Mkuu wa Nchi akiitwa "Our Beloved President", aibu.
Kauli hii ina Siri kubwa ya utapeli wa kisiasa. Ni lugha ya ulaghai, wizi, woga, hofu na kujiweka karibu na Mamlaka kuficha upigani uliojificha. Hii ni lugha ya Sanaa ya mahusiano yadiyo na afya. Imagine Majaliwa anamwita SSH mpendwa, Tulia Ackson anamwita mpendwa, CDF na IGP nao wamwite mpendwa, hivi wajukuu zake, wanaye, mumewe wamwiteje?
Rais ogopa na ukatae kuitwa Rais mpendwa. Behind the phrase kuna kuna ajenda ya kukupaka mafuta kwa mgongo wa chupa usione maovu Yao. Kataa tena hadharani kama Nyerere alivyokataa kuitwa mheshimiwa akataka aitwe Ndugu. Ni kwa vipi unaweza kumwajibisha anayekuitwa mpendwa?
Lakini kama na wewe unafurahi kuitwa mpendwa basi tumejua wapigadili wamefanikiwa 100% maana tunaambiwa Kwa Sasa Kuna mashindano baina na kati ya wateule wako nani akaunti yake inasoma B's na mzembe gani akaunti yake inasoma Ms. Wawili miongoni mwao wameshagonga Ts. Hallelujah!