Ni taratibu zipi zinafatwa kuanzisha/ kusajili Kampuni?

Sine r Winters

Senior Member
Joined
Jul 10, 2012
Posts
110
Reaction score
15
Vp wakuu, ni taratibu zipi zinafatwa mpaka uweze kusajili kampuni? Na huwa zinasajiliwa taasisi gani?

NB: kampuni ya IT.
 
BRELA ndie wakala wa kusajili kampuni Tanzania. unapaswa kuchagua jina la kampuni kwanza. wao ukiwapa pendekezo la jina, wataangalia kama hakuna kampuni inayotumia, na kama hakuna watakuruhusu utumie. utapaswa kuandaa nyaraka mbili ambazo ni memorandum of understanding na article of association. hizi nyaraka zinapigwa mhuri na mwanasheria au mhasibu. sheria zetu zinahitaji wamiliki wa kampuni wawe kuanzia 2 na kuendelea. kuna gharama unazolipa moja kwa moja BRELA ambazo ni ada ya usajili na gharama ya kuangalia jina. kama ukishirikisha wataalam kama sisi, tutakuchaji gharama ya ku facilitate mchakato mzima. cha kufahamu, kampuni ni kama binadamu tu, kwa hiyo ikihitaji kufanya biashara inapaswa kwenda kwenye mamlaka husika kupata kibali cha kuendesha biashara. nilikuwa naweka msisitizo hapa, kampuni sio kibali cha kufanya biashara
 
Vp wakuu, ni taratibu zipi zinafatwa mpaka uweze kusajili kampuni? Na huwa zinasajiliwa taasisi gani?

NB: kampuni ya IT.
Mkuu nakupa heshima zako.Mimi naweza kukusaidia kwenye mchakato mzima kuanzia name search,memorandum and articles of association mpaka pale utapewa certificate of Incorporation na BRELA.We niPM au nipigie simu namba 0769210807 tushauriane.Nimefungua kampuni kadhaa zikiwepo za IT na Telecoms kwa hivyo taratibu nazielewa sana
 

sheria zimerekebishwa na sasa mmiliki/mkurugenzi anaweza kuwa mmoja.
 
asanteni sana kwa msaada wenu, nw nimepata mwanga. garama zake zikoje mpaka kumaliza usajili na BRELA inapatikana mikoa yote nchini e.g dodoma moshi etc
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…