Ni ujio wa mara nyingine tena.

Sajunne

Senior Member
Joined
Jul 19, 2011
Posts
104
Reaction score
58
Napenda kuwashukuru sana wadau wote walio changia mada yangu na wale ambao hawakubahatika kuchangia mnamo mwezi AGOSTI, ushauri wenu na mawazo yenu niliyazingatia na kuyafanyia kazi kwa ipasavyo. But nimerudi na muendelezo wa topic mpya kama sio mpya kwani ni kama mwendelezo. Yule girl niliyewahi kuwaletea mada imuhusuyo yeye yalitokea mengine ya kutokea, kwani nilikaa kimya kama mlivyo shauri. Lakini mnamo mwezi wa OKTOBA tarehe siikumbuki vizuri, alikuja home huyo girl gafla kwa kuwa sikuwa na mawasiliano nae ya aina yeyote, nilikuwa ndani mara nikasikia hodi, nilipofungua mlango nikakuta ni yeye {girl} nikamuuliza nikusaidie nini ! Akasema anaomba kuongea na mimi japo dk 5, sikuwa na kinyongo zaidi nakamruhusu kuongea. Mara akapiga magoti na kuanza kutembelea magoti akisema anaomba nimsamehe na turudi kuwa wapenzi , kwa kutaka kuepusha mengi ambayo yangezua mjadala kwa muda mrefu nikamwambia mimi nilisha msamehe toka muda. Bt baada ya hapo akawa ameondoka amerudi kwao, lakini kitu kichonishangaza zaidi mida ya usiku siku hiyohiyo akanipigia cm na nikapokea 2kapiga story kiana na mwisho wa maongezi akaomba hela Tsh 10,000 ana shida. Kuanzia siku hiyo sikupokea cm yake wala kujibu msg zake. Na hadi leo huwa ananipigia cm na kunitumia msg lakini huwa sipokei na wala kuzijibu meseji zake. Wadau mnafikiri ni kwanini huyu dem aliamua kunitafuta tena? Sikuwa na jibu la maswali haya yote. Girl mwenyewe anaishi sehemu ya squater's . Wadau nifanyete ili asinisumbue tena. Pia nilimpenda sana huyu demu na kumuhudumia kwa kiasi furani ndio maana anazidi kunisumbua.
 
Kumbe story za humu jf huwa zina series?huyo demu nae njaa sana,anagongea hadi buku 10!!
 
Katika mapenzi ukiwa mnyonge utaumia ,
we ndo hivyo tayari,
japo sielewi hiyo story yako but huyo demu hafai atakutesa zaidi,
 
Umeamua kupiga chini,piga chini kiujumla si unakuja kulalamika lalamika hapa na kuhojihoji.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…