Ni wakati muafaka kwa Serikali kumpangia Maxence Melo majukumu makubwa ya Kitaifa kwa Maslahi mapana ya nchi yetu

Kwa jinsi ninavyomjua Mtani wangu wa Kihaya, Kaka yangu, Mkuu wangu na Genius IT Guru Maxence Melo akikubali Teuzi yoyote ile ndani ya Tanzania hii ya sasa yenye Siasa za Kinafiki, Kujipendekeza na Tawala zisizojielewa zenye Kuharibu badala ya Kujenga nitamdharau mazima hadi Umauti wangu.

Kwa IQ yake Maxence Melo nchi ambazo nikisikia kapata 'Ulaji' huko na GENTAMYCINE nitafurahi na Kumfurahia ni za Rwanda, USA, Russia, Israel, China, South Africa, Germany, England na Uganda ila siyo Tanzania.

Acheni tu abakie Kututumikia Sisi Watoa Maoni Huru kupitia huu Mtandao wake ambao kiukweli una Faida kubwa Kwetu Watanzania kuliko hata angekuwa katika Teuzi yoyote ile ya Kiserikali.

Ni Cheo Kimoja tu ambacho GENTAMYCINE naona kitamfaa kwa Tanzania hii nacho ni cha Yeye kuwa Head of State ( Rais ) na siyo Vingenevyo na akiwa Rais upesi sana aniteue kuwa Makamu wake ili kwa pamoja Akili za Kihaya na za Kizanaki ( wala Sato na Sangara wanasababisha Akili nyingi Kichwani ) ziwaongoze vyema Watanzania na ndani ya Mwaka Mmoja Tanzania itakuwa mbali sana Kimaendeleo na Kiustawi.
 
Napinga vibaya sana! Nina sababu ambazo hakuna ukurasa wa JF unaotosha kuandika .

Yaani Max akawe chini ya Ndugai na Siyani !
 
Maxence Melo akili kubwa. Hizi teuzi huwa zinavuruga na kuharibu misimamo ya haki na ukweli ya wateuliwa. Kumbuka Profesa aliyesema alitolewa jalalani na ndugu Slow Slow? Sikubaliani na wazo la mtoa mada.
 
Bonge ya point, kwa maneno nane umeandika hoja kubwa sana inayofaa kuzingatiwa na waTanzania wote hasa sisi vijana.
Hii dhana ya watu kudhani kulitumikia taifa ni lazima uwe na kitambulisho chenye nembo ya bibi na bwana , ila Maxence na tim yake wamelitumikia hili taifa kiliko maelezo kupitia hii kitu
 
Umeandika kama pimbi
 
🤣🤣Naona umemsifia Maxence Melo halafu haukuacha kujipigia bonge la pasi ya goli uwe V.P 🤣🤣
 
Mimi ninakubaliana nawe katika jambo moja, nalo ni "Uzalendo wa KiTanzania."

Hii nchi imekuwa ya kipuuzi sana, na hasa kupitia humu JF, imekuwa ni rahisi sana kujua ujuha mwingi unaowakabili waTanzania.

Sasa usije na mapovu yakikutoka mdomoni, ukinilaumu kwa kudhani mkuu 'Maxence' sitambui uwezo wake mkubwa; lakini ukitumia akili kidogo utatambua ujuha wa pendekezo lako, kama yalivyo mengi yanayojitokeza kwenye jukwaa hili la JF.

Watu wa aina yako, badala ya kuongeza thamani ya michango inayoletwa hapa, haya mnayoyaleta kwa sababu mzijuwazo wenyewe, yanazidi kuporomosha hadhi ya JF.

Sasa sijui tutakwenda vipi na mada za aina hiii zimejaza ukumbi mzima.
 
Kulitumikia taifa sio lazima uwe kibarua wa serikali
Na kwa uhakika kabisa mchango wake kupitia JF unathamani kubwa kwa Tanzania kuliko mengi wanayofanya waliko huko serikalini.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…