Ni wakati sasa Uwanja wa CCM Kirumba kuwekewa nyasi bandia

SaaMbovu

JF-Expert Member
Joined
Oct 8, 2013
Posts
6,027
Reaction score
5,344
Naimani mpo poa.
Kiukweli uwanja huo haujawahi kupata shughuli kubwa kama hii ya 9 December. Kutokana na maandalizi ya gwaride lililofanyika hapa takribani wiki 2 hivi na mvua zilizokuwa zikinyesha hali ya uwanja sasa hasa kwenye pitch ni mbaya sana. Zimepigwa kwata, bado wale sungusungu takribani zaidi ya 1200 wote miguu yao ilikuwa inapitia pale. Uwanja kwa sasa unahali mbaya sana unahitaji rehabilitation ya nguvu.

Hata hivyo CCM Kirumba ni moja ya viwanja ambavyo vipo busy sana na kwasasa kimepata faida ya sherehe hii ya Uhuru kwakuwa kuna baadhi vitu vingi vimefanyiwa ukarabati kama vile vyoo, rooms, ofisi, jukwaa upande wa Simba na Yanga yameongezewa paa, sehemu za kukalia zimepakwa rangi nk tatizo lipo kwenye pitch.

CCM wekeni nyasi bandia uwanja hadhi iongezeke kwakuwa unawalipa sana la sivyo rudisheni viwanja serikalini ili vifanyiwe ukarabati.
Ahsanteni.
 
Ccm hawana uchungu na hivyo viwanja sababu 'walivipora' kutoka kwa wananchi!
 
Kocha Mbrazil Maxime alikuaga hataki kabisa viwanja vya mipira kufanyiwa shughuli nyingine hata shughuli za riadha marufuku.

Ila alikua hajui tu viwanja vyote ni vya CCM.
 
Kocha Mbrazil Maxime alikuaga hataki kabisa viwanja vya mipira kufanyiwa shughuli nyingine hata shughuli za riadha marufuku.

Ila alikua hajui tu viwanja vyote ni vya CCM.
Maximo
 
Ulijazwa udongo leo,sasa sijui kama utarudi hali ya kawaida kwa namna nilivyouona umeharibika na kwata
 
Nyasi bandia ni teknolojia mfu, ulaya wanatumia viwanja vya nyasi bandia kwa mazoez ya timu mara chache. Ushaur mzur uwanja upandwe nyasi mpya na umwagiliwe...
 
Ulijazwa udongo leo,sasa sijui kama utarudi hali ya kawaida kwa namna nilivyouona umeharibika na kwata
Walijaza kabla Mh hajapita maana njia hiyo ndio alikuwa anapita kwaajili ya kukagua gwaride. Uwanja kwakweli umeharibika.
 
Nyasi bandia ni teknolojia mfu, ulaya wanatumia viwanja vya nyasi bandia kwa mazoez ya timu mara chache. Ushaur mzur uwanja upandwe nyasi mpya na umwagiliwe...
Nani kasema technology mfu. Mkuu hata nyasi zina grade ujue kama lami vile. Angalia Wanda Metropolitano acha kabisa.
 
Wale sungusungu ndio kabisa waliharibu kwa jinsi walivyokuwa wanakanyaga duuuu inabidi ufungiwe tu
 
Nani kasema technology mfu. Mkuu hata nyasi zina grade ujue kama lami vile. Angalia Wanda Metropolitano acha kabisa.
Mkuu Wanda kumbe pamepigwa nyasi fake, sikuwahi kujua hilo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…