Alhamisi 6 ya mwezi MAY mwaka 2004 magazeti mengi ya ulaya yaliandika kuwa Jose Mourinho ameiambia Fc Porto kuwa ataondoka baada ya fainali ya UEFA champions league mwaka 2004. Baada ya kuifunga 3-0 monaco kwenye fainali iliyopigwa arena Auf Schalke Jose aliondoka Porto
Jose aliwahi kusema kama angetaka kazi rahisi basi angesalia Fc Porto na kuwa mungu mtu pale..Lakini amemua kuondoka ili kusaka changamoto mpya.. Mpaka sasa baada ya kuondoka Porto amezunguka katika vilabu vingine vi 4 tofauti ambavyo ni Chelsea,Inter milan,Real Madrid na Manchester united
Hata Pep Guardiola aliwahi kusema “nahitaji changamoto mpya.nataka kutumia nafasi hii kuwa kocha pale uingereza nataka kuzoea hali ya uingereza...nina miaka 44 ni wakati sahihi ..kuna ofa lakini sijasaini yeyote mpaka
sasa..nitakapopata timu mpya nitawajuza nyote”
Kuna wakati mwanadamu unafika unahitaji changamoto mpya..Kwa mfano Pep 2012 aliona wazi kuwa wachezaji wa Fc Barcelona wote tayari wameshashinda kila kitu..
Hawakuwa na laziada wanalo hitaji..Yamkini walihitaji mwalimu mpya mwenye mbinu mpya ambaye angeweza kurudisha hamu yao ya ushindani kuwa maradufu..Pep alikwenda kupumzika Marekani
Hata jose alikwisha liona jambo kama hili… Isinge wezekana kirahisi kwa timu kama Porto kuweza kurudia mafanikio ya 2004..Jose aliangalia mbali Zaidi aliona jinsi ambavyo samaki wakubwa wangeitafuna Porto msimu uliofuata kwa kuwachukua wachezaji wake imara
Baada ya msimu wa 2013-2014 niliamini Diego Simeone angeondoka Atletico Madrid..Atletico walichukua La Liga na kufika fainali ya UEFA champions league na kufungwa na Real Madrid..Kwakuwa niliona Atletico ingewachukua muda kuweza kurudi katika ubora ..
Chelsea waliwachukua Thibaut Courtois,Fellipe Luis na Diego Costa watu waliokuwa muhimu sana..
Lakini Simeone aliamua kubaki na hatimaye msimu wa 2015-2016 akafika fainali ya UEFA kwa mara ya pili japo alifungwa na hasimu wake yule yule Real madrid..Aliwasajili wachezaji imara sana kama Jan Oblack na Antoinne Grezman
Msimu huu Atletico imekuwa timu ya kawaida sana haswa ndani ya Champions league..Ilitolewa katika raundi ya makundi baada ya Chelsea na As Roma kuweza kupita kwenye kundi hilo ..Na hata waliposhushwa kuja kwenye Europa league sikuamini kama wangeweza kufika walipofika..
Hatimaye wamechukua taji
Huu ni wakati sahihi wa Diego Simeoni kutafuta changamoto mpya..Amewapa kila kitu Atletico kasoro UEFA champions league..
Ni muda wake wa kwenda kwenye vibarua vyenye pressure Zaidi na kukutana na wachezaji wakubwa Zaidi..Ni wakati wa kwenda kuifundisha Arsenal,Chelsea au hata Inter milan
Tatizo la Diego(El Cholo) ana moyo wa Atletico Madrid..sidhani kama ataondoka kirahisi
Jose aliwahi kusema kama angetaka kazi rahisi basi angesalia Fc Porto na kuwa mungu mtu pale..Lakini amemua kuondoka ili kusaka changamoto mpya.. Mpaka sasa baada ya kuondoka Porto amezunguka katika vilabu vingine vi 4 tofauti ambavyo ni Chelsea,Inter milan,Real Madrid na Manchester united
Hata Pep Guardiola aliwahi kusema “nahitaji changamoto mpya.nataka kutumia nafasi hii kuwa kocha pale uingereza nataka kuzoea hali ya uingereza...nina miaka 44 ni wakati sahihi ..kuna ofa lakini sijasaini yeyote mpaka
sasa..nitakapopata timu mpya nitawajuza nyote”
Kuna wakati mwanadamu unafika unahitaji changamoto mpya..Kwa mfano Pep 2012 aliona wazi kuwa wachezaji wa Fc Barcelona wote tayari wameshashinda kila kitu..
Hawakuwa na laziada wanalo hitaji..Yamkini walihitaji mwalimu mpya mwenye mbinu mpya ambaye angeweza kurudisha hamu yao ya ushindani kuwa maradufu..Pep alikwenda kupumzika Marekani
Hata jose alikwisha liona jambo kama hili… Isinge wezekana kirahisi kwa timu kama Porto kuweza kurudia mafanikio ya 2004..Jose aliangalia mbali Zaidi aliona jinsi ambavyo samaki wakubwa wangeitafuna Porto msimu uliofuata kwa kuwachukua wachezaji wake imara
Baada ya msimu wa 2013-2014 niliamini Diego Simeone angeondoka Atletico Madrid..Atletico walichukua La Liga na kufika fainali ya UEFA champions league na kufungwa na Real Madrid..Kwakuwa niliona Atletico ingewachukua muda kuweza kurudi katika ubora ..
Chelsea waliwachukua Thibaut Courtois,Fellipe Luis na Diego Costa watu waliokuwa muhimu sana..
Lakini Simeone aliamua kubaki na hatimaye msimu wa 2015-2016 akafika fainali ya UEFA kwa mara ya pili japo alifungwa na hasimu wake yule yule Real madrid..Aliwasajili wachezaji imara sana kama Jan Oblack na Antoinne Grezman
Msimu huu Atletico imekuwa timu ya kawaida sana haswa ndani ya Champions league..Ilitolewa katika raundi ya makundi baada ya Chelsea na As Roma kuweza kupita kwenye kundi hilo ..Na hata waliposhushwa kuja kwenye Europa league sikuamini kama wangeweza kufika walipofika..
Hatimaye wamechukua taji
Huu ni wakati sahihi wa Diego Simeoni kutafuta changamoto mpya..Amewapa kila kitu Atletico kasoro UEFA champions league..
Ni muda wake wa kwenda kwenye vibarua vyenye pressure Zaidi na kukutana na wachezaji wakubwa Zaidi..Ni wakati wa kwenda kuifundisha Arsenal,Chelsea au hata Inter milan
Tatizo la Diego(El Cholo) ana moyo wa Atletico Madrid..sidhani kama ataondoka kirahisi