Nyankurungu2020
JF-Expert Member
- Oct 2, 2020
- 4,170
- 6,757
Wanabodi hili ni bandiko la kuelezana ukweli,na kama viongozi wetu ni wakweli basi hakuna haja za kusubiri mpaka mei mosi ifike ili mishahara ya watumishi wa umma iongezwe.
Mwaka 2017 kwenye mkutano mkuu wa 33 wa ALAT jijini Dar es salaam rais JPM alisema hawezi kuongeza mishahara ya watumishi wa umma sababu uzalishaji ulikuwa chini na hivyo serikali ilikuwa bado na mzigo mkubwa kuwahudumia wananchi.
Rais JPM alisisitiza kuwa wananchi wanatakiwa wahimizwe kulipa kodi na kufanya shughuli za uzalishaji ili pato la taifa liongezeke.
Hivi sasa TRA wanakusanya Tril 2 kwa mwezi ongezeko ambalo ni kama 50% ya kusanyo la bil 800 walizokuwa wanakusanya wakati wa awamu ya nne. Hivyo ni dhahiri kuwa sasa uzalishaji umeongezeka kama alivyotaka Rais JPM. Na kwa mantiki hii serikali inaouwezo wa kuongeza mishahara huku ikiwahudumia wananchi vizuri tu bila shida.
Ni aibu kubwa kwa taifa ambalo limeingia uchumi wa kati,huku mfumuko wa bei upo juu na kuna Mtanzania analipwa sh 390000 kama basic pay. Akikatwa kodi anabaki na sh 360000. Hapo mtu utaweza kuishi kwa raha?
My take; TUCTA na vyama vya upinzani viibane serikali ili iwakumbuke kupandisha mishahara watumishi wanaohangaika kwa kipato kidogo huku kila siku wanasota kuwatumikia wananchi.
Mwaka 2017 kwenye mkutano mkuu wa 33 wa ALAT jijini Dar es salaam rais JPM alisema hawezi kuongeza mishahara ya watumishi wa umma sababu uzalishaji ulikuwa chini na hivyo serikali ilikuwa bado na mzigo mkubwa kuwahudumia wananchi.
Rais JPM alisisitiza kuwa wananchi wanatakiwa wahimizwe kulipa kodi na kufanya shughuli za uzalishaji ili pato la taifa liongezeke.
Hivi sasa TRA wanakusanya Tril 2 kwa mwezi ongezeko ambalo ni kama 50% ya kusanyo la bil 800 walizokuwa wanakusanya wakati wa awamu ya nne. Hivyo ni dhahiri kuwa sasa uzalishaji umeongezeka kama alivyotaka Rais JPM. Na kwa mantiki hii serikali inaouwezo wa kuongeza mishahara huku ikiwahudumia wananchi vizuri tu bila shida.
Ni aibu kubwa kwa taifa ambalo limeingia uchumi wa kati,huku mfumuko wa bei upo juu na kuna Mtanzania analipwa sh 390000 kama basic pay. Akikatwa kodi anabaki na sh 360000. Hapo mtu utaweza kuishi kwa raha?
My take; TUCTA na vyama vya upinzani viibane serikali ili iwakumbuke kupandisha mishahara watumishi wanaohangaika kwa kipato kidogo huku kila siku wanasota kuwatumikia wananchi.