Ni wapi au kampuni gani inajishuhulisha na uuzaji wa kuku aina hii ya Chotara Kuroiler ambao ni uzao wa kwanza F1?

Ni wapi au kampuni gani inajishuhulisha na uuzaji wa kuku aina hii ya Chotara Kuroiler ambao ni uzao wa kwanza F1?

Afrika_Bora

Member
Joined
Oct 20, 2020
Posts
77
Reaction score
159
Kuroiler ni kuku Chotara ambae hupatikana kwa kupandishia kuku wa jamii mbili tafauti ili kupata matokeo mazuri zaidi ukilinganisha na kuku wa kawaida.

Matokeo hayo ni pamoja na kutaga mayai mengi au/na pia kuwa na miili mikubwa kwaajili ya nyama.

Hivyo kumfanya mfugaji wa kibishara kupata kipato kizuri kabisa.

Kila penye fursa huwa hapakosi upigaji. Kutokana na shuhuda mbali mbali kutoka kwa wafugaji ni kwamba ili upate faida nzuri kupitia kuku hawa, unahitajika kuwa na kuku wale wa Uzao wa kwanza (First filial generation "F1") au wanao karibiana na hawa, yaani F2.
Ikiwa na maana kila uzao unavokwenda mbele ndio matokeo mazuri kibiashara hupungua.

SWALI : Ni wapi au kampuni gani inajishuhulisha na uuzaji wa kuku aina hii ya Chotara Kuroiler ambao ni uzao wa kwanza F1 ?

Karibuni wadau tujadili na tupeane taarifa pia maarifa sahihi kwaajili ya ufugaji wa kibiashara na kujikwamua kiuchumi .
 
Nenda jkt ruvu utapata kila aina ya kuku na vifaa vya aina zote pia seminar elekezi kwa kiwango kikubwa kisicho cha kiraia raia
Asante mkuu.. Kama una contacts zao ama page zao za mtandaoni unaweza kunipatia kama hatua ya mwanzo
 
Hivi hawa Kuroiler, jike anaweza kupandwa na jogoo wakienyeji na akataga mayai pia vp kuhusu jogoo wa kuroler anaweza kumpanda mtetea wakienyeji na akataga AU NILAZIMA WAPANDANE QENYEWE KWA WENYEWE?
 
Hivi hawa Kuroiler, jike anaweza kupandwa na jogoo wakienyeji na akataga mayai pia vp kuhusu jogoo wa kuroler anaweza kumpanda mtetea wakienyeji na akataga AU NILAZIMA WAPANDANE QENYEWE KWA WENYEWE?
Ndio inawezekana
 
Back
Top Bottom