Ni wapi katika katiba au sheria inayopiga marufuku sheria za Kiislam au za Kikiristo kutumika nchini?

Ni wapi katika katiba au sheria inayopiga marufuku sheria za Kiislam au za Kikiristo kutumika nchini?

Mohamed Abubakar

JF-Expert Member
Joined
Jun 26, 2014
Posts
984
Reaction score
1,179
Tamko la rais (decree) anapolitoa huwa ni sheria. Kinachofanyoka hutungiwa mwongozo wa mipaka ya matumizi yake.

Wakati rais wa awamu ya pili aliporuhusu mabinti wa kiislam kuvaa hijab, wako wakimpinga sheria hii wakinukuu kifungu cha katiba kuwa serikali haina dini.

Wasichoelewa ni kuwa si taifa halina dini, bali serikali ndio haina dini. Serikali ni sehemu ya tu ya kitu kinachoitwa taifa.

Na kwamba kikatiba wananchi wana haki ya kutumia sheria za kimila, kidini na sheria zinatungwa na wananchi kupitia bunge na Tamko la Rais (decree).

If that is a case ni kwa sheria au kifungu gani cha katiba kinachopiga marufuku kutumika sheria za kiislam au kikristo.

Kama serikali yetu ni ya kijamaa. Na Ujamaa ni imani Na dini ni imani.

Hii ina maana Ujamaa ni dini. Hivyo kama kuna sheria inapiga marufuku sheria za dini.

Bali kwa sheria hiyo hiyo inapaswa kutumika kupiga marufuku sheria za imani au dini ya Ujamaa
 
Back
Top Bottom