Ni wapi katika Mkoa wa Dodoma na Wilaya zake panapoweza kulimwa alizeti kwa tija?

Ni wapi katika Mkoa wa Dodoma na Wilaya zake panapoweza kulimwa alizeti kwa tija?

Joined
Mar 11, 2021
Posts
35
Reaction score
31
Ndugu wanajamvi,

Nimehamasika sana na ushauri uliotolewa hivi karibuni na mh. Waziri mkuu Majaliwa kwamba sasa ni zamu ya watanzania kutajirika kupitia zao la alizeti.

Naamini huu ushauri umekuja baada ya hali ya bei ya mafuta inchini kupanda sana kwa kipindi kifupi.

Mimi ninaishi Arusha lakini nina mpango wa kuhamia Dodoma kwa shughuli zangu za kibiashara lakini pia natamani sana kuanzisha kilimo cha alizeti kutokana na hii hamasa ya mheshimiwa PM. Lakini pia kwa ukweli kwamba mafuta bado hatujitoshelezi kama inchi kwani sehemu kubwa bado tunaagiza nje.

Wadau wenye uzoefu najua humu mpo ndio maana nimekuja ili nipate mawili matatu ili kujua kama ninachokiwaza kufanyia hapo dom kinafaa au la.

Asanteni.
 
Ndani ya halmashauri ya jiji la Dodoma lenyewe panafaa, wilaya ya kongwa na wilaya ya mpwapwa bila kuacha wilaya ya chamwino. Ingawaje koote huko hutegemea mvua. Karibu Dodoma
 
Dodoma sehemu zote zinavaa cha msingi mvua ,kama unaweza fanya kilimo cha umwagiliaji pia kwa uhakika zaidi.Maana alizeti haiitaji mvua nyingi.
 
Ndugu wanajamvi,

Nimehamasika sana na ushauri uliotolewa hivi karibuni na mh. Waziri mkuu Majaliwa kwamba sasa ni zamu ya watanzania kutajirika kupitia zao la alizeti.

Naamini huu ushauri umekuja baada ya hali ya bei ya mafuta inchini kupanda sana kwa kipindi kifupi.

Mimi ninaishi Arusha lakini nina mpango wa kuhamia Dodoma kwa shughuli zangu za kibiashara lakini pia natamani sana kuanzisha kilimo cha alizeti kutokana na hii hamasa ya mheshimiwa PM. Lakini pia kwa ukweli kwamba mafuta bado hatujitoshelezi kama inchi kwani sehemu kubwa bado tunaagiza nje.

Wadau wenye uzoefu najua humu mpo ndio maana nimekuja ili nipate mawili matatu ili kujua kama ninachokiwaza kufanyia hapo dom kinafaa au la.

Asanteni.
Ndugu, matamko ya wanasiasa mzuri sana. Chunguza nawew kwanza kabla ya kwenda na kauli zao. Usishangae mwakani wakaingiza mafuta ya kula
 
Tatizo alizeti no Bei kuwa ndogo kuliko gharama za kulima...Dodoma yote inafaa kulima alizeti
 
Back
Top Bottom