Ni wema gani uliwahi kuutenda ukaishia kujuta mpaka leo

Ni wema gani uliwahi kuutenda ukaishia kujuta mpaka leo

Nakumbuka nikiwa zangu msasani beach tumelala kwenye bot bovu alikuja jamaa anakimbia usiku tukamuuliza vipi, akasema kuna maaskari wametimba maskani kukamata wahalifu, basi ilikuwa kama saa tano usiku tukampa hifadhi, ilipo fika kesho asubuhi tukakuta hayupo na kaondoka na viatu vyetu.
Mnahitaji viatu vya nini baharini, muache aende navyo.
 
Wema hauozi, unaweza usione faida yake sasa ila baadae utaleta faida kwako au kwa watu wako wa karibu.
Mkuu usijidanganye. Mmatumbi hata ukimsaidiaje. Kwa mmatumbi haki ya nani wema unaoza.
 
[emoji848][emoji848][emoji848]
 
Ukimuungisha mshikaji anaifanya kazi yako kishikaji pia
 
Nakumbuka nikiwa zangu msasani beach tumelala kwenye bot bovu alikuja jamaa anakimbia usiku tukamuuliza vipi, akasema kuna maaskari wametimba maskani kukamata wahalifu, basi ilikuwa kama saa tano usiku tukampa hifadhi, ilipo fika kesho asubuhi tukakuta hayupo na kaondoka na viatu vyetu.
..Mkuu, kumbe Umeanza mbali! Umelala kwenye Maboti Mabovu??
 
MTU mmoja rafiki yangu alikuja kunililia hitaji la mkopo wa tsh 350,000/- ili arudishe ndani ya wiki mbili tangu 2017 hadi leo hajawahi kukumbuka kurejesha fedha hiyo badala take akawa adui mkubwa nilipo mkumbusha deni hilo.
 
Umenikumbusha mbali sana na jaribu kubwa maishani mwangu.

Nikiwa nimemaliza chuo kikuu na kupata ajira serikalini huko Magharibi ya nchi. Kufika huko nikakuta viwanja na mshamba bei rahisi nikanunua mashamba na viwanja. Baada ya mwaka mmoja nikaanza kuinua pagale na kufanikiwa kumaliza ndani ya miaka miwili.

Nilipomaliza nikaanza kujenga fence ya tofali za kuchoma. Sasa jamaa yangu mmoja akanishauri nitafute vijana wa kunichomea tofali ili kupunguza gharama. Nikapata watatu wakawa wanapiga kazi wakati huo mimi nipo nyumba ya kupanga. Nikawaambia wakae kwangu.

Wakamaliza kazi mmoja nikamwambia akae nami. Jamaa nikawa namlisha, mvalisha na anakaa kwangu bure kwani nilikuwa nasafiri safiri kikazi na sikuwa nimeoa wakazi huo. Jamaa akavuta mke nikawa nawalisha na kuwavalisha. Mke akiumwa mimi natumia pesa za matibabu.

Nikaja kuoa na kupata mtoto nikasema sasa nikakae kwangu na mke na mtoto. Yeye jamaa alishindwana na mkewe akaondoka. Nikawa naishi naye na mke wangu na mtoto wangu ili nikisafiri awape kampani. Sasa nikirudi mke wangu ananiambia huyu jamaa anasema anataka akupeleke kwa mganga ili upendwe na upandishwe cheo kazini. Wakati huo nilikuwa siamini uchawi nikawa napuuzia. Sasa kuna siku si chini ya mara tatu nikiwa nipo nyumbani nasikia harufu ya udi/uvumba ule wa kupandisha mashetani usiku wa manane. Namuuliza unafanya nini akaniambia anatambika mizimu. Aiseee, nikamfukuza. Akaondoka kwa hasira kisha akanitumia sms kuwa ananichukia na kwamba nitaona si nina jivunia kazi niliyonayo? Nikampuuzia. Siku 1 usiku nipo kwangu naona pikipiki imekuja na kuishia getini kisha ikaondoka. Nikapuuzia asubuhi nikapita pale getini na kwenda kazini.

Hapo ndipo mateso yangu yalipoanza hadi kuacha kila kitu na kukimbia mkoa ule japo ulinikubali na kunifanya nishike pesa... Nikiona jamaa wanasema humu kuwa hakuna uchawi huwa nawaangalia tu,............. Itaendelea
 
Nakumbuka nikiwa zangu msasani beach tumelala kwenye bot bovu alikuja jamaa anakimbia usiku tukamuuliza vipi, akasema kuna maaskari wametimba maskani kukamata wahalifu, basi ilikuwa kama saa tano usiku tukampa hifadhi, ilipo fika kesho asubuhi tukakuta hayupo na kaondoka na viatu vyetu.
Way back 2017 nikiwa katika project za ujenzi.
Enzi hizo Jiwe yupo on pick ya kutumbua tumbua watu.
Nilikuwa mtaalamu sana wa kusuka na kutengeneza matenki ya maji. ([emoji16]Siyo haya ya simtank ni ya miradi ya maji)

Sasa akatokea jamaa mmoja hivi engineer (DWE) akawa analeta ujuaji mwingi mixer kujifanya kasoma sana akawa analeta mbwembwe za darasani. (Miradi mingi ya maji mafundi wa mitaani ndiyo wapo competition kuliko wasomi, Kampuni nyingi zinatumia mafundi kusuka na kutengeneza na ikiwezekana ushauri wa kitaalamu)

Kila nikumuelewesha anajifanya machinoo, muhuni nikakaa pembeni kuhepusha kuonekana bashite.

Lahaula zimebaki siku chache mradi ukamilishwe tanki likawa Linavuja na Maji yakawa hayana presha ya kupanda juu ya tank [emoji38].

DWE akanitafuta kusema anaomba msaada wangu na blaha blaha kibaoo,maana Kipindi hicho waziri alikuwa on fire kweli kutumbua tumbua.

Mwamba nikaamua kufoji na kufoji na kukubali kubebeshwa zigo lote.

[emoji16]Ajabu siku anakuja Eng Lwenge ndiyo alikuwa waziri wa maji wakati huo.
mwamba nikashangaa ana nisnitch kuwa kampuni YETU imeshindwa kutekeleza mradi na blaha blaha kibao.

Kilichotokea Serikali ikagoma kutulipa pesa zetu (Enzi hizo ulikuwa unajenga kwa pesa yako, mradi ukishakamilika ndiyo unalipwa chako).
 
Achana na ndugu zake, usiingilie undugu wa watu! Damu nzito kuliko nyoraa
ndugu wa Mzee ni ndugu zangu mkuu.
nikimuona Mzee anasikitika/kuumwa pale ambapo huyasikia wanayoyasema/kuyafanya juu yake na uhalisia naujua ...huwa sifurahii

Effect yake mwenye kufanya hivyo ni mwenye kuiumiza familia yetu ....siwezi kumtazama huku nikikenua Meno .......kwangu namchukulia kama adui na c ndugu.
 
Back
Top Bottom