Lord OSAGYEFO
JF-Expert Member
- Feb 19, 2021
- 3,085
- 4,890
Wadau naomba kujua yafuatayo juu ya sifa za kuteuliwa Ukuu wa Wilaya na KAZI za MKUU wa WILAYA.
1. Elimu
2. Umri
3. Ujuzi
4. Itikadi
5. Uzoefu
Ili tusiwalaumu walioteuliwa kumbe wanasifa sahihi.
Pia je, kama sio Watumishi Taarifa zao zinapatikana Wapi maana hawana MAFAILI.
====
1. Elimu
2. Umri
3. Ujuzi
4. Itikadi
5. Uzoefu
Ili tusiwalaumu walioteuliwa kumbe wanasifa sahihi.
Pia je, kama sio Watumishi Taarifa zao zinapatikana Wapi maana hawana MAFAILI.
====
MAJUKUMU YA MKUU WA WILAYA
(i) Kumweka mtu kizuizini kwa muda wa saa 48 mfululizo iwapo atashukiwa kuwa ni mhalifu au anayehatarisha hali ya utulivu na Amani (Sheria ya tawala za mikoa Na 19/1997).
(ii) Kufungisha ndoa za serikali (Law of Marriage Act No 5/1971).
(iii) Kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa, kuwa mwenyekiti wa Kamati yaMkoa inayochambua maombi ya watu wanaotaka kuuza madawa ya sumu (Pharmaceuticals and Poisons Act No 9/1978).
(iv) Kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa, kuongoza Kamati ya kusikiliza rufani za leseni za biashara mkoani (Business Licensing Authority Act No 25/1972, ib. 1).
(v) Kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa, kuwa mwenyekiti wa Kamati ya Rufaa ya leseni za vileo (Intoxicating Liquours Act No 28/1968)
(vi) Kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa, kuteua wakaguzi wa magereza (Prisons Act No 34/1967, ib. 100).
(vii) Kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa, kuwashughulikia watu wanaodhaniwa kuwa ni wachawi (Witchcraft Ordinance Cap 18).
(viii) Kuwa mhimili msaidizi wa Halmashauri za Wilaya (Sheria Na 7/1982).
(ix) Kuwa mwenyekiti wa Kamati mbalimbali zitakazoundwa Wilayani.
(x) Kuhudhuria vikao vya Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kamamjumbe.
(xi) Kushughulikia malalamiko ya wananchi na kuyapatia ufumbuzi.
(xii) Kumsaidia Mkuu wa Mkoa katika kuzisimamia Halmashauri za Wilaya na kuhakikisha kuwa zinatoa huduma nzuri kwa wananchi na kwa ufanisi
(xiii) Kuziwekea Halmashauri za Wilaya mazingira mazuri na kuhakikisha kuwa zinatekeleza majukumu yake kulingana na sera za serikali.
(xiv) Kutekeleza majukumu yote atakayopewa kisheria au kukasimiwa na Mkuu waMkoa.
From random individual somewhere in facebook