Pole mkuu. Mimi pia nina story kama hii ya kwako, japo ya kwako ni cha mtoto ukilinganisha na ya kwangu. Kuna dada mmoja tunayefahamiana japo si karibu sana alikuwa na shida akaniomba nimkopeshe pesa. Nikamkopesha na nikaahidiwa ningerudishiwa mwezi unaofuata. Mwezi ukaisha nikaanza kupewa series ya matatizo aliyonayo (nahisi ilikuwa ni namna ya kuniambia nisimdai tena), mara ana harusi ya ndugu yake mara ana mgonjwa mara hiki mara kile na sikumwambia chochote. Ikapita kama miezi 2 hivi akaja na shida nyingine ya dharura akaomba nimkopeshe tena na nikaahidiwa ningerushiwa baada ya miezi miwili mpaka sasa sijarudishiwa. Kwa jumla namdai zaidi ya Tshs. 2.6 mil. Dada mwenyewe ana kazi nzuri sana yenye mshahara usipoungua Tshs. 1.9 mil. kwa mwezi. Nimemkumbushia mara kadhaa jibu ninalopewa nivumilie kidogo. Lol! Sasa najiuliza huyu dada yangu anafikiri mimi sijihitaji hizo pesa jamani? Na mimi niliahirisha mipango yangu baada ya kuhakikishiwa ningezipata tu bila shida. Kwa kweli amenipa somo, na nahisi ana ajenda ya siri sasa.