NIDA kutaka kusitisha matumizi ya namba za utambulisho haitasaidia, tumieni njia mbadala ya usambazaji, wananchi hawajakaidi kuvichukua

NIDA kutaka kusitisha matumizi ya namba za utambulisho haitasaidia, tumieni njia mbadala ya usambazaji, wananchi hawajakaidi kuvichukua

The Watchman

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
896
Reaction score
1,427
Hili la kutaka kufungia namba za utambulisho wazee mnazingua, wananchi hawajagoma kuchukua vitambulisho vyao.
***
Mamlaka ya vitambulisho vya taifa NIDA leo imetangaza kuwa itasitisha matumizi ya namba za utambulisho za wananchi ambao hawatachukua vitambulisho vyao baada ya kutumiwa ujumbe mfupi ndani ya siku 30.

Soma pia: NIDA kusitisha matumizi ya namba kwa wasiofuata vitambulisho vyao

Taarifa hii inakuja mara baada ya mamlaka hiyo kuzalisha vitambulisho hivyo na kuvisambaza katika maeneo ambako wananchi walijiandikisha ambapo muitikio wa wananchi kwenda kuchukua umekua hafifu sana.

Mamlaka inatangaza kusitisha matumizi ya namba hizo kwa watu watakaokaidi kwa muda uliotolewa, kwani tatizo ni wananchi kwamba wamegoma kuvichukua? Au mamlaka yenyewe imekosa ubunifu wa njia sahihi ya kuwafikia wananchi walipo?

Mfano mzuri pengine mtu alijiandikisha akiwa Bukoba mwaka 2019, katika harakati za utafutaji anapata mishemishe mkoa mwingine mfano Njombe, leo kitambulisho cha NIDA kimetoka kinapelekwa Bukoba, Je mtu huyu atakubali kwenda Bukoba kwa kutumia gharama kubwa kufuata kitambulisho tu na kuacha kibarua chake kiyeyuke au kazi kusimama? Pitieni hata maoni ya wananchi katika kurasa zenu hili linalalamikiwa.

Kuvifungia matumizi namba hizo si suluhisho kwamba wananchi wataenda kuvifuata, asilimia kubwa ya ambao hawajachukua ni wale ambao wapo mbali na maeneo yao waliyojiandikishia.

Ninawashauri NIDA wasiachwe nyuma na teknolojia, wawasiliane na watu ambao hawajachukua vitambulisho ili kujua maeneo walipo, ili ofisi zilizo karibu yao zitumike kutoa vitambulisho hivyo. Inaweza kuwa kwa kutumia ujumbe mfupi au kupiga simu au katika mfumo wa tovuti ya mamlaka iwekwe sehemu ambayo itamruhusu mtu kuchagua kitambulisho chake akakichukulie wapi tofauti na alipojiandikishia.

Igeni kutoka kwa benki mbalimbali, kadi inaweza ikamezwa Singida ATM ukiwa safarini lakini kesho yake ukiwapigia customer care watakuuliza upo wapi kadi yako iletwe karibu na tawi lao ulilopo hata kama ni Songea huko.
 
Usitutishe
By Malhum Maalim Seif Sharif Hamad
 
NIDA wanaposema wananchi wanakaidi kuchukua vitambulisho vyao si kweli, hiyo nyaraka ni muhimu kama ilivyo vyeti vya shule/chuo. Kusitisha matumizi ya namba hizo wakati zinatumika ni dhahiri wenye vitambulisho wapo hai ila wapo mbali sana na walikojiandikisha. Unakuta mtu alijiandikisha kilimanjaro kabla havijatoka akahamia mtwara, ni shughuli pevu kusafiri kutoka mtwara kufuatilia kitambulisho chake alikojiandiksha kilimanjaro. Hebu NIDA watoe walau miezi mitatu wananchi wafuatilie vitambulisho vyao huko mbali walikojiandikisha. NIDA wapitie maoni ya wanachi mitandaoni kuona ni namna gani wata solve kadhia hii kuliko kuwakurupusha tu ndani ya mwezi mmoja wasitishe matumizi ya namba huo utakuwa ni usumbufu mkubwa kwa wananchi, hakuna anayekaidi kuchukua kitambulisho chake
 
NIDA wanaposema wananchi wanakaidi kuchukua vitambulisho vyao si kweli, hiyo nyaraka ni muhimu kama ilivyo vyeti vya shule/chuo. Kusitisha matumizi ya namba hizo wakati zinatumika ni dhahiri wenye vitambulisho wapo hai ila wapo mbali sana na walikojiandikisha. Unakuta mtu alijiandikisha kilimanjaro kabla havijatoka akahamia mtwara, ni shughuli pevu kusafiri kutoka mtwara kufuatilia kitambulisho chake alikojiandiksha kilimanjaro. Hebu NIDA watoe walau miezi mitatu wananchi wafuatilie vitambulisho vyao huko mbali walikojiandikisha. NIDA wapitie maoni ya wanachi mitandaoni kuona ni namna gani wata solve kadhia hii kuliko kuwakurupusha tu ndani ya mwezi mmoja wasitishe matumizi ya namba huo utakuwa ni usumbufu mkubwa kwa wananchi, hakuna anayekaidi kuchukua kitambulisho chake
Wavute subra na kuona namna ambayo watawafikia wananchi popote walipo
 
Wavute subra na kuona namna ambayo watawafikia wananchi popote walipo
maana hata huko waliko wananchi wamefuatilia kuona ni kwa namna gani watapata vitambulisho kwa local office za NIDA hujibiwa haiwezekani kuletewa waliko ni mpaka waende walikojiandikisha
 
Mawqzo ya kijinga kabisa haya, Je kama mru kapoteza kitambulisho?
 
Ila NIDA kwakweli hebu muwe unatumia hata utu kidogo............. Sie tumewavumilia zaidi ya miaka mitatu kusubiri vitambulisho hivyo,nayie pia muwe na subira tu,kwani kuna wamepatia namba mkoa mwingine na sasa yupo mkoa mwingine hata nauli tu ya kutoka sehemu A kwenda B.... Hivyo tunaomba busara itumike hali ni ngumu sana jamani
 
NIDA imekosa ubunifu, namba za simu wanazo, lakini hawatoi taarifa kwamba kitambulisho kiko tayari, na kiko wapi
 
Hili la kutaka kufungia namba za utambulisho wazee mnazingua, wananchi hawajagoma kuchukua vitambulisho vyao.
***
Mamlaka ya vitambulisho vya taifa NIDA leo imetangaza kuwa itasitisha matumizi ya namba za utambulisho za wananchi ambao hawatachukua vitambulisho vyao baada ya kutumiwa ujumbe mfupi ndani ya siku 30.

Soma pia: NIDA kusitisha matumizi ya namba kwa wasiofuata vitambulisho vyao

Taarifa hii inakuja mara baada ya mamlaka hiyo kuzalisha vitambulisho hivyo na kuvisambaza katika maeneo ambako wananchi walijiandikisha ambapo muitikio wa wananchi kwenda kuchukua umekua hafifu sana.

Mamlaka inatangaza kusitisha matumizi ya namba hizo kwa watu watakaokaidi kwa muda uliotolewa, kwani tatizo ni wananchi kwamba wamegoma kuvichukua? Au mamlaka yenyewe imekosa ubunifu wa njia sahihi ya kuwafikia wananchi walipo?

Mfano mzuri pengine mtu alijiandikisha akiwa Bukoba mwaka 2019, katika harakati za utafutaji anapata mishemishe mkoa mwingine mfano Njombe, leo kitambulisho cha NIDA kimetoka kinapelekwa Bukoba, Je mtu huyu atakubali kwenda Bukoba kwa kutumia gharama kubwa kufuata kitambulisho tu na kuacha kibarua chake kiyeyuke au kazi kusimama? Pitieni hata maoni ya wananchi katika kurasa zenu hili linalalamikiwa.

Kuvifungia matumizi namba hizo si suluhisho kwamba wananchi wataenda kuvifuata, asilimia kubwa ya ambao hawajachukua ni wale ambao wapo mbali na maeneo yao waliyojiandikishia.

Ninawashauri NIDA wasiachwe nyuma na teknolojia, wawasiliane na watu ambao hawajachukua vitambulisho ili kujua maeneo walipo, ili ofisi zilizo karibu yao zitumike kutoa vitambulisho hivyo. Inaweza kuwa kwa kutumia ujumbe mfupi au kupiga simu au katika mfumo wa tovuti ya mamlaka iwekwe sehemu ambayo itamruhusu mtu kuchagua kitambulisho chake akakichukulie wapi tofauti na alipojiandikishia.

Igeni kutoka kwa benki mbalimbali, kadi inaweza ikamezwa Singida ATM ukiwa safarini lakini kesho yake ukiwapigia customer care watakuuliza upo wapi kadi yako iletwe karibu na tawi lao ulilopo hata kama ni Songea huko.
Dash! Tizedi bana, wao ndo wanafanya mambo yawe magumu,, yaani wametengeneza tatizo afu wamekosa ufumbuzi
 
maana hata huko waliko wananchi wamefuatilia kuona ni kwa namna gani watapata vitambulisho kwa local office za NIDA hujibiwa haiwezekani kuletewa waliko ni mpaka waende walikojiandikisha
Sasa huu ni udhaifuu watafakari vizuri hapa
 
NIDA imekosa ubunifu, namba za simu wanazo, lakini hawatoi taarifa kwamba kitambulisho kiko tayari, na kiko wapi
Pia wampe option mtu ya kuchagua achukulie wapi kitambulisho ili kurahisisha kuwafikia watu wengi
 
Back
Top Bottom