NIDA mmeongeza nyaraka za kukabidhi ili kupata Kitambulisho cha Taifa. Hii ni halali kweli? | NIDA wafafanua, wataja vitu vitatu muhimu kuwa navyo

NIDA mmeongeza nyaraka za kukabidhi ili kupata Kitambulisho cha Taifa. Hii ni halali kweli? | NIDA wafafanua, wataja vitu vitatu muhimu kuwa navyo

BabaMia

JF-Expert Member
Joined
Jan 7, 2024
Posts
270
Reaction score
554
Mwanzoni walihitaji kitambulisho cha kura, baadaye wakahitaji cheti cha kuzaliwa. Na kwasasa wanahitaji tuwe na:

Cheti cha kuzaliwa
Cheti kutoka Migration
Cheti cha kidato cha nne
Cheti cha darasa la saba.

Uwe navyo vyote. Ni halali kweli hii?

======
JamiiForums, imezungumza na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Geofrey Tengeneza kufahamu iwapo wameongeza nyaraka za kukabidhi ili kupata Kitambulisho cha Taifa (NIDA) ambaye ameeleza kuwa taarifa hiyo haina ukweli na siyo sahihi.

"Hiyo siyo kweli na siyo sahihi kabisa, vitu va msingi kabisa kwa jaili ya kusajili kupata kitambulisho cha NIDA ni:-
  • Cheti cha kuzaliwa cha mtu anayeomba analeta nakala
  • Cheti cha kuzaliwa(nakala) cha mzazi mmojawapo, baba au mama, na kama hawana hicho cheti cha kuzaliwa kama wana kitambulisho cha NIDA cha mzazi mmjowapo baba au mama basi unaambatanisha nakala ya cheti cha NIDA cha mzazi mmojawapo baba au mama. Na kama hawana vyote hivyo cheti cha kuzaliwa au nakala ya NIDA basi unakwenda kwa mwanasheria au mahakamani, anakupa kiapo unaapa kwa jina kinaitwa affidavit kwa ajili ya mzazi mmoja wapo, unaapa kisha unaambatanisha hiyo affidavit.
  • Kitu cha tatu cha msingi ni barua ya Serikali za mtaaa unakoishi, kwa hiyo lazima uwe na barua ya Serikali za mtaa unakoishi wanaeleza kwamba wanakutambua kama mkazi katika huo mtaa katika lile eneo.
Kwa hiyo hivi ndio vitu vitatu vya msingi sasa hivi vitu vingine vitu unaweza ukaambiwa kama cheti cha mpiga kura nakala, ama leseni ya udereva, cheti cha elimu ya msingi au sekondari hivi ni vitu vya nyongeza tu ili kutia uzito maombi yako, lakini siyo vitu vya msingi, lakini haina maana kama ukiwa huna hivyo hautasajiliwa, hata kama huna hivyo na unavyo vile vitu vitatu vya msingi, kama cheti cha kuzaliwa, checti cha kuzaliwa cha mzazi au kadi yake ya NIDA au affidavit na barua ya serikali za mtaa basi utasajiliwa tu.

Hivo vitu vingine ni vitu tu vya kuongeza kama utakuwa navyo mwenyewe kutia nguvu maombi yako na si kwamba kama utakuwa hauna hiyo vya kuongezea hautasajiliwa hiyo si kweli, hata kama huna hivyo vya kuongezea utasajiliwa tu". Geofrey Tengeneza Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA)

Pia soma:Vitu 3 muhimu vya kuwa navyo unapoomba Kitambulisho cha Taifa (NIDA)
 
Mwanzoni walihitaji kitambulisho cha kura,baadaye wakahitaji cheti cha kuzaliwa. Na kwasasa wanahitajivuwe na
Cheti cha kuzaliwa
Cheti kutoka Migration
Cheti cha kidato cha nne
Cheti cha darasa la saba.
Uwe navyo vyote . Ni halalu kweli hii?
Nani hao wanaohitaji hivyo vyeti, na immigration inatowa vyeti gani?
 
Nani hao wanaohitaji hivyo vyeti, na immigration inatowa vyeti gani?
Kuna saini inahitajika kutoka uhamiaji,baada ya Mtendaji na Mwenyekiti. Pia uwe na cheti cha kuzaliwa pamoja na cha shule ya msingi darasa la saba au kidato cha nne. Hivyo vyote uambatanishe pamoja. Ina maana kama hujasoma huwezi kukipata kwa sasa?
 
Kuna saini inahitajika kutoka uhamiaji,baada ya Mtendaji na Mwenyekiti. Pia uwe na cheti cha kuzaliwa pamoja na cha shule ya msingi darasa la saba au kidato cha nne. Hivyo vyote uambatanishe pamoja. Inamaana ksma hujasoma huwezi kukipata kwa sasa?
Sio vyote nadhani hukuelewa. Form unayochukua nida baada ya kujaza kuna sehemu uhamiaji wanasaini na si cheti kama unavosema. Viambatanishi ni cheti cha kuzaliwa au cheti kingine kilichoorodheshwa
 
Kuna saini inahitajika kutoka uhamiaji,baada ya Mtendaji na Mwenyekiti. Pia uwe na cheti cha kuzaliwa pamoja na cha shule ya msingi darasa la saba au kidato cha nne. Hivyo vyote uambatanishe pamoja. Inamaana ksma hujasoma huwezi kukipata kwa sasa?
Wamepenyezewa taarifa kuna wageni toka Nchi zingine HUKO wanapewa vitambulisho vya NIDA kihorela na SIO raia wa Tanzania, uzi UPO HUMU kule Fichua Maovu kwa HIO wanafanyia kazi
 
Mwanzoni walihitaji kitambulisho cha kura, baadaye wakahitaji cheti cha kuzaliwa. Na kwasasa wanahitaji tuwe na
Cheti cha kuzaliwa
Cheti kutoka Migration
Cheti cha kidato cha nne
Cheti cha darasa la saba.
Uwe navyo vyote . Ni halali kweli hii?
Mwendokasi imewashinda waweze NIDA .Team kataa ccm wakati sasa
 
SIjui hii batch iliyotoka sasa ya vitambulisho vya NIDA ili printiwa wapi. Kitambulisho ukikiweka mfukoni kinabanduka maandishi yote, unabakiwa na kadi tu isiyokuwa na maandishi yeyote.
 
Mh! Mkuu we umejichanganya NIDA ukijaza kitu hakikisha unacho ukijaza namba ya nida ya mzazi hakikisha unakopi ya kitambulisho sasa wewe ukute ulijaza unavyo ndio maana wakavihitaji.. muhimu uwe na cheti cha kuzaliwa vyeti vya shule si muhimu sana hata ukiacha kujaza,nafikiri ni uelewa by the way take it easy
 
mh! mkuu we umejichanganya nida ukijaza kitu hakikisha unacho ukijaza namba ya nida ya mzazi hakikisha unakopi ya kitambulisho sasa wewe ukute ulijaza unavyo ndio maana wakavihitaji.. muhimu uwe na cheti cha kuzaliwa vyeti vya shule si muhimu sana hata ukiacha kujaza,nafikiri ni uelewa by the way take it easy
mh! mkuu we umejichanganya nida ukijaza kitu hakikisha unacho ukijaza namba ya nida ya mzazi hakikisha unakopi ya kitambulisho sasa wewe ukute ulijaza unavyo ndio maana wakavihitaji.. muhimu uwe na cheti cha kuzaliwa vyeti vya shule si muhimu sana hata ukiacha kujaza,nafikiri ni uelewa by the way take it easy
Exactly
 
Kwa tuliozaliwa mikoa ya mipakani ni shida sana, ID ikitoka ukienda kuchukua unaambiwa nenda kwanza Ofisi ya Uhamiaji,ukifika huko unaanza kupigwa maswali,majina matatu,mtaa,kata,wilaya na mkoa uliozaliwa,majina matatu ya wazazi wote wawili na sehemu walipozaliwa,elimu yako,na mwishoni unaulizwa kwani unahitaji ID ya kazi gani.Ukijibu unapewa kikaratasi kimepigwa muhuri kabisa kuwa mpeni ID
 
Back
Top Bottom