Mbavu za Mbwa
JF-Expert Member
- Jan 2, 2011
- 303
- 154
Wana bodi! Ni hadithi ndefu sana, ila kwa ufupi wake ni kuwa mtumishi mwenzangu tunaefanya kazi ofisi moja na desk moja amemuweka kimada aliyekuwa mpenzi wangu kwa miaka 4 na ofisi nzima wanamjua. Nilijaribu kumsihi huyu jamaa kuwa asitishe uhusiano wao kwa kuwa unaweza kutuvuruga, hakukubali. Simuonei wivu kabisa, hofu yangu ni kuwa; Je, hakuna uwezekano wa kujengeka uadui kati yangu na huyu jamaa? Ukizingatia, nyumba wanayoishi ndipo kuna duka langu na huwa nakuwepo hapo dukani(nyumban kwao) muda wote nikitoka kazin na siku za weekend. Mbaya zaidi mwanamke huyo amekuwa akinipigia simu na kuni-sms kuwa mimi ni mtu muhimu sana kwake na kamwe hawezi kukata mawasiliano nami. Nimekuwa sipokei simu wala kujibu msg zake. Nikibadili namba za simu, anazitafuta. Naomba ushauri, nitaepukaje janga hili? Maana hata dukan kwangu nakuwa sina amani pindi akija kununua vitu, naogopa huyo bwana wake akimuona dukan si atahisi bado tu wapenzi? Na uwezo wa kutafuta eneo lingine nihamishe duka sina. NISHAURINI NDUGU ZANGU.