Nifanyaje, niachane na huyu binti?

endelea na huyu wa sasa ila mwambie ukweli kuhusa mama yake mdogo, usipomwambia sasa halafu akajua baadae haitapendeza.
 
Hiyo ndoa imeingia doa!

Watakuletea matatizo baadaye!
Tafuta msichana mwingine hapo kimenuka, huyo binti atakusababisha matatizo!
 
Kwa mtazamo wangu kwa 7 umeshagundua ukweli mapema bora uwapotezee wote kwan utakuja kuleta ugomvi baina mdogo mtu na na ma.mdogo na family pia mshukuru Mungu kwa kukuonyesha mapema.
 

HorsePower mbona huyu jamaa yako tayari ameishaongea ukweli wote hapo kwa red. Kwakuwa ameishasema hana mapenzi na huyo wa zamani, ina maana option aliyobaki nayo ni aidha kuendelea na huyo wa sasa (bila kujali implication yake kwenye jamii na kwa huyo mkewe mtarajiwa kwani atakuja kujua tu!) au atafute mwingine ili kuepusha haya yote.

Binafsi ningeshauri amwambie ukweli huyo wa sasa (kwamba alishawahi kuwa na mahusiano na mama yake mdogo), then asikilizie mwenzie anasemaje kuhusu kama waendelee hivyo hivyo na mipango yao ya ndoa au wakatishe kila mtu aanze upya kivyake.

Nashauri hivyo kwa sababu akimwacha bila kumwambia atakuwa hajamtendea haki (unfair), na akimuoa bila kumwambia ni hatari sana kwa mustakabali wa maisha yao ya ndoa kwani mkewe ataumia sana atakapojua, na uwezekano wa kujua ni mkubwa mno!
 
mpelekeee ushauri unaotolewa hapa kwa tahadhari:alien:
 
Kama mmeisha anza taratibu za ndoa, songa mbele uoe hizo complications zingine weka pembeni ibilisi anataka kuingilia ndoa yako tu. na asikutishe mtu na maandiko yanasema nini sijui,
 
Hell No, acheni nidhamu ya woga enyi vizazi vya nyoka. Awaache wote wawili ili iwaje? Je huyu mchumba wake (Mtoto wa yule aliyemkimbia) anamefanya kosa gani hapo? Mkuu we WOWA tena kwa harusi ya ukweli na u-show love hadi yule mama mtu aone what she has missed from you.
NB: Ila mwambie kwanza mchumba wako mkasa wate afu umuache achague yeye, which I hope atapotezea tu maana mwenyewe anajua mama yake mdogo kicheche.
 
Kama ni makosa anayo hiyo bi mkubwa anaejifanya kukudondokea kwa sasa, hakuona umuhimu wa kuendelea kuwasiliana na wewe alipoenda ughaibuni, so kumuacha dem wako wa sasa si jambo la busara kabisa! Bi mkubwa angekuwa anakupenda kweli asingepoteza masiliano!
 
Usiachane na Mpenzi wako mpya, mueleze ukweli, jamii haitakuelewa vibaya cause ulikuwa hujui kabisa, hukujua kama ni ndugu na ulikuwa hutembei nao at hte same time, huyo wa zamani usicheke nae, atakuharibia uhusiano wako mpya, anaonekana ni mnafiki na mchonganishi, usimzoee, si mtu mwema, mweleze ukweli Mpenzi wako mpya na mueleze kuwa apart ya hayo yote, pamoja na kutomueleza ukweli baada ya kuugundua, kwasababu ulijihisi aibu, bado unampenda na hautaki mtengani, huyo mkweo mpuuze tu, asikuumize akili, huna kosa, usihofu, na yeye, Mpenzi wako mpya hana kosa kukupenda na kuwa na wewe, kuna vitu vinatokea katika maisha, tunashangaa, tunashtuka, but it just happened na maisha yanaendelea, ishi namna inayokupendeza, inayompendeza Mungu na furahia kwa kumpata unayempenda na anayekupenda, usikubali kumuachia kirahisi, pigania relation yako, usimfikirie huyo mpuuzi, anayetaka kukuharibia uhusiano wako
 
achana na huyo nini kizee(msichana wako wa zamani) angekuwa anakupenda angekutafuta.....
oa huyo uliyenae sasa hivi tena haraka sana....
ila usisahau kumweleza mpenzio wa sasa ukweli na hizo text anazokutumia huyo bibi(ex) ziwe ushahidi....wa kusumbuliwa
 
Usiachane na Mpenzi wako mpya, mueleze ukweli, jamii haitakuelewa vibaya cause ulikuwa hujui kabisa, hukujua kama ni ndugu na ulikuwa hutembei nao at the same time, huyo wa zamani usicheke nae, atakuharibia uhusiano wako mpya, anaonekana ni mnafiki na mchonganishi, usimzoee, si mtu mwema, mweleze ukweli Mpenzi wako mpya na mueleze kuwa apart ya hayo yote, pamoja na kutomueleza ukweli baada ya kuugundua, kwasababu ulijihisi aibu, bado unampenda na hautaki mtengani, huyo mkweo mpuuze tu, asikuumize akili, huna kosa, usihofu, na yeye, Mpenzi wako mpya hana kosa kukupenda na kuwa na wewe, kuna vitu vinatokea katika maisha, tunashangaa, tunashtuka, but it just happened na maisha yanaendelea, ishi namna inayokupendeza, inayompendeza Mungu na furahia kwa kumpata unayempenda na anayekupenda, usikubali kumuachia kirahisi, pigania relation yako, usimfikirie huyo mpuuzi, anayetaka kukuharibia uhusiano wako
 
kumwacha binti atakuwa hakumtendea haki muhimu amweleza ukweli kuhusu mahusiano ya zamani na mamamdogo wake amsikie atasema nini na haswa waangalie upendo wao zaidi
 

Huyu wa sasa ndio wa kumuowa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…