Nifanye Nini ili anipende??

Boflo

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2010
Posts
4,383
Reaction score
4,412
Nimempa pesa nyingi sana..

Nimemlipia ada ya chuo..

Nimeingia chumvini...

Ufundi mwingi nimetumia...

Zawadi nyingi sana nimemnunulia...

Sehemu za starehe nyingi nimempeleka..

Na mambo kadhaa wa kadhaa....

Bado namuona hana upendo na anachokitaka kwangu ni pesa tu ...

Wataalamu wa Jf nawauliza inawezekana kweli kumbadili aweze kunipenda??

Detailz za mwanamke mwenyewe
1-22 years old
2-Amewahi kuumizwa sana kimapenzi(story amenipa mwenyewe)
3-Ni Msukuma
4-Mahusiano yetu=mwaka 1
 
Uyo basi anataka roho yako, mwee! Mi namuunga mguu alosema mpe mimba, thats the solution, atanyooka tu
 
Tupa kule tafuta mwingine ana wake huyo iko siku atakukimbia tena wakati unamhitaji kweli....
 
Boflo hapo jibu ni rahisi, hivyo ulivyovitaja na vingine ambavyo hukutaja ndo vinavyosababisha uendelee kuwa naye, na inaelekea ulivitanguliza hivyo kama gia yako ya kumpata, so ujue siku vikikatika ndo umuoni tena!

Ushauri: endelea kumfanyia ili uendelee naye au tafuta anayekupenda kwa dhati uachane na huyo. Na ukiamua kutafuta mwingine, usitangulize tena hayo makitu kitu yako, vinginevyo utaishia kupata fake tena.
 
Ingawa hujasema uhusiano umekaa kwa muda gani, lakini kama unadhani hana mapenzi kwako nadhani ungeachana naye. Mbaya zaidi umesema anaonekana kupenda hela, hiyo ni mbaya zaidi. Mimi nisingejiuliza mara mbili hapo, kitambo ningepiga chini, tena huwezi jua pengine pesa anachota kwako then naye anaenda kuhonga huko. Achana naye.
 
kama hakupendi kubali hizo facts otherwise kubali kuachwa baadA kutimiza ndoto zake
 
ulitanguliza pesa subiri zikuishie ndo macho yatafunguka.
 
Pole Boflo, msukuma??? afu wewe wa Pwani???

Mmmh, siwasemei wote ila wanawake wa kaisukuma wanapenda wanamme wenye nguvu
 
Pole Boflo, msukuma??? afu wewe wa Pwani???

Mmmh, siwasemei wote ila wanawake wa kaisukuma wanapenda wanamme wenye nguvu
Kongosho yaani umewaza sawa na mimi, Boflo...........mbona kama huna nguvu aisee???????? ile mambo inakufanya uwe kama finyofinyo vile.
 
Last edited by a moderator:
Ukipenda usipopendwa ni kazi bure kama vp mweleze ukwl unavyojisikia asipokukubal au kukupenda kama unavyotaka tafuta mwingine unapoteza muda wako
 
Tatizo la hawa viumbe wakionyeshwa upendo wa dhati, wanajisikia We kauka jifanye huna taimu nae utaona mwenyewe anajishtukia huyo, tena yeye ndio ataanza kukuonea wivu na malalamiko kibao kuwa "mbona siku hizi umebadilika".
 
kaka unaweza ukawa unamhudumia yeye na kibwana chake,sio bure
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…