Nifanye nini nipandishe kiwango cha mauzo yangu kwa siku?

Fuqin

JF-Expert Member
Joined
Dec 2, 2018
Posts
306
Reaction score
625
Natumai mko poa kabisa watu wa humu ndani...

Kama mnavyojua mimi ni mfanyabiashara wa nafaka za Jumla na mauzo yangu kwa siku ni kilo 700 hadi 1000 ndi wastani kwa siku... sasa hali ya maisha ishakuwa ngumu vitu nimepanda bei sana na kipato kinakuwa hakitoshi tena

Nahitaji mawazo yenu ili niweze kuuza kilo 1500 hadi 2000 kwa siku hii itasababisha maisha yawe ahueni... MAWAZO YENU NI MUHIMU SANA KWANGU.

SHUKRANI SANA!
 
Hii biashara ningekuwa naielewa vizuri ningesema chochote.

Ila hongera mzunguko wako kama kila kilo unalaza sh 100 basi kwenda na laki nyumbani kila siku si haba
 
Shusha bei ili uvutie wateja wengi, na hivyo kuuza kilo nyingi zaidi kwa siku.
 
Mshukuru sana Mwenyezi Mungu. Kama unauza kilo 700 nakuendelea kwa kipindi hichi aisee we ni Don. Kuna wenzako kumaliza kilo 100 tu ni kesi sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…