Nifanyeje nipende soka la ndani, habari za simba na yanga?

goodfool

JF-Expert Member
Joined
Oct 11, 2016
Posts
1,668
Reaction score
994
Wakuu,

Kwa kipindi kirefu najitahidi angalau niwe na mapenzi na hizi timu zetu, soka La ndani, nashindwa kabisa.

Mimi ni mpenzi Wa soka, na ni mzalendo haswa, ila mambo ya VPL, habari za soka LA ndani siwezi hata kusoma.

Hasa nikiona mambo kama vile fitna na mitafaruku katika vilabu, mambo yasiyo na weledi katika uendeshaji wa vilabu hivyo, kuchanganywa michezo na politics nk.

Je, kuna meditation yoyote?

Asanteni.
 
Vuta ndumu huwe kama manara.
 
Mimi natamani niache kushabikia soka la ndani lakini nashindwa. Hata mimi sijui nifanyeje.... Yaani najitahidi kuto fuatilia weeee lakini ikifika siku Simba SC inacheza naahirisha kufanya mambo yangu mengine yote ili nifuatilie hiyo mechi. Ila mechi za nje sina mzuka nazo kabisa
 
Tunamatatizo tofauti yanayofanana , DDDD
 
1. Amua
2. Nenda uwanjani
3. Anza kufuatilia mara kwa mara

N.B Hivi kwa nini ujilazimishe kupenda kitu ambacho hunacho moyoni?
 
Mie ninaishi miaka 22 sasa nje ya Tanzania lakini ninafuatilia mpira wa Tanzania hususani timu yangu pendwa ya Simba utafikiri ninaishi Tanzania. Nikija kutembelea familia kila miaka miwili, lazima niende Taifa kuangalia mechi za Simba na kupiga picha na wachezaji. Ninafuatilia usajili, magazeti, kwenye mitandao pamoja na blogs zote za mipira.
Kwa miaka ya karibuni Azam TV wamefanya niwe ninaamka asubuhi (kutokana na tofauti ya masaa) kuangalia mechi za Simba (na wakati mwingine Yanga) live kwenye Azam app yao. Kwa kweli siwezi kuacha kushabikia Simba.
Mwezi uliopita nilikuwa nyumbani kwa msiba wa mama, lakini nilikwenda Taifa kuona mechi ya Simba na African Lyon pamoja na Tanzania na Cape Verde.
Simba ikifungwa nyumbani hakukaliki lol.
 
Tafuta jamaa anayeshabikia Yanga, we njoo kwa wanyama halafu mada zianzie hapo.
 
Jitahidi usiwe unaangalia mechi za Yanga. Utazidi kuchukia Soka la Tanzania maana hiyo timu huwa inacheza soka bovu lakini inashinda. Nakushauri uwe unaangalia mechi za Simba na Azam utapata burudani safi kama lile la Arsenal.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…