Nigeria: Mamia waokolewa msikitini wakiwa wamefungwa minyororo

Nigeria: Mamia waokolewa msikitini wakiwa wamefungwa minyororo

beth

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
3,880
Reaction score
6,368
Polisi nchini Nigeria imewaokoa watu 259 kutoka katika kituo kisichokubalika kisheria kilichopo ndani ya msikiti katika mji wa Ibadan, uliopo katika jimbo la kusini magharibi mwa nchi hiyo la Oyo, vimeripoti vyombo vya habari nchini humo.

Wengi miongoni mwa waliookolewa katika uvamizi wa polisi walikuwa wamefungwa kwa minyororo katika eneo la msikiti, amesema msemaji wa Polisi Gbenga Fadeyi.

78C51C88-995F-4C1F-AD0B-C126ADE34F25.jpeg

Katika kipindi cha uliopita, zaidi ya watu 1,000 wameokolewa kutoka kwenye vituo vya kidini ambako mara kwa mara watu wamekuwa wakishikiliwa katika hali mbaya.

Wazazi wamekuwa wakiwatuma watoto wanaowasumbua kitabia na vijana wanaoaminiwa kuwa na uraibu wa madawa ya kulevya au wale waliopatikana na makosa madogo katika vituo vya Quran vya kurekebisha tabia.

Lakini maafisa wamevifananisha vituo hivyo na vituo vya ukatili ambapo watu wanafungwa minyororo, kufungwa pamoja na kufanyiwa dhuluma.

BEA88F30-6125-40A1-BF8E-E489DA7A4850.jpeg

Waliotekwa waliachiliwa Jumatatu jioni baada ya polisi kupewa taarifa na kijana mwenye umri wa maika 17 ambaye alikuwa ametoroka kutoka katika mahabusu nyingine katika eneo hilo.

Mmiliki wa mahabusu hiyo na watu wengine wanane wamekamatwa, limeripoti gazeti la Punch nchini humo.

Kamishna wa Polisi wa jimbo hilo Bwana Shina Olukolu alinukuliwa akisema kwamba baadhi ya waathriwa wa utekaji huo wamesema wamekuwa wakishikiliwa kwa miaka kadhaa.

Hali katika msikiti huo ilikuwa ni mbaya kwa binadamu kuishi na baadhi ya vifo vya waathirika vilivyotokea havikuripotiwa, alinukuliwa akisema.

Huu ni mojawapo ya uvamizi wa wa hivi karibuni wa vituo vinavyoitwa ''vituo vya kiurekebisha tabia'' nchini Nigeria ambamo watu wanashikiliwa katika hali mbaya mkiwemo kufungwa na minyororo.

Wengi husajiliwa kwenye taasisi hizo na ndugu zao ili kupata usaidizi wa kiroho na kurekebisha tabia kwa wanaotumia madawa ya kulevya.

76CA6AAE-736D-4588-BDAF-ED19D455D549.jpeg
 
Modern day slavery 🤦🏽‍♂️😞
 
Mnaacha kujadili huo ukatili wanaofanya waafrika wenzenu mnaamisha magoli kwenye dini,nilichokiona hapo ni kwamba ukatili hauna dini wala jamii fulani kama ambavyo huwa tunasema wazungu na waarabu ni makatili..
 
Tutajie basi hao wasiokuwa na dini ili tulinganishe matendo yao na matendo ya wenye dini ili tujue kuwa tatizo ni dini au watu wenyewe.
Sihitaji kukupa stats, angalia nchi za kiislamu wanavyoishi alafu linganisha na nchi ambazo hazijali dini then utapata majibu, hata nchi zisizo na dini wanaosababisha matatizo mara nyingi ni watu wa dini, marekani terrorist wengi walioua watu ni waislamu, facts speak louder than just words. Watu waliouawa kwa sababu ya dini ni millions, wakristo wameua sana zamani, waislamu siku hizi ndo wanaua sana in the name of religion. Uzuri nimetembea nchi zote hizi sio nakaa nyuma ya keyboard kama wewe hujui kinachoendelea duniani.

We unataka proof gani zaidi? hiyo habari hapo juu hujaisoma? au hujaelewa kua hao wamepelekwa ili kunyooshwa na waislamu wenzao? hata tanzania nakumbuka enzi hizo high school waislamu walikua wasipoenda msikitini sheikh anawafuata na fimbo shuleni wanaenda wanatandikwa viboko, mambo ya kulazimishana. Mtu moja kajichanganya akaingia msikitini na viatu alikua anakimbizwa na watu, walimkamata alipigwa kipigo hatokuja kusahau, religion of peace my ass.
 
Sihitaji kukupa stats, angalia nchi za kiislamu wanavyoishi alafu linganisha na nchi ambazo hazijali dini then utapata majibu, hata nchi zisizo na dini wanaosababisha matatizo mara nyingi ni watu wa dini, marekani terrorist wengi walioua watu ni waislamu, facts speak louder than just words. Watu waliouawa kwa sababu ya dini ni millions, wakristo wameua sana zamani, waislamu siku hizi ndo wanaua sana in the name of religion. Uzuri nimetembea nchi zote hizi sio nakaa nyuma ya keyboard kama wewe hujui kinachoendelea duniani.

We unataka proof gani zaidi? hiyo habari hapo juu hujaisoma? au hujaelewa kua hao wamepelekwa ili kunyooshwa na waislamu wenzao? hata Tanzania nakumbuka enzi hizo high school waislamu walikua wasipoenda msikitini sheikh anawafuata na fimbo shuleni wanaenda wanatandikwa viboko, mambo ya kulazimishana. Mtu moja kajichanganya akaingia msikitini na viatu alikua anakimbizwa na watu, walimkamata alipigwa kipigo hatokuja kusahau.
Mbona unaeleza kijumla jumla tu hebu taja majina ya hizo nchi ambazo hazijali dini ili tulinganishe na unachokisema,sababu kwa mfano nchi kama Marekani au southafrica tunajua zina uhalifu na hakuna watu wenye kujali hizo dini ambazo wewe ndio unaona ni chanzo cha uhalifu.
 
Siyo kila asiye na dini anapenda ushoga, tatizo hua mnatafuta visingizio kuonyesha kua dini ni kitu cha muhimu kwenye morality. Mimi siamini kama kuna mungu ila still sipendi ushoga naona kama uchafu, sipendi kuona watu wanatumia hormones kujibadilisha jinsia, hii hai-prove chochote, morality ni morality tu regardless mtu ana dini au hana.

Tatizo la dini umezaliwa Mkristo au Muislamu au moja ya dini nyingine elfu kadhaa, dini yako inakwambia Mungu ni moja na Mungu wa kweli ni wa dini yako. Hehehe! hebu tumia akili, kati ya dini elfu kadhaa unahisi dini yako ina nini special cha kufanya mungu wako awe wa kweli na wa wengine wote awe feki? sababu inabaki kua umeshika kwa kua ulizaliwa huko ila hamna sababu nyingine, na mtoto ukim-brain wash akikua ni ngumu sana kubadili mawazo maana ndo kitu amekijua maisha yake yote. Nashukuru sana kutoa kwenye kifungo cha kijinga hicho maana hata mi nilikua mtu wa dini sana, nilivyoanza kuquestion nikashika kitabu nikakisoma mwanzo mwisho kama mara tatu ndo nikagundua ilikua upuuzi mtupu, kinajipingapinga, paragraph hii unaambiwa aliruka inayofuata unaambiwa alikaa, alafu unaamini vyote. fkn nonsense!
 
beth,
Nahisi hii habari imetiwa mikono ebu tunaomba chanzo cha habari ili tutafsiri wenyewe sio kuamini kila kinachaondikwa kama mnavyojua dunia ya Leo watu wanapindisha Sana maneno msikitini hakuwezi kuwa na itikadi hizo za kufungana nyororo miguu Kwanza uislamu unakata labda kama ni watu wanajinasibisha na uislamu ili kuuchafua kama hao magaidi wakutengenezwa ili kuonyesha dunia kama uislamu ni ugaidi na wajinga wakaamini
 
Haya ni matendo ya binadamu kwa kivuli cha dini, naona unataka kumpa Mungu lawama asizostahili. Graph
 
Mada kama hii unamweka Mzungu kwa vipi?

Kama nawewe ungekuwa unajadili mada iliyopo mezani huwezi kumtaja Mzungu au Mkristo hapo.

Mada inahusu waliofungwa na kuteswa MSIKITINI.
Ni kweli mada inahusu waliyofungwa na kuteswa kwenye hicho kituo ambacho kipo msikitini ila watu katika uchangiaji wao wanaleta masuala ya kidini kwa kutaka ionekane waislamu ni makatili,ndiyo nimewakumbusha kuwa ukatili ni suala binafsi la mtu halihusiani na dini wala jamii ya watu kama tumekuwa tukisema kuwa waarabu na wazungu kuwa ni makatili.
 
Azarel,
Hao ni Waafrika wenzio wenye kufanya huo ukatili haijalishi ni imani gani, ila ukweli mchungu kuwa hao ni Waafrika.
 
Hao ni waafrika wenzio wenye kufanya huo ukatili haijarishi ni imani gani ila ukweli mchungu kuwa hao ni waafrika.

Huyo jamaa ni mjinga, anaendekeza sana chuki za kidini! Huko huko Nigeria, majuzi tu hapa kulikuwa na tukio kama hilo lakini limetokea kanisani na wala sio msikitini: Police arrest prophet, rescue 15 chained persons in Lagos church

Na mmoja wa waliookolewa, ni mtoto wa miaka 9.

Sasa hiyo sijui watasemaje! Tena hayo yanatokea Lagos, huko mashambani kuna hali gani? Ni Ukristo wa wapi unaruhusu ushenzi kama huo? But still, kuna baadhi ya washenzi in the name of Christianity wamefanya huo wendawazimu
 
Haya ni matendo ya binadamu kwa kivuli cha dini, naona unataka kumps Mungu lawama asizostahili
Huyo ana matatizo yani yeye alitaka asisikie uhalifu wowote kutoka kwa watu wenye kuamini dini kisa tu wanaamini dini,hivyo mtu akifanya kosa anaona dini ndio tatizo na si kwamba binaadamu ndio wako hivyo hukosea. Jamaa huwa anaamini hadi kwamba wasioamini Mungu ndiyo wenye uwezo wa kimali kuliko wenye kuamini Mungu.
 
Azarel,

Binaadamu sio kama malaika hivyo binaadamu siku zote hufanya makosa hakuna asiyefanya makosa maana hatujakamilika, sasa wewe unavyosema wakristo hufanya dhambi wazi bila kificho unaona ni jambo la sifa kwamba ni kiburi sana huna wa kumuogopa hadi ujifiche?
 
Why argue with a fool? The Holy Bible prevents such an act. Ona hapa biblia inasema nini kuhusu watu walioharibika akili kama wewe:

Zaburi 14 (Biblia Takatifu)
¯¯¯¯¯¯¯¯¯¯
¹ Mpumbavu amesema moyoni, Hakuna Mungu;
 
Waislam wa Afrika ni akili mgando baadhi.
 
Back
Top Bottom