Dark City
JF-Expert Member
- Oct 18, 2008
- 16,253
- 11,626
Samahani wadau wa jukwaa letu tukufu la MMU,
Kwanza kabisa, naamini mko wazim na mnadunda...Mie pia ni mzima na nimewa-miss kikweli kweli!!
Leo nimejikuta napatwa na mawazo ya ajabu ajabu kuhusu hili jambo ambalo katika makuzi yetu hatukukutana nalo. Enzi zetu mama alikuwa mtu wa shamba na baba anafanya kazi kidogo shamba na kutumia muda wake mwingi kuzunguka mitaa kama jogoo!!
Siku hizi, hiki kizazi kimejikuta kikikabiliwa na changamoto za kimaisha. Ni jambo la kawaida kukuta wanandoa wote wanafanya kazi na mmoja wao au wote wanalazimka kuwa na zamu za usiku.
Kwa wale wenye kazi za namna hiyo au wanafahamu washikaji/jamaa wenye kazi kama hizo, wanaweza kutupatia uzoefu wao kuhusu changamoto za kazi za namna hii especially katika sekta ya MMU??
Wenu awapendaye,
Babu DC!!
Kwanza kabisa, naamini mko wazim na mnadunda...Mie pia ni mzima na nimewa-miss kikweli kweli!!
Leo nimejikuta napatwa na mawazo ya ajabu ajabu kuhusu hili jambo ambalo katika makuzi yetu hatukukutana nalo. Enzi zetu mama alikuwa mtu wa shamba na baba anafanya kazi kidogo shamba na kutumia muda wake mwingi kuzunguka mitaa kama jogoo!!
Siku hizi, hiki kizazi kimejikuta kikikabiliwa na changamoto za kimaisha. Ni jambo la kawaida kukuta wanandoa wote wanafanya kazi na mmoja wao au wote wanalazimka kuwa na zamu za usiku.
Kwa wale wenye kazi za namna hiyo au wanafahamu washikaji/jamaa wenye kazi kama hizo, wanaweza kutupatia uzoefu wao kuhusu changamoto za kazi za namna hii especially katika sekta ya MMU??
Wenu awapendaye,
Babu DC!!