Sina uelewa sana na haya mambo ya betting,
1.Mkeka ni set ya kutabiri mechi zaidi ya moja,kwenye betting jinsi unavyobashiri mechi nyingi na uwezekano wa kubashiri mechi nyingi ina maana ukishinda utapata hela nyingi.Unaweza ukatabiri mechi 6 ,tano ukapatia lakini moja ikagoma hapo wanasema hiyo uliyokosea imechana mkeka
2.Kwenye bet huwa kuna timu mbili na zote zinapewa point kutokana na kiwango cha timu kwa wakati huo,timu kubwa hupewa point ndogo na timu kubwa hupewa point nyingi.
Mfano:Manchester City VS Sunderland, uwezekano wa ManCity kushinda ni mkubwa so Man City atapewa point chache na uwezekano wa Sunderland kushinda ni mdogo so Sunderland atapewa point nyingi.Ikiwa ulitabiri Sunderland akashinda na kweli akashinda utapata hela nyingi kuliko yule aliyetabiri Man City itashinda na kweli ikashinda
3.Watu wa betting wana mawakala wao ambapo ukishinda unaenda kuchukua hela yako
4.Kushinda hela nyingi unatakiwa upatie kubashiri matokeo ya mechi nyingi na dau lako la ku-bet liwe kubwa na timu ulizo ziwekea dau ziwe na point nyingi
Mfano:Ukibet mechi 10 na zote ukapatia na dau lako lilikuwa kubwa kama 50,000 hapo utashinda mamilioni