Pamoja na maelezo mazuri ya Ambitious, maneno haya yanakaribiana sana, kiasi kwamba unapolitumia moja, linaweza kujihusisha na jengine.
Hizi hapa maana kwa mujbu wa Kamusi la Kiswahili Sanifu la TUKI:
Uasherati: Tabia ya kupenda kuzini, dondoo, kiranga.
Ukahaba: Mwenendo wa m'me au m'ke wa kushiriki uasherati kama biashara yake; umalaya, uteleleshi, uzinifu, uzinzi
Umalaya: Ukahaba
Uzinzi: Hali ya ukware, uasherati, uzinifu, dondoo.
**************************************
Kama kidokezo tu, hii inanikumbusha jambo moja. Waeskimo wana majina mengi kwa ajili ya barafu, kwa sababu ndio waliyonayo nyingi. Vilevile Waswahili tuna majina mengi ya matumizi ya maji (kukoga, kunawa,kutawaza, kufua, kuchanyata, kujisafisha....), pengine kwa sababu tunayo mengi.
Kuhusu maneno haya: uasherati, ukahaba, umalaya na uzinzi, kama utaaangalia yote yanahusiana na ngono isiyo halali. Jee hakuna uwezekano wa kuwa tuko kama walivyo Waeskimo na barafu, sisi na ngono isiyo halali?