Nikajifanya kumchanganya, akalikoroga zaidi…..!

Nikajifanya kumchanganya, akalikoroga zaidi…..!

Mtambuzi

Platinum Member
Joined
Oct 29, 2008
Posts
8,809
Reaction score
15,421
Nilikuwa nimetoka shule ya sekondari ya Pugu, ambako nilienda kumwona ndugu yangu anayesoma pale. Nakumbuka ilikuwa ni Jumapili mwaka 1999. Nilipanda basi kurudi mjini baada ya mazungumzo na huyo ndugu yangu. Wakati nikiwa kwenye basi, alipanda abiria mmoja ambaye alionekana kuutwika mtindi. Kwa Jumapili jioni, huwezi kushangaa kukuta mtu kautwika mtungi saa 11 jioni. Yule bwana kwa bahati mbaya akaja kukaa kwenye kiti nilichokuwa nimekaa.

Alipokaa hakunisalimia, bali alinitazama sana, yaani kwa muda mrefu hadi nikakereka. Halafu alisema, ‘usinitishe bwana, kwani nimefanya nini. Kama mambo yalishaisha sasa kwani ni lazima uyaendeleze.' Nilishangaa, kwa sababu nilikuwa simfahamu na sikuwa naelewa anachosema. Aliendelea, ‘sikiliza afande, najua leo umenishika, lakini mambo si yalishaisha, hela zake nilimrudishia, basi kama unaona kunikamata ndio utafaidi, sawa nikamate niko tayari.' Sikumwelewa, lakini nilihisi kwamba ananichanganya na polisi fulani.

Niliona nimchanganye tu na yeye. ‘Kwa nini ulizichukuwa hela zile?' Nilimuuliza. ‘Wewe mwenyewe unajua usawa wa nyumbani, ungekuwa hutujui sawa. Wewe mwenyewe unamchukua mamangu mdogo anakupa stori za homu, sasa unauliza kwa nini nilizichukuwa, si shida.' Niliona naanza kuadhirika kwa sababu abiria wengi waligeuka kumtazama huyo afande anayemchukuwa mama mdogo wa yule mlevi ambaye pia alishajitangazia kuwa ni kibaka. ‘Sawa, nimeelewa, yameisha, sina haja ya kukukamata.' Nilisema nikijua yameisha, kumbe yalikuwa ndiyo yanaanza.

Aliniambia, ‘lakini afande wewe siyo mchezo. Mama yangu unamchukuwa, sista umebamba, haikutosha, mama Mona naye hukuachia, halafu yule demu mwenye grosari karibu na mtendeni shop ukabeba. Haki ya Mungu afande unaniacha hoi, unafagia...! lakini angalia ukimwi, angalia afande....!'
‘Kama usiponyamaza nitakukamata nikurundike ndani,' nilisema nikiwa nimekereka. Niligundua kwamba, mtu anaweza kufanya jambo kimzaha, likageuka hadi mwenyewe akalihisi kama ni kweli. Nilijuta kumjibu kwa kujifanya mimi ni huyo afande kweli.
‘Hapo sasa ndiyo sikuelewi. Wewe siri zako zikianikwa unatishia kuniaresti. Mimi nimesema ukweli tu, lakini unakuwa mkali, wala sijakosea wala nini, na wala sitamtonya mama mdogo kwamba wewe ni kifyagio. Kwanza nilipie nauli.' Alisema.

Nilitoa nauli haraka na kumlipia. ‘hapo sasa sawa. Simwambii mama mdogo wala sista, wewe swaga tu, wanawake wa mjini nao wanapenda mkwanja sana...' Alisema na kusimama. Alikuwa amefika. Alishuka huku akisema, ‘lakini afande angalia, ngoma, kilo mbili hatari...' Abiria wote sasa macho yalikuwa kwangu. ‘Uzuri wa ulevi ndio huo,.. unampa mtu ukweli wake bila kujali,'abiria mmoja alisema. Sikutaka kujibu, sikutaka yawe makubwa zaidi.


Hii kusema cha ukweli inanihusu mimi mwenyewe na wala sio rafiki yangu…………..LOL
 
Shikamoo baba,
Pole na mwaswaibu hayo,
Bora ungempotezea tu kuliko ulivyomjibu lol!
 
Shkamoo baba. Impersonation ni mbaya sana, mie mtu akinifananisha tu naruka kimanga futi 100.
Sasa baba, zile nguo za mwaka mpya si unaleta leo maduka yameshaanza kufunguliwa?
 
Shkamoo baba. Impersonation ni mbaya sana, mie mtu akinifananisha tu naruka kimanga futi 100.
Sasa baba, zile nguo za mwaka mpya si unaleta leo maduka yameshaanza kufunguliwa?

Yale maneno ya changu wa Kinondoni niloweka humu last week umemwambia mama yako, imekuwa taabu hapa nyumbani! hivi unatarajia kweli nikununulie nguo za za thikukuu
 
Mtambuzi heri ya mwaka mpya,
pole pia na masahibu ya mvua,
pole sana na hayo ya kibaka,

Na mimi dada yako mkubwa uliniahidi kuwa mwaka huu
utaninunulia shamba kule Bagamoyo,
je ahadi yako unaikumbuka?
 
Siku zote ukiona mlevi jaribu kukae naye distance y ambali sana, mana hana akili, mwenye akili hawezi kwenda kununua ujinga.

Ukikaa naye inabidi na wewe ukbali kuitwa mjinga.
 
heri ya mwaka mpya ,... nafurahi mwaka umeanza na naamini utakuwa mzuri kwako na kusahau machungu ya 2011
 
hahaha mtambuzi leo inakuhusu ww nimekukubali.
pole kwa maswahibu hayo mkuu.
ila unajua kupanga maneno jaman , yan unaadithia had balaa loh.
jiunge 2 na shigongo jaman.
hapy new year mkuu.
 
hahahahahahaha pole, sipati picha ulivyojawa fadhaa siku hiyo,
inawezekana alikuwa kweli amelewa au hakuwa na nauli akatumia njia hiyo
mjini shule...
 
hahahahahahaha pole, sipati picha ulivyojawa fadhaa siku hiyo,
inawezekana alikuwa kweli amelewa au hakuwa na nauli akatumia njia hiyo
mjini shule...

Kweli mjini shule..................
 
Siku zote ukiona mlevi jaribu kukae naye distance y ambali sana, mana hana akili, mwenye akili hawezi kwenda kununua ujinga.

Ukikaa naye inabidi na wewe ukbali kuitwa mjinga.

Tangu tukio hili linipate, ujinga umenitoka..................... Na nimepunguza kihehere
 
Tangu tukio hili linipate, ujinga umenitoka..................... Na nimepunguza kihehere

Sasa kila mtu ana cheo chake wenye kuita Babu, Mjomba, haya nami naita Babu sasa tuone nani zaidi, baada ya hayo Pole sana Babu yangu.
 
heri ya mwaka mpya mtambuzi...umenifanya nijisikie vizuri....kuna uzi mmoja kule kwenye Siasa wa akina ENL, RA,JKM umenitoa kwenye 'mudi' tangu jana. Asante mkuu!
 
Back
Top Bottom