Habari wana JF, naomba msaada kama hili ni tatizo kiafya au ni hali ya kawaida!
Mara nyingi nikiangalia tukio la kusisimua hasa lenye kuleta furaha/faraja/huzuni kwenye tv, (movie au live event) huwa najikuta nabubujikwa machozi hasa nikiwa peke yangu! Ninapokuwa na wengine naweza kujikaza au kufuta machozi haraka haraka lakini mtu akinichunguza vizuri atalingundua hilo.
Sasa nashindwa kuelewa kama hili ni tatizo ama ni hali ya kawaida, na kama kuna namna ya kupunguza hali hii