nikila tu napata maumivu ya tumbo

sepuka

Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
11
Reaction score
0
habari zenu wana jf shida yangu kubwa ni kwamba nina siku tatu kila nikila chakula si asubuhi nikinywa chai au mchana pia hata usiku napata maumivu makali ya tumbo pia linavuruga sana na kuunguruma naombeni msaada wenu madoctor nijue tatizo langu hospital bado sijaenda kwasababu nipo mbali na hospital kubwa.
 
CHADEMA watakua wanahusika.
 
Mr kamwone Daktari kwanza halafu ndiyo utaweza kurudi na jibu una shida gani ndiyo tuweze kukusaidia zaidi
 
Pole sana.Hizo ni dalili za Gastritis kitaam.Kwa lugha yab kawaida ni hatua ya mwanzo ya vidonda au michubuko tumboni.Maelezo yako si ya kutosha.D alili mojawapo ni maumivu ya tumbo eneo la chembe kama kunawaka moto,ukila chakula tumbo linavuruga na gesi kwa wingi.kubeua na kujamba.Maumivu yanaendana na vyakula vya aina fulani.km chai,kahawa,ndimu,pilipili na vyakula vyenye viungo.Watu wa namna hii inawezekana wakawa na tabia ya kutokuwa na muda maalum wa kula.Ili kupata nafuu...acha vyakula vyenye asili ya ukali,kula mda maalum,tumia na antiacid km magnesiamu au dawa km Relcer Gel km hakuha hata maziwa husaidia.Unahitaji kwenda kwa Daktari upimwe kujua chanzo ni nn.Bakteria aina ya H.pylori husababisha pia.Ugua oole
 

Karibu yote umemaliza mkuu, ndio maana ukaona watu wamekaa kimya. big up!
 
nashukuruni kwa ushauri wenu pia green marwa kwa kunikumbusha kuhusu chembe ya moyo na tumbo kuwaka moto kweli hivyo vinanitokea napata maumivu makali mno.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…