MSANII anayezidi kungara kwenye filamu mbalimbali Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu', amedai kuwa, anapenda kuvaa nguo fupi kwa sababu akivaa nguo ndefu anawashwa. Akizungumza na Ijumaa juzi ndani ya Viwanja vya Leaders Club Kinondoni, Dar es Salaam, Lulu alisema kuwa, hiyo ndiyo sababu kubwa ambayo inamfanya kila anapotoka avae nguo hizo za kihasarahasara.
"Yaani huwezi kuamini, nikivaa nguo ndefu, basi siku hiyo nitajikuna sana maana nitawashwa mwili mzima, kuanzia kiunoni, hasa mapajani kuelekea miguuni," alisema msanii huyo na kuongeza:
"Ujue kuvaa kwangu nguo fupi siyo kwamba naiga kwa watu wengine, tangu nikiwa mtoto nilikuwa navaa hivyo na ndiyo maana kubadilika ni ngumu kidogo."
Lulu ni msanii wa kike mwenye umri mdogo ambaye mara kadhaa amekuwa akilalamikiwa kutokana na tabia yake ya kuvaa nguo fupi....