Nikki wa 2 na Izzo Bizness nani zaidi?

Viol

JF-Expert Member
Joined
Dec 15, 2009
Posts
25,420
Reaction score
18,298
Nani unamkubali au unadhani nani anajua zaidi?
 
Genre tofauti ....Izzo anaimba Crank na Nikki wa Pil ni HipHop . .sasa sijui unashndanishaje.....
 
Genre tofauti ....Izzo anaimba Crank na Nikki wa Pil ni HipHop . .sasa sijui unashndanishaje.....

Ni kweli hawaendani,ila na wewe umekosea.Izzo haimbi crank,Izzo anafanya hiphop commercial while Nikki anajaribu kufanya Hiphop ile yenyewe
 
nikki ni zaidi. izzo b anamistari laini sana. hana punch lines. style yake inawai kuboa. single pekee anayojivunia ni naongea Rizwan. kwa kifupi ni kwamba Izzo hajui mziki
 
Nicki wa pili ni zaid ya izzo b, izzo b anafanya hip hop laini huu akili za ziada kuifikiria mistal yake lakin nick inabid utulie kumelewa anachoimba
 
HUYU izzo b HAJUI KITU ASHUKURU MUNGU ALIKUA ANAJUANA NA ADAM MCHOMVU COZ MCHOMVU AMEWAHI KUA MTANGAZAJI KULE MBEYA SO AKAMUOMBEA LABEL MJ NDO AKATUSUA..
 
huu mziki wa kibongo ukiwa pimbi huwezi toka utabaki unasifiwa na masela kama wanavyosifiwa kina nash emcee sijui takataka gani!.....kwa kuelewa hilo mkali IZZO B aliamua kubadilika na kufanya mziki unaopendwa na wengi!...!kila ngoma na kichupa kikali!mziki kama haukupi pesa basi inabidi ukupe mademu wakali!.......izzo ni mkali!...kimuonekano mpaka kwa game anayoifanya
 
Ndo hapo wabongo hawaelewi wanafanya mziki kwa ajili ya biashara au kutafuta jina
 

Hahahahahaahahaaa masela wanajua kusifiana sana ooh mara Nash Mc mkali,mara sijui Nick Mbishi,na ukiwabishia wapo tayari hata kurusha ngumi ila waambie hata kununua CD yao ni mtihani,wao kazi kuchoma CD tu,show nazo wanavizia zile za bure za viwanjani halafu anajifanya anauchungu sana na huyo msanii.Ukitaka ufanye biashara ya mziki na utengeneze maisha inabidi uachane na kuwaridhisha masela,wapenzi wa kweli na wanunuzi wa kazi za sanaa ni Wamama,Wadada na 'Magentlemen',hao ndo hata show za wasanii wapo tayari kutoa kiingilio cha elfu 50.Polezao wa kina Nash MC wanaosifiwa sana na masela halafu wanaishia kuishi maisha ya kubangaiza ya kutembeza cd mtaani,wenyewe wanajiita 'wanaharakati' teh.Wakiwaoana wasanii kama hao wakina Izzo wanafanya vizuri sokoni wanawabeza kwa kuwaita majina kibao sijui ma-waki.IZZO we edelea kukaza bwana achana na masela,haya maisha aisee
 
HUYU izzo b HAJUI KITU ASHUKURU MUNGU ALIKUA ANAJUANA NA ADAM MCHOMVU COZ MCHOMVU AMEWAHI KUA MTANGAZAJI KULE MBEYA SO AKAMUOMBEA LABEL MJ NDO AKATUSUA..

Acha chuki binafsi,mi nilikuwa naishi Iringa.Izzo kaanza kutamba huko mikoa ya nyanda za juu kusini esp. Iringa na Mbeya wakati huo hata Adam Mchomvu simjui.Izzo kaanza kupewa promo na Clouds baadae sana wakati huo watu tunaoishi mikoa hiyo tumeshaujua uwezo wake na alikuwa kashakuwa star pande hizo.Alianza kukimbiza Mbeya na Iringa kabla hajaja mjini halafu unasema anabebwa?
 

mkuu kama hujaelewa kitu uwage unauliza,izzo alikua anasoma st.aggrey mbeya,kipindi hicho adamu mchomvu anatangaza radio mbeya(alikua field,alitangaza kwa miez mitatu),hapo ndio izzo akajuana na mchomvu lakin sio kivile,kama umeanza kumckia izzo kabla ya mchomvu bas we ni muongo kipind hcho mchomvu alikua anajiita "tall wa ajabu",kipind hicho mbeya na nyanda za juu kusini izzo alikua asikiki kabsa,waliokua wanatamba kwa pale ni kama TWALI B,FESTO G,MARU n.k,IZZO akaja badae,lakin kutokana na unyenyekevu wake kipindi hicho anatafta jina akawa anaiva na ma-presenter wote wa mbeya akiwemo A.MCHOMVU(TALL WA AJABU),na badae akaja dar kusoma IT ndo akaanza harakati za kutoka,akamfuata mchomvu,mchomvu akampeleka kwa M.J na kumuombea lebel na wimbo wa kwanza chini ya MJ aliomshirikisha SUMALEE(business) ndo kidogo ukamtoa,na kama ukiusikiliza ule wimbo vizur beat ndo imembeba,baada ya hapo akakorofishana na M.CHALI kwasababu alikuta CHALI kampa GODZILLA beat yake(beat ambayo GODZILLA kaimbia wimbo wa SALASALA),akaachna na CHALI na kwenda kwa TUDDY THOMAS ndo akatoa ile ngoma ya RIZONE(huu ndo wimbo sasa),..
kama unadhan IZZO ni mkali kwanini hakutoka kabla ya kuonana na MCHOMVU hapa dar,na zile nyimbo kama TENZI ZA MAPENZI,HUU MUZIKI,MI NDIO MBEYA,PISHA NIPITE e.t.c.? Mkare_wenu
 
Last edited by a moderator:

hamfahamu huyu mkuu.....ndo hawa hawa wanaosema Marlaw alianza muziki alipokuja dar!
Izzo kaanza kubamba kusini huko kitambo.....viji show vya mbeya na iringa kule,ruvuma na rukwa tangu kitambo...

ila angeendelea na staili ile kutusua ingekua ndoto!!kabadilika.kaanza kufanya ''biashara'' na katusua kweli!

nyimbo kama Hukumu ya ndotoni - Rado,Homa ya dunia ya Traveller,ngoma nyingi za Hashim dogo sio za biashara!
ni wadau tu,tena tuki miss mambo magumu basi ndo tunasikiliza...............hupigi club,magoma hayapati mzuka nazo na hauko ndo kwenye biashara kweli!

so...izzo yuko poa kwa mtazamo wangu.
 

Twaha,Festo,Ng'ombe,Maru wote hawa wamefanya muziki wakati Izzo anafanya muziki!tangu kanasoma Agrrey! kutoka ni platform kubwa kupatikana na zaidi sana MUKTADHA wa muziki wake!aliacha kufanya hayo mnayodhani ni hip hop halisi il tu apate sifa za kijinga kwa wana...........akafanya ''biashara'' ya muziki na matokeo yanaonekana!

nyimbo kama Huu muziki,Wananong'ona nk zisingemtoa yeye kabisa!

ishu ya unyenyekevu sijui kama ni kwasababu alikuwa akitafuta kutoka...sijamuona siku kitambo,ila kwangu na washikaji alikua dogo poa sana,mnyenyekevu sana bonge la mtu!
 


mkuu ina maana ili utusue ni lazma ufanye hiphop lain.?
mbona akina FID Q wametusua na ugumu wao.?
kimsingi IZZO hakua na nyimbo ngumu(za hiphop) za kumfanya atusue na ukweli ni kwamba hawez kufanya hiphop kamili,hana kichwa cha kutunga mistar ya hiphop kamili na akatoka..
anafanya mziki kama anaofanya YOUNG DEE,MR.BLUE,hvo huwez mfanansha na mtu anaeumiza kichwa kama NIKKI..
 

Kipindi mimi nipo Iringa hizo Redio za Mbeya zilikuwa hazisikiki so ntamjuaje Mchomvu?Izzo mi nilimjua kupitia Redio za Iringa palepale ndo zilikuwa zinacheza nyimbo zake,na wasanii kama wakina Marlaw ambao kwa Iringa walikuwa maarufu tayari kabla hawajajaja town.Kuhusu hizo nyimbo zake za awali zilikuwa nzuri pia ila hakupata nafasi ya kupewa promo,wangapi wananyimbo kali lakini hawatoki?Sikatai kwamba Mchomvu kamsaidia kwa kiasi kikubwa lakini uwezo pia anao i mean anabebeka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…