Niko sahihi au?

Inaonekana umebadili dini kumfuata lakn hufanyi yanayoendana na dini yake. Pia ww ndio umesabbisha yote hayo. Iv hujafunzwa unyagoni jnc ya kumrdisha mwanaume kwenye hal ya kawaid kama mmekwaruzana? Hebu mchape na upande wa kanga afu uone responce yake.
 
inaonyesha kwa kiasi fulani unakiburi huwezi na wala huna mamlaka ya kumwona mume wako kinya ukasema wajisikia kichefuchefu piga una anaye kupa kiburi rejea kwa mola wako kisha haya yote utaona ni mepesi kila mmoja wetu anamaelekezo ya namna ya kuishi na mwenzi wake pole sana mwan jm
 
mhhh:tape:

Today 04:52 PM
shosti
JF Senior Expert Member
This message has been deleted by shosti.



SHOSTI
wewe, acha kabisa kuchezea akili za watu, halafu vile Mungu si Athumani umejiumbua mwenyewe. Pamoja na kufuta post, foot print hizo.


$£&&*%$"*&%$



Ninamaanisha SHOSTI member wa JF ndiye Salma Juma. Kajisahau akiwa kalog in kama SHOSTI akajibu post kama SALMA JUMA. Mineisoma wakati naiquote ili kumwambia nilimwambia hapo juu, akawa tayari kaifuta.

Hii michezo ina mwisho wake

Aisee Hivi wewe Salma ndio Shosti?

Yaelekea mnajua sana, hata idadi ya watoto na mahusiano yenu ya ndani mnajuana?

Huyo Shosti alisababishaje wewe kuuliza swali..
Dah..JF ina mambo.

Ushauri wangu nina-ureserve kwanza mpaka uje na ufafanuzi wa hayo hapo juu
 
Lazima wewe au yeye mnakula nje au wote.

Mmh inaonekana hujaongea yote humu na sijui unataka ushauri gani haswa.

Ila usije humia roho siku ukija jua anafamilia huko nje na watoto.
 
nashukuru umehitaji ufafanuzi mkubwa,angalia tar yangu ya kujiunga utagundua kuwa nilifungua hii id siku nyingi zaidi ila sikuiumia hata siku moja kutokana na sababu ambazo siwezi kuzitaja kwa sasa,mdada namfahamu si chini ya miaka mitano sasa na siwezi sema yote ila baadhi ya matatizo ya mumewe huwa tunaelezana kama marafiki wa kawaida...mara zote tulikuwa tunashauriana kikawaida tu ila leo kidogo hakuwa vizuri kuchelea ushabiki nikamuomba tuuweke mgogoro wake hapa kwa imani aatasaidiwa ila kinyume chake imekuwa ndivyo sivyo..kashukuru kugundua kwamba kuupeleka mgogoro huu kwenye familia yanaweza tokea yaliotokea hapa ila kiukweli mmemsononesha sana mdada wa watu,kabla hatujawahukumu wenzetu tukumbuke kuna siku tutahukumiwa na wengine.
 

najua wewe ni mtu mzima si vizuri kukuhoji kama mtoto..Pale kwenyer red juu, inamaansha hiyo ID ilikuwa yako na umemwazima rafiki yako leo??

Any way, kama hili si stori ya kutunga, basi mwambie rafiki yako asitarajie njia ya mkato kutafuta suluhu kama kweli anaitaka.
Hayo yaliyomsononesha ndio haswa anatakiwa akayafanyie kazi.
Lazima AJIVUE GAMBA. Kilichompeleka kwenye ndio sio matunzo ya watoto, bali ni mume wake..Akiacha kiburi na kujiamini, basi anaweza.

Ila hilo sharti la kwamba mwanaume lazima ajirekebisha kwa kumjali mwanae, dada, huyo mtoto ni wenu wote wawili, si kwamba hajui wajibu wake, ila tabia unayomwonesha ndo inamfanya mwanaume akuache umtunze na kumjali peke yako. Sasa kama ndoa umefunga na mtoto wako basi usitarajie makubwa.
 
kama unamwona mume wako kinyaa,inakuwaje kwa wana jf?↲Mimi naona hata ushauri wetu hautasaidia kama kamlia mume wake buyu kwa miaka mi4 inamana czani kama ushauri wetu utaweza yabadilisha hayo.fikiria kauli aliyoitoa ya kua anajisikia KICHEFUCHEFU.II NI zARAU. We tapika ili ijulikane mbichi na iliyoiva.
 

sijamwazima ila siitumii kabisa na yeye si mwanachama humu na ndicho kilichopelekea kutumia id ambayo haijawahi kutumika hata siku moja,hadithi si ya kutunga tangu namfahamu mdada nimewakuta na matatizo yao na mumewe,ila nadhani ya,mezidi au ni kutapatapa ndo mdada aliniuliza swali gumu na la mtigo siwezi kuliweka hapa ndugu zangu,ila sijawahi kuolewa wala sijui ndoa ina umuhimu gani ndipo tukaliweka swali lake humu...ila hebu tujiulize inakuwaje mtu unakosa dk 10 tu kwa wiki za kuongea na mwanao kuhusu maisha nafikiri kama tungekuwa waungwana kidogo tungemwelewa mdada vizuri tu maana kuna mengi yaliyojificha nyuma ya hili jambo nami siwezi kuyabwaga hapa hayanihusu.
 

Hapo kwenye red naona unajichanganya tu. kwa kifupi ilikuwa ni ya kwako..Lakini mleta thread amesema yeye alikuwa mfuatilaji toka muda mrefu, kwa hiyo sio mgeni sana..

Hapo kwenye blue, huwezi kuleta stori nusunusu halafu utegemee suluhisho kamili. Inaonesha kumbe kuna sababu ya mwanamke kukimbia chumba kwa miaka 4.
Kama kweli mmedhamiria kupata ufumbuzi kutoka hapa JF, basi wekeni stori kamili. Kuna watu hapa ambao wamepitia kama yenu na wanaweza kuwapa ushauri wa kuwasaidia...
 
pole sana dada salma , me kwa maoni yangu naona kuna umuhimu wa kuwashirikisha wazazi wote wa pande mbili kutatua matatizo yenu,
 

la kuweka story nzima ni uamuzi wa mdada mwenye tatizo lake nami ni muhadithiwa tu nsijidai mdomo mkubwa hapa kumbe hadithi zenyewe sizijui kivile..nadhani atafatilia na kama atakuwa tayari mtamuona tena hapa kinyume chake wao wenyewe wananafasi kubwa ama kusuka au kunyoa.naenda kazini jamani kama tunavyojua asiyefanya kazi na asile maana nami kazi ndio mume wangu ngoja nimbembeleze haswaaaaaaa!!!
 

halazimishwi kuleta stori kamili ni hiari yake...
 
Sikiza nikwambie mwanakwetu, mwanaume wako ni mrahisi sana kumgeuza fikra zake ni wewe tu hujampatia, kwanza kabisa akikaa kwenye sofa nyie mnakula unapakua unamfata pale mnakula wote yaani unampakulia,then ukioona aanzi kula jaribu kumlisha sidhani kama ni robot la aina hiyo mpaka akatae kula hata akilishwa, mwonyeshe upendo aliou kosa kwa wazazi wake, maana ni kama analipiza vile, Pia inawezekana kabisa alimchukia mtoto alipozaliwa akaona kachukua nafasi yake, wapo wanaume wa aina hii wengine mpaka wanawaziba pumzi watoto wafe ili abaki na mkewe.
Bibi wewe rudi chumbani kwako, Ondoa chuki, mpe mapenzi baba , mwonyeshe mapenzi mtoto wako ya kupitiliza ili umsaidie, anaathirika kisaikolojia.Cha mwisho ondoa mahasira just be happy, maana unaweza pata maradhi ya moyo ukamwacha mwanao na baba yake sasa hapo sijui atamtunzaje mtoto!Mwisho kabisa pole sana Mumeo si mkatili ila navyoona aliathirika katika makuzi yake, msaidie.
 
Shosti jamani ni nini tena unafanya??!! ndio nimesoma nimeelewa sasa. loooooooo sina hamu
 
du! pole sana.... hii case inakuwa complicated zaid sababu ipo upande mmoja kwamba Mr "alijifungia kitambo". kwa kiasi fulani upo sahihi kwa ulichofanya sababu we ni binadamu na unachoka kuvumilia...
Tungekuwa na kitengo (au kama kipo) katika ustawi wa jamii, nadhani ungefungua file, nadhani inaapaswa kuwa na taratibu za kuwawajibisha wakina baba wa namna hiyo ili walazimike kuwajibika kwa watoto wao,
Siwezi kusemea sana mapenzi yenu na baba watoto, saiv inabidi ujitoe muhanga kwa ajili ya mtoto tu, Vipi kanisa umelishirikisha vipi?
 
salma, kwa maelezo uliyotoa nashawishika kabisa kuamini kuwa tatizo la mumeo ni malezi yake. wewe ulikulia katika familia ambayo baba alikuwa na mapenzi na familia, wakati mumeo katika makuzi yake hakupata mapenzi hayo toka kwa wazazi hasa baba. Na inaonekana pia katika ukuaji wake yapo mengi yaliyomsibu. Hivyo, nakusihi, rudisha upendo wa kwanza, mpende tena, kwani huna hisia naye kwa kuwa ktk ubongo umeshaweka dharau. lakini pia, chukua jukumu la baba kwa mtoto wako, kwa kumuonyesha kuwa baba anamjali na kumpenda, maana mtoto naye atajenga chuki kubwa sana, juu yake, na katika familia yake tatizo hilo linaweza kumtokea kama babaye.
Lakini mwisho wa yote, nenda kanisani, Mungu anaweza yote, na una mume mzuri tu. mpe nafasi tena katika moyo wako, kupenda ni kuamua.
 
Nafikiri ni vema kwanza kama wewe ni mkatoliki ukasoma sheria za ndoa za kanisa katoliki Code of Canon Law - IntraText halafu kama mna mkanda/ DVD ya harusi yenu kuanzia unajipamba salon mpaka kwenye reception mjaribu kuuangalia mkiwa wote wawili na mtoto wenu ili mkumbuke maagano yenu; tatu inaonekana wewe ndio chanzo cha tatizo kwani umehama chumba, mwenzio akikusemesha unaona kichefuchefu. Nne, je wajua kazi ya mumeo; yawezekana inamfanya awe busy mno. tano, je wajua kusamehe kama kweli ni mkristo, mkatoliki wa vitendo basi ishi Injili - samehe saba mara sabini. Pia ukumbuke kuwa 'kiingiacho mwilini si najisi bali kitokacho kupitia mdomoni ndicho najisi'.

Hivi kutoa pesa kwa mahitaji yote sio kujali familia?

Kwa kifupi hauko sahihi!
 


mumeo ni jasusi.........
 
huyu dada ana ID mbili.....shost na salma juma ni mtu mmoja............anatuchezea akili tu huu nilishani anaonewa kumbe anatuzuga hapa.......
 
Pole sana dada, hapo mmechelewa sana na mmempa nafasi shetani atawale maisha yenu, kwangu mimi sioni kama 4 years ni nyingi pasipo kupata suluhisho la moja kwa moja, mimi nakushauri usifiche kidonda, umefunga ndoa ya kanisa, mshirikishe mzee wa kanisa au kwa kuwa babu yupo hai na ana nguvu.. basi mshirikishe babu ili muweze kutatua tatizo, kwa kuwa anahudumia, na anajali mpaka ndugu zako, bado nafasi yenu ya maisha ipo sana, ni iblis au shetani tu anaharibu nafsi zenu, mkiomba, mkimrudia mungu na kushirikisha wazee wa kanisa au babu suluhu nzuri itapatikana... toa kinyongo na fanya hivyo salma, kwa uwezo wa Mungu utarudi kwenye hali ya kawaida.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…