nikope shiling ngapi?

rebeca

Senior Member
Joined
Dec 18, 2011
Posts
190
Reaction score
27
jamani nataka kufanya biashara ya gari ya tax pamoja na bajaji moja,zote nataka kununua second hand....ila zisiwe zimechakaa sana zisije kuanza kunipa tabu matengenezo,je shiling ngapi nikope kama mtaji???milioni sita zinatosha kwa vyote viwili?kwa week/siku zinaingiza kama shilingi ngapi?/baada ya muda gani nitegemee kurudisha mtaji?.....wapi nitapata hivi vitu vikiwa in good conditions? nilisikia bandarini wanauza kwa nji ya mnada magari....huwa unafanyika lini?na magari huanzia shiling ngapi kuuzwa???

thanks in advance......
 
Labda nikuulize Rebeca, kwa nini umechagua biashara hiyo kama huielewi vizuri?
 
Habari dada Rebeca,
kwa ushauri wangu mimi kwa kuwa ndo unataka kuanza hiyo aina ya biashara uliyoifikiria, ni vyema ukabadili idea kwa kuwa mtaji wenyewe ni wa kukopa mahali, na kama unavyojua biashara huanza kama mtoto anapozaliwa yaani unahitajika kuwa mvumilivu hadi ikue na kukomaa ( kuanzia miezi 3, miezi 6 hadi mwaka 1). Pili kwa biashara za taxi kwa siku unaweza kupata Tsh 10,000 hadi 20,000 na bajaji ni Tsh 10,000 hadi 15,000 kulingana na hali ya chombo, msimamizi (dereva), mahali zinapofanyia kazi nk.. hivyo kwa hiyo Milioni 6 hata kama ukifanikiwa kupata gari na bajaji nzuri, itakuchukua zaidi ya mwaka hadi miaka miwili kurudisha mtaji.. Una nafasi ya kukopa hadi kiasi gani? kwa riba gani? marejesho ni ya muda gani?..nakushauri fanya biashara hizi zifuatazo kwea huo mtaji (mda mfupi unaweza kurudisha mtaji na kuanza kupata faida):
- Jiko la Bar
- Kibanda kizuri cha kuuza chips
- Choo cha kulipia
- Duka la vyakula
- Duka la jumla
- Kuuza mayai kwa jumla
- Ufugaji wa kuku
- Vipodozi
- Salon ya kiume
- Fast Food Cafe etc etc
 


thanks,naweza kujaribu hio ya vipodozi.....
 
Mwali hakuna aliyezaliwa anajua,kuuliza maswali ni part ya kujua.
Basi acha uwezekano wa kubadili biashara ikiwa utakuta hii hailipi kama ulivo tegemea. Alafu nadhani millioni 6 ni dogo kwa biashara yote mbili. Anza na moja, ikianza kuingiza lipa deni, alafu ndio uanzishe ya pili. Ni mtazamo wangu tu.
 
Ml6 ni pesa nyingi kwa kuanzia mtaji.ila hiyo biashara ya tax&bajaji sikushauri kuifanya.kuna changamoto nyingi sana ktk biashara hiyo kama kukamatwa mala kwa mala,matengenezo,ajali na mengine kibao.kwa mtu kama wewe ambae pesa unakuwa umeipata kwa mkopo ni hatari kwa afya yako,unaweza pata bp.
 
Usiende huko fungua duka la dawa na vipodozi na butique ya kina dada u'll make it
 
Habari Dada Rebeca
kwa biashara yeyote unayotaka kuifanya sisi tutakusaidia na kuifanya kuwa ya kimataifa zaidi
kama ulivyoambiwa na kushauriwa na wadau hapo juu sisi tutakusaidia kuitangangaza biashara yako online ....
tu pm kwa maelezo zaidi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…