SoC01 Nikosoeni; Nakataa bustani ya Edeni haiko Mashariki ya Kati

SoC01 Nikosoeni; Nakataa bustani ya Edeni haiko Mashariki ya Kati

Stories of Change - 2021 Competition

Gnyaisa

Member
Joined
Jul 13, 2021
Posts
23
Reaction score
24
Katika BIBLIA kuna maandiko kadhaa yanayoonesha ahadi za Mwenyezi Mungu kwa taifa la Israel pindi alipokuwa akiwatoa utumwani Misri. Ni ahadi ya kuwapeleka katika nchi ya maajabu, nchi inayotiririsha maziwa na asali! Sina uelewa mkubwa katika masuala ya dini na elimu ya jiografia lakini NAKATAA maelezo ya wachambuzi wetu duniani kuhusu ilipo bustani hiyo.

Naamini nchi hiyo ya Mungu haiko Mashariki ya kati bali hapahapa barani Afrika. Naamini Nabii Musa hakupaswa kuvuka bahari ya Shamu na kwenda bara jingine bali alipaswa kuvuka jangwa la Sahara na kuja Mashariki mwa Afrika (Pengine ndio maana safari ilikuwa ya mbinde sana). Bado naamini Tanzania ndilo taifa aliloahidiwa Abrahamu na sisi watanzania (hasa vijana) tuna kila sababu za kujivunia hilo. Hebu tutazame maajabu yafuatayo;

Kwa miaka mingi wanasayansi mbalimbali walikuwa wakizunguka duniani kote kutafuta asili ya binadamu. Wataalamu hawa wa masuala ya jiolojia na historia walizunguka katika mabara yote na mataifa mbalimbali bila mafanikio. Walipiga kambi Mashariki ya Kati lakini hawakuambulia kitu! Baadae wakaamua kuja Afrika ili kukamilisha ushahidi kwamba walitembelea dunia nzima. Mnamo mwaka 1911, mjerumani Wilhelm Kattwinkel alifanikiwa kupiga kambi katika Bonde la Oldupai Gorge nchini Tanzania na kujionea mafuvu mengi ya binadamu wa kale!

Baadae mwaka 1913 mjerumani mwenzake Hans Reck alikuja na timu ya wataalamu ili kujiaminisha lakini vita ya kwanza ya dunia ikasitisha tafiti zao. Miaka kadhaa baadae, magwiji wawili wa sayansi, Louis na Mary Leakey waliithibitishia dunia kwamba binadamu wa kale aliishi katika eneo ambalo kwa sasa ni nchi ya Tanzania zaidi ya miaka milioni moja iliyopita. Mpaka sasa hakuna tafiti mpya za kisayansi zinazopinga hilo.

Mbali na uvumbuzi huo, zipo shahidi mbalimbali za kimazingira zenye kuelezea wazi kwamba taifa letu ni bustani tosha ya Edeni iliyokosa matunzo. Hebu tutazame kwa kifupi;

Sifa kuu ya bustani yoyote ni uwepo wa mandhari yenye kuvutia na viumbe mbalimbali wa asili katika eneo hilo. Tanzania ni taifa pekee duniani lenye viumbe wengi wa asili ambao hawapatikani katika maeneo mengine. Tuna utitiri wa hifadhi za taifa zinazovutia maelfu ya watalii kila mwaka. Tuna hifadhi ya taifa Ruaha (Hifadhi ya pili kwa ukubwa Afrika baada ya Kafue iliyoko Zambia), pia tunayo hifadhi ya taifa Arusha, hifadhi ya taifa Gombe, hifadhi ya taifa Katavi, hifadhi ya taifa Kilimanjaro, hifadhi ya taifa Mahale, hifadhi ya taifa Mikumi, hifadhi ya taifa ziwa Manyara, hifadhi ya taifa Rubondo, hifadhi ya taifa Serengeti, hifadhi ya taifa Saadani, hifadhi ya taifa Tarangire, Hifadhi ya taifa Udzungwa, hifadhi ya taifa Kitulo, hifadhi ya taifa Mkomazi, na hifadhi ya taifa tarajiwa ya Saanane. Hifadhi ya Serengeti pekee ni kubwa kuliko taifa la Gambia!

Katika maajabu saba ya asili ya bara la Afrika, maajabu matatu yanatoka nchini Tanzania huku ajabu la 4 (mto Nile) chimbuko lake likiwa Ziwa Viktoria linalomilikiwa na Tanzania kwa zaidi ya asilimia 50. Hakuna wa kunipinga nikisema Nabii Musa na hata YESU KRISTO walikunywa maji kutoka Tanzania maana tumefundishwa uhai wa nchi ya MISRI unatokana na mto Nile (Nile is Egypt and Egypt is Nile). Shughuli zote za kilimo na maisha za wakazi wa Misri zinategemea mto Nile unaotoa maji yake Ziwa Victoria.

Ukitaka kusimama sehemu yenye mwinuko mrefu kuliko zote barani Afrika ili kujionea uzuri wa bara zima inakulazimu uje Tanzania kisha upande mlima Kilimanjaro. Aidha, ukitaka kuzama sehemu yenye kina kirefu kwenda chini barani Afrika inakulazimu tena uje Tanzania katika ziwa Tanganyika. Ndilo ziwa lenye kina kirefu kuliko yote Afrika na la pili duniani. Hata mti mrefu kuliko yote barani Afrika uko nchini Tanzania. Una urefu wa mita 81, unatoka katika familia ya Entandrophragma excelsum (Mti mrefu zaidi Afrika wagunduliwa Tanzania - BBC News Swahili).

Ni katika taifa la Tanzania pekee unaweza kukutana na aina mbalimbali za wanyama na viumbe wa asili. Tuna aina za vyura ambao mataifa mengine duniani hayana. Vyura aina ya Nectophrynoides asperginis (Vyura wa kihansi), hawapatikani sehemu nyingine yoyote duniani isipokuwa katika bonde la Kihansi nchini Tanzania. Tanzania ni miongoni mwa nchi 6 za maziwa makuu barani Afrika zikiwa na jumla ya maziwa 4 (Viktoria, Tanganyika, Nyasa na Rukwa) kati ya maziwa 9 (tisa) yaliyoko katika orodha rasmi ya maziwa makuu. Tafiti zinaonesha kuwa asilimia 10 ya aina zote za samaki duniani zinapatikana katika maziwa haya makuu huku maziwa ya Viktoria, Tanganyika na Nyasa yakichangia moja ya nne (1/4) ya maji baridi yanayopatinana duniani.

Taifa hili ambalo ni la 13 kwa ukubwa wa eneo barani Afrika na la 31 duniani, limetenga zaidi ya asilimia 35 ya ardhi yote kuwa hifadhi ya taifa kwa maana ya mapori ya akiba na mbuga za wanyama. Kwa zaidi ya nusu karne sasa tumekuwa kisiwa cha Amani na kimbilio la wanyonge kutoka mataifa mbalimbali.

Pamoja na taifa hili kuwa na makabila zaidi ya 120 na tofauti mbalimbali za kiimani, bado tumeendelea kuishangaza dunia kwa jinsi tunavyoishi kwa kuvumiliana na kuelewana. Ni taifa pekee Afrika ambalo licha ya watu wake kuwa na lugha zao nyingi za asili, WOTE wanaunganishwa na lugha moja ya Kiswahili ambayo sio lugha ya mkoloni!

Tanzania imebarikiwa kuwa nchi ya pili barani Afrika kwa wingi wa mifugo (ng’ombe, mbuzi na kondoo) nyuma ya Ethiopia lakini hatuna bomba hata moja linalotiririsha maziwa. Bado Tanzania ni taifa linaloongoza kwa kuagiza maziwa ya kopo kutoka ughaibuni. Viatu, mikoba na bidhaa mbalimbali za ngozi ambazo taifa lingeweza kuzalisha hazipo tena kwa sababu tunaongoza kwa kuuza mifugo hai nchini Kenya kisha wao wanachinja na kuuza kupata bidhaa zaidi ya kumi. Watanzania tubadilike.

Tanzania imebarikiwa kuwa na misitu mingi ya asili pamoja na nyika. Ardhi nzuri tuliyonayo na mvua ya kutosha ni fursa nzuri ya kuwa na misitu mingi ya kupandwa nchini lakini haipo na wala hatuna bomba hata moja linalotiririsha asali katika misitu na nyika hizo! Mungu atupe nini?

Tanzania imebarikiwa kuwa na tambarare na mabonde mazuri kuliko mataifa mengi hapa duniani. Tuna bonde la mto Pangani lenye ukubwa wa kilometa za mraba 53,600 (Ukubwa sawa na mataifa ya Rwanda na Burundi kwa pamoja!), tuna bonde la mto Ruvuma lenye ukubwa wa kilometa za mraba 152,200 ambazo kati ya hizo kilometa za mraba 52,200 (ukubwa zaidi ya taifa la Denmark!) ziko nchini Tanzania na eneo linalosalia liko Msumbiji na Malawi.

Tuna bonde la ziwa Nyasa lenye kilometa za mraba 132,000 lililoko katika nchi za Tanzania, Malawi na Msumbiji ambapo eneo la bonde kwa Tanzania ni kilometa za mraba 37,000 (ukubwa zaidi ya taifa la Ubelgiji!). Tuna bonde la ziwa Rukwa lenye ukubwa wa kilometa za mraba 88,000 (ukubwa zaidi ya taifa la Austria). Pia tuna bonde la Wami Ruvu lenye kilometa za mraba 72,930 (ukubwa mara mbili ya mataifa ya Haiti na Jamaica kwa pamoja!). Pia tunayo mabonde ya ziwa Tanganyika, bonde la Ziwa Viktoria na mabonde ya ziwa Eyasi, Manyara na Bubu. Mabonde yote haya yana maji ya kutosha na ardhi yenye rutuba kwa kilimo na ufugaji wa kisasa wa samaki.

Katika utajiri wa maliasili ni wazi taifa letu limependelewa. Mpaka sasa tuna akiba ya madini ya Dhahabu inayofikia wakia milioni 36, uzalishaji utakaotufanya tushike nafasi ya tatu baada ya Ghana na Afrika Kusini. Tuna hazina kubwa ya madini ya Urani, uzalishaji ambao utatuweka katika nafasi ya tatu Afrika baada ya Niger na Namibia. Tuna gesi asilia yenye ujazo wa zaidi ya futi trilioni 26, tuna madini ya makaa ya mawe yanayofikia tani milioni 50.94, tuna madini ya chuma pia. Tuna madini adimu ya Tanzanite ambayo hayapatikani sehemu yoyote ile duniani na zaidi ya yote, hivi karibuni imepatikana hazina kubwa ya madini ya magadi soda huko Monduli mkoani Arusha.

Eneo hilo lenye mita za ujazo bilioni 4.6 za madini hayo zitaipaisha Tanzania hadi nafasi ya tatu nyuma ya Marekani na Uturuki kwa uzalishaji. Pamoja na hazina yote hii, bado tunaambiwa kwa mdomo eti pale jangwani upande wa pili wa Misri ndipo ilipokuwa bustani ya Edeni. NAKATAA.

Kitabu kitakatifu cha Biblia kinaielezea bustani ile kuwa ilizungukwa na maji pande zote nne kwa maana ya kaskazini, kusini, mashariki na magharibi na maji yale yalikuwa yakitiririka kuingia bustanini (Mwanzo 2:10-14). Hakuna TAIFA lingine hapa duniani lenye aina hiyo ya maji zaidi ya Tanzania. Upande wa kaskazini tumezungukwa na mito ya maji ya ziwa Viktoria, hili ni ziwa la kwanza kwa ukubwa barani Afrika na la pili duniani baada ya ziwa Superior lililoko Amerika ya Kaskazini.

Upande wa Magharibi tumezungukwa na ziwa Tanganyika ambalo ni ziwa lenye kina kirefu kuliko yote barani Afrika na la pili duniani baada ya ziwa Baikal lililoko Asia. Upande wa Kusini tumezungukwa na ziwa Nyasa. Hili ni ziwa la tisa kwa ukubwa duniani, la tatu kwa ukubwa na la pili kwa kina barani Afrika. Upande wa mashariki tumezungukwa na ufukwe wa Bahari ya Hindi wenye urefu wa zaidi ya kilomita 800 kuanzia mkoani Tanga hadi Mtwara. Pamoja na maji yote haya yanayotiririshwa na Mungu kuingia bustanini bado mnaniambia hii sio Edeni? POA NIKOSOENI LAKINI EDENI HAIKO MASHARIKI YA KATI.

Watanzania tuamke, tubadilike na tupambane katika kuinua uchumi wa taifa letu. Wasomi tuache kunung’unika na badala yake tujikite katika kupambana na changamoto zinazoikumba jamii kwa kuzibadili kuwa fusa za ajira na serikali ijikite katika kutengeneza mazingira bora na yaliyo rafiki kwa raia wake kuishi kwa amani na utulivu. (gnyaissa@yahoo.com)
 
Upvote 3
Uzi wako ulitakiwa uishie palepale uliposewa "Huna uelewa mkubwa kuhusu dini na jiografia"

Lakini yote kwa yote, Mungu Ibariki Tanzania.
Hahaha. Hiyo ni lugha ya picha tu ili kutoa nafasi kwa wenye uelewa zaidi kumwelewesha mwandishi
 
Bustani ya Eden ilikuwa mbinguni huko huko, ndio maana Mungu alilowafukuza Adam na Hawa baada ya kula tunda akawaleta duniani, huku wakaja kuzaa kwa uchungu, na kula kwa jasho, na matokeo ya dhambi yao Mungu akawaambia mtakufa, hope walikufa na kuzikwa duniani huku huku.
 
Bustani ya Eden ilikuwa mbinguni huko huko, ndio maana Mungu alilowafukuza Adam na Hawa baada ya kula tunda akawaleta duniani, huku wakaja kuzaa kwa uchungu, na kula kwa jasho, na matokeo ya dhambi yao Mungu akawaambia mtakufa, hope walikufa na kuzikwa duniani huku huku.
Duh! Aiseeee.. inashangaza kwa wengine, ila kwangu haishangazi (maana Roho wa Mungu alishaniambia kila kitu).. kaka kwa wema nikushauri, chagua moja.. go hard or go home, hakuna nafasi ya udananda mbele za Mungu.

Ni kweli bustani ya edeni ilikuwa mbinguni? Ni kweli hayo uliyoandika? Kweli kaka?

Jifunze kwanza kusoma na kuichambua Biblia (Nafahamu kichwani hujui hata vifungu, na ndio maana nilipo kuuliza kile cha Yesu ulibaki unashangaa).

Ok Kila kitu kimeelezwa kwenye Biblia tupe ushahidi wa hicho ulichokisema...

Kwako Bw DNO J
 
Katika BIBLIA kuna maandiko kadhaa yanayoonesha ahadi za Mwenyezi Mungu kwa taifa la Israel pindi alipokuwa akiwatoa utumwani Misri. Ni ahadi ya kuwapeleka katika nchi ya maajabu, nchi inayotiririsha maziwa na asali! Sina uelewa mkubwa katika masuala ya dini na elimu ya jiografia lakini NAKATAA maelezo ya wachambuzi wetu duniani kuhusu ilipo bustani hiyo. Naamini nchi hiyo ya Mungu haiko Mashariki ya kati bali hapahapa barani Afrika. Naamini Nabii Musa hakupaswa kuvuka bahari ya Shamu na kwenda bara jingine bali alipaswa kuvuka jangwa la Sahara na kuja Mashariki mwa Afrika (Pengine ndio maana safari ilikuwa ya mbinde sana). Bado naamini Tanzania ndilo taifa aliloahidiwa Abrahamu na sisi watanzania (hasa vijana) tuna kila sababu za kujivunia hilo. Hebu tutazame maajabu yafuatayo;

Kwa miaka mingi wanasayansi mbalimbali walikuwa wakizunguka duniani kote kutafuta asili ya binadamu. Wataalamu hawa wa masuala ya jiolojia na historia walizunguka katika mabara yote na mataifa mbalimbali bila mafanikio. Walipiga kambi Mashariki ya Kati lakini hawakuambulia kitu! Baadae wakaamua kuja Afrika ili kukamilisha ushahidi kwamba walitembelea dunia nzima. Mnamo mwaka 1911, mjerumani Wilhelm Kattwinkel alifanikiwa kupiga kambi katika Bonde la Oldupai Gorge nchini Tanzania na kujionea mafuvu mengi ya binadamu wa kale! Baadae mwaka 1913 mjerumani mwenzake Hans Reck alikuja na timu ya wataalamu ili kujiaminisha lakini vita ya kwanza ya dunia ikasitisha tafiti zao. Miaka kadhaa baadae, magwiji wawili wa sayansi, Louis na Mary Leakey waliithibitishia dunia kwamba binadamu wa kale aliishi katika eneo ambalo kwa sasa ni nchi ya Tanzania zaidi ya miaka milioni moja iliyopita. Mpaka sasa hakuna tafiti mpya za kisayansi zinazopinga hilo.

Mbali na uvumbuzi huo, zipo shahidi mbalimbali za kimazingira zenye kuelezea wazi kwamba taifa letu ni bustani tosha ya Edeni iliyokosa matunzo. Hebu tutazame kwa kifupi;

Sifa kuu ya bustani yoyote ni uwepo wa mandhari yenye kuvutia na viumbe mbalimbali wa asili katika eneo hilo. Tanzania ni taifa pekee duniani lenye viumbe wengi wa asili ambao hawapatikani katika maeneo mengine. Tuna utitiri wa hifadhi za taifa zinazovutia maelfu ya watalii kila mwaka. Tuna hifadhi ya taifa Ruaha (Hifadhi ya pili kwa ukubwa Afrika baada ya Kafue iliyoko Zambia), pia tunayo hifadhi ya taifa Arusha, hifadhi ya taifa Gombe, hifadhi ya taifa Katavi, hifadhi ya taifa Kilimanjaro, hifadhi ya taifa Mahale, hifadhi ya taifa Mikumi, hifadhi ya taifa ziwa Manyara, hifadhi ya taifa Rubondo, hifadhi ya taifa Serengeti, hifadhi ya taifa Saadani, hifadhi ya taifa Tarangire, Hifadhi ya taifa Udzungwa, hifadhi ya taifa Kitulo, hifadhi ya taifa Mkomazi, na hifadhi ya taifa tarajiwa ya Saanane. Hifadhi ya Serengeti pekee ni kubwa kuliko taifa la Gambia!

Katika maajabu saba ya asili ya bara la Afrika, maajabu matatu yanatoka nchini Tanzania huku ajabu la 4 (mto Nile) chimbuko lake likiwa Ziwa Viktoria linalomilikiwa na Tanzania kwa zaidi ya asilimia 50. Hakuna wa kunipinga nikisema Nabii Musa na hata YESU KRISTO walikunywa maji kutoka Tanzania maana tumefundishwa uhai wa nchi ya MISRI unatokana na mto Nile (Nile is Egypt and Egypt is Nile). Shughuli zote za kilimo na maisha za wakazi wa Misri zinategemea mto Nile unaotoa maji yake Ziwa Victoria.

Ukitaka kusimama sehemu yenye mwinuko mrefu kuliko zote barani Afrika ili kujionea uzuri wa bara zima inakulazimu uje Tanzania kisha upande mlima Kilimanjaro. Aidha, ukitaka kuzama sehemu yenye kina kirefu kwenda chini barani Afrika inakulazimu tena uje Tanzania katika ziwa Tanganyika. Ndilo ziwa lenye kina kirefu kuliko yote Afrika na la pili duniani. Hata mti mrefu kuliko yote barani Afrika uko nchini Tanzania. Una urefu wa mita 81, unatoka katika familia ya Entandrophragma excelsum (Mti mrefu zaidi Afrika wagunduliwa Tanzania - BBC News Swahili).

Ni katika taifa la Tanzania pekee unaweza kukutana na aina mbalimbali za wanyama na viumbe wa asili. Tuna aina za vyura ambao mataifa mengine duniani hayana. Vyura aina ya Nectophrynoides asperginis (Vyura wa kihansi), hawapatikani sehemu nyingine yoyote duniani isipokuwa katika bonde la Kihansi nchini Tanzania. Tanzania ni miongoni mwa nchi 6 za maziwa makuu barani Afrika zikiwa na jumla ya maziwa 4 (Viktoria, Tanganyika, Nyasa na Rukwa) kati ya maziwa 9 (tisa) yaliyoko katika orodha rasmi ya maziwa makuu. Tafiti zinaonesha kuwa asilimia 10 ya aina zote za samaki duniani zinapatikana katika maziwa haya makuu huku maziwa ya Viktoria, Tanganyika na Nyasa yakichangia moja ya nne (1/4) ya maji baridi yanayopatinana duniani.

Taifa hili ambalo ni la 13 kwa ukubwa wa eneo barani Afrika na la 31 duniani, limetenga zaidi ya asilimia 35 ya ardhi yote kuwa hifadhi ya taifa kwa maana ya mapori ya akiba na mbuga za wanyama. Kwa zaidi ya nusu karne sasa tumekuwa kisiwa cha Amani na kimbilio la wanyonge kutoka mataifa mbalimbali. Pamoja na taifa hili kuwa na makabila zaidi ya 120 na tofauti mbalimbali za kiimani, bado tumeendelea kuishangaza dunia kwa jinsi tunavyoishi kwa kuvumiliana na kuelewana. Ni taifa pekee Afrika ambalo licha ya watu wake kuwa na lugha zao nyingi za asili, WOTE wanaunganishwa na lugha moja ya Kiswahili ambayo sio lugha ya mkoloni!

Tanzania imebarikiwa kuwa nchi ya pili barani Afrika kwa wingi wa mifugo (ng’ombe, mbuzi na kondoo) nyuma ya Ethiopia lakini hatuna bomba hata moja linalotiririsha maziwa. Bado Tanzania ni taifa linaloongoza kwa kuagiza maziwa ya kopo kutoka ughaibuni. Viatu, mikoba na bidhaa mbalimbali za ngozi ambazo taifa lingeweza kuzalisha hazipo tena kwa sababu tunaongoza kwa kuuza mifugo hai nchini Kenya kisha wao wanachinja na kuuza kupata bidhaa zaidi ya kumi. Watanzania tubadilike.

Tanzania imebarikiwa kuwa na misitu mingi ya asili pamoja na nyika. Ardhi nzuri tuliyonayo na mvua ya kutosha ni fursa nzuri ya kuwa na misitu mingi ya kupandwa nchini lakini haipo na wala hatuna bomba hata moja linalotiririsha asali katika misitu na nyika hizo! Mungu atupe nini?

Tanzania imebarikiwa kuwa na tambarare na mabonde mazuri kuliko mataifa mengi hapa duniani. Tuna bonde la mto Pangani lenye ukubwa wa kilometa za mraba 53,600 (Ukubwa sawa na mataifa ya Rwanda na Burundi kwa pamoja!), tuna bonde la mto Ruvuma lenye ukubwa wa kilometa za mraba 152,200 ambazo kati ya hizo kilometa za mraba 52,200 (ukubwa zaidi ya taifa la Denmark!) ziko nchini Tanzania na eneo linalosalia liko Msumbiji na Malawi. Tuna bonde la ziwa Nyasa lenye kilometa za mraba 132,000 lililoko katika nchi za Tanzania, Malawi na Msumbiji ambapo eneo la bonde kwa Tanzania ni kilometa za mraba 37,000 (ukubwa zaidi ya taifa la Ubelgiji!). Tuna bonde la ziwa Rukwa lenye ukubwa wa kilometa za mraba 88,000 (ukubwa zaidi ya taifa la Austria). Pia tuna bonde la Wami Ruvu lenye kilometa za mraba 72,930 (ukubwa mara mbili ya mataifa ya Haiti na Jamaica kwa pamoja!). Pia tunayo mabonde ya ziwa Tanganyika, bonde la Ziwa Viktoria na mabonde ya ziwa Eyasi, Manyara na Bubu. Mabonde yote haya yana maji ya kutosha na ardhi yenye rutuba kwa kilimo na ufugaji wa kisasa wa samaki.

Katika utajiri wa maliasili ni wazi taifa letu limependelewa. Mpaka sasa tuna akiba ya madini ya Dhahabu inayofikia wakia milioni 36, uzalishaji utakaotufanya tushike nafasi ya tatu baada ya Ghana na Afrika Kusini. Tuna hazina kubwa ya madini ya Urani, uzalishaji ambao utatuweka katika nafasi ya tatu Afrika baada ya Niger na Namibia. Tuna gesi asilia yenye ujazo wa zaidi ya futi trilioni 26, tuna madini ya makaa ya mawe yanayofikia tani milioni 50.94, tuna madini ya chuma pia. Tuna madini adimu ya Tanzanite ambayo hayapatikani sehemu yoyote ile duniani na zaidi ya yote, hivi karibuni imepatikana hazina kubwa ya madini ya magadi soda huko Monduli mkoani Arusha. Eneo hilo lenye mita za ujazo bilioni 4.6 za madini hayo zitaipaisha Tanzania hadi nafasi ya tatu nyuma ya Marekani na Uturuki kwa uzalishaji. Pamoja na hazina yote hii, bado tunaambiwa kwa mdomo eti pale jangwani upande wa pili wa Misri ndipo ilipokuwa bustani ya Edeni. NAKATAA.

Kitabu kitakatifu cha Biblia kinaielezea bustani ile kuwa ilizungukwa na maji pande zote nne kwa maana ya kaskazini, kusini, mashariki na magharibi na maji yale yalikuwa yakitiririka kuingia bustanini (Mwanzo 2:10-14). Hakuna TAIFA lingine hapa duniani lenye aina hiyo ya maji zaidi ya Tanzania. Upande wa kaskazini tumezungukwa na mito ya maji ya ziwa Viktoria, hili ni ziwa la kwanza kwa ukubwa barani Afrika na la pili duniani baada ya ziwa Superior lililoko Amerika ya Kaskazini. Upande wa Magharibi tumezungukwa na ziwa Tanganyika ambalo ni ziwa lenye kina kirefu kuliko yote barani Afrika na la pili duniani baada ya ziwa Baikal lililoko Asia. Upande wa Kusini tumezungukwa na ziwa Nyasa. Hili ni ziwa la tisa kwa ukubwa duniani, la tatu kwa ukubwa na la pili kwa kina barani Afrika. Upande wa mashariki tumezungukwa na ufukwe wa Bahari ya Hindi wenye urefu wa zaidi ya kilomita 800 kuanzia mkoani Tanga hadi Mtwara. Pamoja na maji yote haya yanayotiririshwa na Mungu kuingia bustanini bado mnaniambia hii sio Edeni? POA NIKOSOENI LAKINI EDENI HAIKO MASHARIKI YA KATI.

Watanzania tuamke, tubadilike na tupambane katika kuinua uchumi wa taifa letu. Wasomi tuache kunung’unika na badala yake tujikite katika kupambana na changamoto zinazoikumba jamii kwa kuzibadili kuwa fusa za ajira na serikali ijikite katika kutengeneza mazingira bora na yaliyo rafiki kwa raia wake kuishi kwa amani na utulivu. (gnyaissa@yahoo.com)
Hiyo Bustani ni mambo ya hadithi za pwagu na pwaguzi na kama ipo basi ni pale ulipozaliwa. Kweli unaamini bustani iwe jangwani badala ya Afrika ambako kuna kila kitu mwanangu. Hata hizo hija wanazofanya waislam kutembelea makaburi ni kutokana na kutojua. Kwani wao hawana makaburi kwao wala ardhi takatifu ambavyo vyote viko kule walikozaliwa?
 
Duh! Aiseeee.. inashangaza kwa wengine, ila kwangu haishangazi (maana Roho wa Mungu alishaniambia kila kitu).. kaka kwa wema nikushauri, chagua moja.. go hard or go home, hakuna nafasi ya udananda mbele za Mungu.

Ni kweli bustani ya edeni ilikuwa mbinguni? Ni kweli hayo uliyoandika? Kweli kaka?

Jifunze kwanza kusoma na kuichambua Biblia (Nafahamu kichwani hujui hata vifungu, na ndio maana nilipo kuuliza kile cha Yesu ulibaki unashangaa).

Ok Kila kitu kimeelezwa kwenye Biblia tupe ushahidi wa hicho ulichokisema...

Kwako Bw DNO J
Kumbe ulihamia huku, mbona unajitesa sana na mimi, usipanic acha huu utoto, au inawezekana ni akili yako ndogo hujui usemacho kwa wengine kitaonekaje; hii topic ni theoretical haipo na complete answer ndio maana mleta mada yeye amesema anakataa haipo mashariki ya kati akasema sababu zake.

Mimi nika SUGGEST (sijui kama unaijua maana yake) kwa sababu zangu ilikuwepo mbinguni, sasa wewe much know unaniambia nikupe mistari inayosema ilikuwepo mbinguni, ndio maana nikakwambia jifunze kufikiria kwa upana usijifungie ndani ya box.

Baadhi ya theories zilizopo kuhusu ilipokuwepo bustani ya Eden ni hizi;

- Wengine wanasema bustani ya Eden ni mwili wa Eva, ndio maana Adam akala "tunda" la mti wa katikati, sasa jamaa unahangaika kushindana na mimi wakati biblia nayoiamini imenikataza kujiingiza kwenye haya malumbano unayotaka yasiyo na maana.

- Wapo pia wanaosema hiyo bustani ilikuwepo Tanzania kwenye bonde la Ngorongoro kule palipokutwa masalia ya anayesadikiwa kuwa mtu wa kwanza.

Kuhusu mistari uliyoitaka kule ipo zaidi ya mitatu inayokukataza kujikweza/tutumua; ningekupa ila tungehamisha mjadala wa mleta mada, tatizo lako again hujui kufikiria nje ya box I told u already, kutokukupa ukadhani sina, grow up buddy, this arrogance of yourz will kill u. Learn to think before you react.

Bwana "much know" nimalizie kwa kukuuliza wewe, nipe mstari complete unaosema wapi hiyo bustani ya Eden ilikuwepo toka kwenye biblia takatifu, nikiamini kabisa kama ungekuwepo pasingekuwepo na hizi dissenting views, ili nipande ndege niende huko, na usiniambie ipo karibu na kitu au mji fulani, hilo sio complete jibu.

Pia ukisema umeoneshwa na "roho wako" Yesu Kristu ananiruhusu nikuulize ni roho wa wapi? roho wa kweli hutoa jibu moja kwa wengi wamuaminio.

N.B.
Nenda kasome uzi wako ujifunze nimekuongezea nyama, sio unawaambia watu wafanye vitu wasivyovijua kama kawaida yako, unatakiwa kuelezea each and everything inside out. Ukitaka kueleweshwa sema usione aibu na ujuaji wako.

- Lastly kukariri vifungu vya biblia sio sababu ya kwenda mbinguni, usiwafundishe wasiojua uongo, kuiishi ndio kila kitu, hata shetani anaijua hiyo mistari so kujidai nayo ni ushamba ambao nilishatoka huko.
 
Kumbe ulihamia huku, mbona unajitesa sana na mimi, usipanic acha huu utoto, au inawezekana ni akili yako ndogo hujui usemacho kwa wengine kitaonekaje; hii topic ni theoretical haipo na complete answer ndio maana mleta mada yeye amesema anakataa haipo mashariki ya kati akasema sababu zake.

Mimi nika SUGGEST (sijui kama unaijua maana yake) kwa sababu zangu ilikuwepo mbinguni, sasa wewe much know unaniambia nikupe mistari inayosema ilikuwepo mbinguni, ndio maana nikakwambia jifunze kufikiria kwa upana usijifungie ndani ya box.

Baadhi ya theories zilizopo kuhusu ilipokuwepo bustani ya Eden ni hizi;

- Wengine wanasema bustani ya Eden ni mwili wa Eva, ndio maana Adam akala "tunda" la mti wa katikati, sasa jamaa unahangaika kushindana na mimi wakati biblia nayoiamini imenikataza kujiingiza kwenye haya malumbano unayotaka yasiyo na maana.

- Wapo pia wanaosema hiyo bustani ilikuwepo Tanzania kwenye bonde la Ngorongoro kule palipokutwa masalia ya anayesadikiwa kuwa mtu wa kwanza.

Kuhusu mistari uliyoitaka kule ipo zaidi ya mitatu inayokukataza kujikweza/tutumua; ningekupa ila tungehamisha mjadala wa mleta mada, tatizo lako again hujui kufikiria nje ya box I told u already, kutokukupa ukadhani sina, grow up buddy, this arrogance of yourz will kill u. Learn to think before you react.

Bwana "much know" nimalizie kwa kukuuliza wewe, nipe mstari complete unaosema wapi hiyo bustani ya Eden ilikuwepo toka kwenye biblia takatifu, nikiamini kabisa kama ungekuwepo pasingekuwepo na hizi dissenting views ili nipande ndege niende.

Ukisema umeoneshwa na "roho wako" Yesu Kristu ananiruhusu nikuulize ni roho wa wapi? roho wa kweli hutoa jibu moja kwa wengi wamuaminio.

N.B.
Nenda kasome uzi wako ujifunze nimekuongezea nyama, sio unawaambia watu wafanye vitu wasivyovijua kama kawaida yako, unatakiwa kuelezea each and everything inside out. Ukitaka kueleweshwa sema usione aibu na ujuaji wako.

- Lastly kukariri vifungu vya biblia sio sababu ya kwenda mbinguni, usiwafundishe wasiojua uongo, kuiishi ndio kila kitu, hata shetani anaijua hiyo mistari kujidai nayo ni ushamba.
At last dhahabu imejulikana na jiwe la kupigia ndege limejulikana bwana J..

Toka umeanza na "Makovu" "LD" "PP" "m amon" n.k hujawai kuwa smart kuficha uzandiki wako..

Kuna sehemu nimeona unasema kusoma Biblia na kusikiliza Gospel sijui kunafanyaje imani... Hahahahahah, Mungu aturehemu Kama kwa kusikiliza tu Gospel ndo mambo yanakuwa vile ulivyosema nakupa kongole..

Watu hatutanii, tupo live na Roho wa Mungu..
 
At last dhahabu imejulikana na jiwe la kupigia ndege limejulikana bwana J..

Toka umeanza na "Makovu" "LD" "PP" "m amon" n.k hujawai kuwa smart kuficha uzandiki wako..

Kuna sehemu nimeona unasema kusoma Biblia na kusikiliza Gospel sijui kunafanyaje imani... Hahahahahah, Mungu aturehemu Kama kwa kusikiliza tu Gospel ndo mambo yanakuwa vile ulivyosema nakupa kongole..

Watu hatutanii, tupo live na Roho wa Mungu..
Naona umeanza kuandika huku unatetemeka, nikuache usije kufa kwa pressure.

Nimekuuliza wapi bustani ya Eden ilipo nipande ndege niende, usiseme ipo karibu na mji au kitu fulani, nipe complete answer, kinyume na hapo jione ulivyo na fikra finyu unabishana na usiemjua.
 
Katika BIBLIA kuna maandiko kadhaa yanayoonesha ahadi za Mwenyezi Mungu kwa taifa la Israel pindi alipokuwa akiwatoa utumwani Misri. Ni ahadi ya kuwapeleka katika nchi ya maajabu, nchi inayotiririsha maziwa na asali! Sina uelewa mkubwa katika masuala ya dini na elimu ya jiografia lakini NAKATAA maelezo ya wachambuzi wetu duniani kuhusu ilipo bustani hiyo. Naamini nchi hiyo ya Mungu haiko Mashariki ya kati bali hapahapa barani Afrika. Naamini Nabii Musa hakupaswa kuvuka bahari ya Shamu na kwenda bara jingine bali alipaswa kuvuka jangwa la Sahara na kuja Mashariki mwa Afrika (Pengine ndio maana safari ilikuwa ya mbinde sana). Bado naamini Tanzania ndilo taifa aliloahidiwa Abrahamu na sisi watanzania (hasa vijana) tuna kila sababu za kujivunia hilo. Hebu tutazame maajabu yafuatayo;

Kwa miaka mingi wanasayansi mbalimbali walikuwa wakizunguka duniani kote kutafuta asili ya binadamu. Wataalamu hawa wa masuala ya jiolojia na historia walizunguka katika mabara yote na mataifa mbalimbali bila mafanikio. Walipiga kambi Mashariki ya Kati lakini hawakuambulia kitu! Baadae wakaamua kuja Afrika ili kukamilisha ushahidi kwamba walitembelea dunia nzima. Mnamo mwaka 1911, mjerumani Wilhelm Kattwinkel alifanikiwa kupiga kambi katika Bonde la Oldupai Gorge nchini Tanzania na kujionea mafuvu mengi ya binadamu wa kale! Baadae mwaka 1913 mjerumani mwenzake Hans Reck alikuja na timu ya wataalamu ili kujiaminisha lakini vita ya kwanza ya dunia ikasitisha tafiti zao. Miaka kadhaa baadae, magwiji wawili wa sayansi, Louis na Mary Leakey waliithibitishia dunia kwamba binadamu wa kale aliishi katika eneo ambalo kwa sasa ni nchi ya Tanzania zaidi ya miaka milioni moja iliyopita. Mpaka sasa hakuna tafiti mpya za kisayansi zinazopinga hilo.

Mbali na uvumbuzi huo, zipo shahidi mbalimbali za kimazingira zenye kuelezea wazi kwamba taifa letu ni bustani tosha ya Edeni iliyokosa matunzo. Hebu tutazame kwa kifupi;

Sifa kuu ya bustani yoyote ni uwepo wa mandhari yenye kuvutia na viumbe mbalimbali wa asili katika eneo hilo. Tanzania ni taifa pekee duniani lenye viumbe wengi wa asili ambao hawapatikani katika maeneo mengine. Tuna utitiri wa hifadhi za taifa zinazovutia maelfu ya watalii kila mwaka. Tuna hifadhi ya taifa Ruaha (Hifadhi ya pili kwa ukubwa Afrika baada ya Kafue iliyoko Zambia), pia tunayo hifadhi ya taifa Arusha, hifadhi ya taifa Gombe, hifadhi ya taifa Katavi, hifadhi ya taifa Kilimanjaro, hifadhi ya taifa Mahale, hifadhi ya taifa Mikumi, hifadhi ya taifa ziwa Manyara, hifadhi ya taifa Rubondo, hifadhi ya taifa Serengeti, hifadhi ya taifa Saadani, hifadhi ya taifa Tarangire, Hifadhi ya taifa Udzungwa, hifadhi ya taifa Kitulo, hifadhi ya taifa Mkomazi, na hifadhi ya taifa tarajiwa ya Saanane. Hifadhi ya Serengeti pekee ni kubwa kuliko taifa la Gambia!

Katika maajabu saba ya asili ya bara la Afrika, maajabu matatu yanatoka nchini Tanzania huku ajabu la 4 (mto Nile) chimbuko lake likiwa Ziwa Viktoria linalomilikiwa na Tanzania kwa zaidi ya asilimia 50. Hakuna wa kunipinga nikisema Nabii Musa na hata YESU KRISTO walikunywa maji kutoka Tanzania maana tumefundishwa uhai wa nchi ya MISRI unatokana na mto Nile (Nile is Egypt and Egypt is Nile). Shughuli zote za kilimo na maisha za wakazi wa Misri zinategemea mto Nile unaotoa maji yake Ziwa Victoria.

Ukitaka kusimama sehemu yenye mwinuko mrefu kuliko zote barani Afrika ili kujionea uzuri wa bara zima inakulazimu uje Tanzania kisha upande mlima Kilimanjaro. Aidha, ukitaka kuzama sehemu yenye kina kirefu kwenda chini barani Afrika inakulazimu tena uje Tanzania katika ziwa Tanganyika. Ndilo ziwa lenye kina kirefu kuliko yote Afrika na la pili duniani. Hata mti mrefu kuliko yote barani Afrika uko nchini Tanzania. Una urefu wa mita 81, unatoka katika familia ya Entandrophragma excelsum (Mti mrefu zaidi Afrika wagunduliwa Tanzania - BBC News Swahili).

Ni katika taifa la Tanzania pekee unaweza kukutana na aina mbalimbali za wanyama na viumbe wa asili. Tuna aina za vyura ambao mataifa mengine duniani hayana. Vyura aina ya Nectophrynoides asperginis (Vyura wa kihansi), hawapatikani sehemu nyingine yoyote duniani isipokuwa katika bonde la Kihansi nchini Tanzania. Tanzania ni miongoni mwa nchi 6 za maziwa makuu barani Afrika zikiwa na jumla ya maziwa 4 (Viktoria, Tanganyika, Nyasa na Rukwa) kati ya maziwa 9 (tisa) yaliyoko katika orodha rasmi ya maziwa makuu. Tafiti zinaonesha kuwa asilimia 10 ya aina zote za samaki duniani zinapatikana katika maziwa haya makuu huku maziwa ya Viktoria, Tanganyika na Nyasa yakichangia moja ya nne (1/4) ya maji baridi yanayopatinana duniani.

Taifa hili ambalo ni la 13 kwa ukubwa wa eneo barani Afrika na la 31 duniani, limetenga zaidi ya asilimia 35 ya ardhi yote kuwa hifadhi ya taifa kwa maana ya mapori ya akiba na mbuga za wanyama. Kwa zaidi ya nusu karne sasa tumekuwa kisiwa cha Amani na kimbilio la wanyonge kutoka mataifa mbalimbali. Pamoja na taifa hili kuwa na makabila zaidi ya 120 na tofauti mbalimbali za kiimani, bado tumeendelea kuishangaza dunia kwa jinsi tunavyoishi kwa kuvumiliana na kuelewana. Ni taifa pekee Afrika ambalo licha ya watu wake kuwa na lugha zao nyingi za asili, WOTE wanaunganishwa na lugha moja ya Kiswahili ambayo sio lugha ya mkoloni!

Tanzania imebarikiwa kuwa nchi ya pili barani Afrika kwa wingi wa mifugo (ng’ombe, mbuzi na kondoo) nyuma ya Ethiopia lakini hatuna bomba hata moja linalotiririsha maziwa. Bado Tanzania ni taifa linaloongoza kwa kuagiza maziwa ya kopo kutoka ughaibuni. Viatu, mikoba na bidhaa mbalimbali za ngozi ambazo taifa lingeweza kuzalisha hazipo tena kwa sababu tunaongoza kwa kuuza mifugo hai nchini Kenya kisha wao wanachinja na kuuza kupata bidhaa zaidi ya kumi. Watanzania tubadilike.

Tanzania imebarikiwa kuwa na misitu mingi ya asili pamoja na nyika. Ardhi nzuri tuliyonayo na mvua ya kutosha ni fursa nzuri ya kuwa na misitu mingi ya kupandwa nchini lakini haipo na wala hatuna bomba hata moja linalotiririsha asali katika misitu na nyika hizo! Mungu atupe nini?

Tanzania imebarikiwa kuwa na tambarare na mabonde mazuri kuliko mataifa mengi hapa duniani. Tuna bonde la mto Pangani lenye ukubwa wa kilometa za mraba 53,600 (Ukubwa sawa na mataifa ya Rwanda na Burundi kwa pamoja!), tuna bonde la mto Ruvuma lenye ukubwa wa kilometa za mraba 152,200 ambazo kati ya hizo kilometa za mraba 52,200 (ukubwa zaidi ya taifa la Denmark!) ziko nchini Tanzania na eneo linalosalia liko Msumbiji na Malawi. Tuna bonde la ziwa Nyasa lenye kilometa za mraba 132,000 lililoko katika nchi za Tanzania, Malawi na Msumbiji ambapo eneo la bonde kwa Tanzania ni kilometa za mraba 37,000 (ukubwa zaidi ya taifa la Ubelgiji!). Tuna bonde la ziwa Rukwa lenye ukubwa wa kilometa za mraba 88,000 (ukubwa zaidi ya taifa la Austria). Pia tuna bonde la Wami Ruvu lenye kilometa za mraba 72,930 (ukubwa mara mbili ya mataifa ya Haiti na Jamaica kwa pamoja!). Pia tunayo mabonde ya ziwa Tanganyika, bonde la Ziwa Viktoria na mabonde ya ziwa Eyasi, Manyara na Bubu. Mabonde yote haya yana maji ya kutosha na ardhi yenye rutuba kwa kilimo na ufugaji wa kisasa wa samaki.

Katika utajiri wa maliasili ni wazi taifa letu limependelewa. Mpaka sasa tuna akiba ya madini ya Dhahabu inayofikia wakia milioni 36, uzalishaji utakaotufanya tushike nafasi ya tatu baada ya Ghana na Afrika Kusini. Tuna hazina kubwa ya madini ya Urani, uzalishaji ambao utatuweka katika nafasi ya tatu Afrika baada ya Niger na Namibia. Tuna gesi asilia yenye ujazo wa zaidi ya futi trilioni 26, tuna madini ya makaa ya mawe yanayofikia tani milioni 50.94, tuna madini ya chuma pia. Tuna madini adimu ya Tanzanite ambayo hayapatikani sehemu yoyote ile duniani na zaidi ya yote, hivi karibuni imepatikana hazina kubwa ya madini ya magadi soda huko Monduli mkoani Arusha. Eneo hilo lenye mita za ujazo bilioni 4.6 za madini hayo zitaipaisha Tanzania hadi nafasi ya tatu nyuma ya Marekani na Uturuki kwa uzalishaji. Pamoja na hazina yote hii, bado tunaambiwa kwa mdomo eti pale jangwani upande wa pili wa Misri ndipo ilipokuwa bustani ya Edeni. NAKATAA.

Kitabu kitakatifu cha Biblia kinaielezea bustani ile kuwa ilizungukwa na maji pande zote nne kwa maana ya kaskazini, kusini, mashariki na magharibi na maji yale yalikuwa yakitiririka kuingia bustanini (Mwanzo 2:10-14). Hakuna TAIFA lingine hapa duniani lenye aina hiyo ya maji zaidi ya Tanzania. Upande wa kaskazini tumezungukwa na mito ya maji ya ziwa Viktoria, hili ni ziwa la kwanza kwa ukubwa barani Afrika na la pili duniani baada ya ziwa Superior lililoko Amerika ya Kaskazini. Upande wa Magharibi tumezungukwa na ziwa Tanganyika ambalo ni ziwa lenye kina kirefu kuliko yote barani Afrika na la pili duniani baada ya ziwa Baikal lililoko Asia. Upande wa Kusini tumezungukwa na ziwa Nyasa. Hili ni ziwa la tisa kwa ukubwa duniani, la tatu kwa ukubwa na la pili kwa kina barani Afrika. Upande wa mashariki tumezungukwa na ufukwe wa Bahari ya Hindi wenye urefu wa zaidi ya kilomita 800 kuanzia mkoani Tanga hadi Mtwara. Pamoja na maji yote haya yanayotiririshwa na Mungu kuingia bustanini bado mnaniambia hii sio Edeni? POA NIKOSOENI LAKINI EDENI HAIKO MASHARIKI YA KATI.

Watanzania tuamke, tubadilike na tupambane katika kuinua uchumi wa taifa letu. Wasomi tuache kunung’unika na badala yake tujikite katika kupambana na changamoto zinazoikumba jamii kwa kuzibadili kuwa fusa za ajira na serikali ijikite katika kutengeneza mazingira bora na yaliyo rafiki kwa raia wake kuishi kwa amani na utulivu. (gnyaissa@yahoo.com)
Historia ya Biblia na Qur'an ni vitu vilivyotungwa tu na watu, wala si maneno ya Mungu, asikudanganye mtu.
 
Naona umeanza kuandika huku unatetemeka, nikuache usije kufa kwa pressure.

Nimekuuliza wapi bustani ya Eden ilipo nipande ndege niende, usiseme ipo karibu na mji au kitu fulani, nipe complete answer, kinyume na hapo jione ulivyo na fikra finyu unabishana na usiemjua.
Kwanza kabla sijakuambia ipo wapi, first tukubaliane wewe ni "empty set" katika dhana zima ya uumbaji.. na si ajabu hujui hata umeumbwa na nani (Maana najua utasema wazazi wako, Hahahahahah)... Kwanini wewe ni empty set? Kwasababu Kama hufahamu kuhusu Eden kibiblia (maana umeniambia sijui kuhusu theories, hahahaha.. usimfedheheshe Mungu wako kwa kuleta theory za wanadamu kwenye Neno Lake ambalo linahitaji Uongozi wa Roho Mtakatifu tu) huwezi kufahamu kuhusu uumbaji.

Pili, tupeane ushirikiano wa kimaandiko.. yale Mambo yako ya principal sijui theory wachia wasio Amini uwepo wa Mungu.. sawa?
 
Mkuu hii nondo imetukia...

Haya ndio mabandiko tunayoyataka Hayachoshi yani.

Ila wadau sio watu wazuri ivi mnawezaje kupita bila kupiga kura, au humu stori tu kula kwenu.
 
Ukiamini kuwa binadamu wa kwanza aliiishi Ngorongoro basi hautaamini kuwa Adam na Hawa ndio walikuwa binadamu wa kwanza, kwa sababu story ya binadamu wa kwanza Kuishi Ngorongoro ina support Evolution theory!
 
Back
Top Bottom