matunduizi
JF-Expert Member
- Aug 20, 2018
- 7,968
- 19,368
Niliingia first Year nikiona mwaka wa mwisho wote wanaijiwa na waajili wakaanze kazi. Siku namaliza hakuna hata hata mmoja aliyekuja. Hali ilikuwa imebadilika. Nilikuwa nimeshaapa sirudi nyumbani afe kipa afe beki.
Plan B
Niliandaa barua na CV kama 200 hivi. Za elimu zote, form 4, six, ya chuo na ya general degree. Nikapuyanga kila ofisi niliyoigugo posta. Lengo sio ajira lengo ni kuzuia njaa kwanza wakati mengine yatafuata hukohuko. Nikatoka kapa, nikaishia kumaliza sole za viatu tu.
Plan C
Nilikutana na mbabe mmoja aliyenipa mbinu ya kuforce kuajiliwa. Huyu alisoma Ulaya, akasota bongo hadi alipojilipua. Kuforce kukutana na bosi wa makampuni kwa kukwepa viunzi vya machawa na Makatibu Muhtasi wanaomzunguka.
Nikaforce ofisi moja, nilimrubuni secretary akanipa access ya kuonana na Boss. Yule jamaa ni mtu mwema sana. Wakubwa wengi ni watu wema na wasikivu sana. Nilivyojieleza na kutestiwa kidogo kesho yake nikaingia kitengo.
Hakuna Interview, hakuna pepa, hiyo transition ilinivusha hadi nilipoendelea na mission zangu ambazo ndio zilikuwa kipaumbele changu.
Kama mkristo nimejifunza.
Sio kila kitu utakipata kwa kufuata utaratibu. Taratibu nyingi na sheria na miongozo ni kwa ajili ya watu wasio na connection.
Nilijifunza, lazima ujilipua na kujihatarisha ili mambo yaende. Sio kila kitu utakipata kwa kusubiri utaratibu. Ukiomba Mungu akikupa kibali unaingia popote kama Malkia Ester alivyowaokoa wayahudi kwa kuingia kwa mfalme kinyume na utaratibu.
Sijasema ni lini, wapi, maana msingi ni nilichojifunza. Hadi leo nikitaka chochote kwa yeyote bila kujali cheo au hadhi nitatafuta mbinu zote nimfikie kama wale jamaa waliotoboa bati ili mgonjwa wao amfikie Yesu baada ya kuona njia za kawaida zimezibwa na makutano.
Ni hayo tu.
Plan B
Niliandaa barua na CV kama 200 hivi. Za elimu zote, form 4, six, ya chuo na ya general degree. Nikapuyanga kila ofisi niliyoigugo posta. Lengo sio ajira lengo ni kuzuia njaa kwanza wakati mengine yatafuata hukohuko. Nikatoka kapa, nikaishia kumaliza sole za viatu tu.
Plan C
Nilikutana na mbabe mmoja aliyenipa mbinu ya kuforce kuajiliwa. Huyu alisoma Ulaya, akasota bongo hadi alipojilipua. Kuforce kukutana na bosi wa makampuni kwa kukwepa viunzi vya machawa na Makatibu Muhtasi wanaomzunguka.
Nikaforce ofisi moja, nilimrubuni secretary akanipa access ya kuonana na Boss. Yule jamaa ni mtu mwema sana. Wakubwa wengi ni watu wema na wasikivu sana. Nilivyojieleza na kutestiwa kidogo kesho yake nikaingia kitengo.
Hakuna Interview, hakuna pepa, hiyo transition ilinivusha hadi nilipoendelea na mission zangu ambazo ndio zilikuwa kipaumbele changu.
Kama mkristo nimejifunza.
Sio kila kitu utakipata kwa kufuata utaratibu. Taratibu nyingi na sheria na miongozo ni kwa ajili ya watu wasio na connection.
Nilijifunza, lazima ujilipua na kujihatarisha ili mambo yaende. Sio kila kitu utakipata kwa kusubiri utaratibu. Ukiomba Mungu akikupa kibali unaingia popote kama Malkia Ester alivyowaokoa wayahudi kwa kuingia kwa mfalme kinyume na utaratibu.
Sijasema ni lini, wapi, maana msingi ni nilichojifunza. Hadi leo nikitaka chochote kwa yeyote bila kujali cheo au hadhi nitatafuta mbinu zote nimfikie kama wale jamaa waliotoboa bati ili mgonjwa wao amfikie Yesu baada ya kuona njia za kawaida zimezibwa na makutano.
Ni hayo tu.