Hapo ulimuweza maana inaaminika dawa ya mchawi ni kumkemea au kumsonya kuonesha kumpuuza,hata mimi ilishanitokea Nyumbani,siku hiyo tumemaliza kula kila mmoja akaenda zake kulala(Nyumba ni self ya vyumba vinne),lakin ilikuwa haina dari juu,sasa mida ya kuanzia saa saa 5-6 kuna kitu kinatua juu ya bati,ni kama ndege fulani(kunguru),sikuwahi kumshuhudia ila ndiyo utuaji wake,(Kunguru ana tabia arfajil anatua kwenye Nyumba na kuanza kutembea),bas akitua anaanza kukwaruza bati na makucha yake hivyo inakuwa kero kubwa usiku huo,siku moja nikapata ujasiri nikaanza kuongea wakati huo nipo ndani usiku,nikasema kwa nguvu -"Watu wengine mmekosa kazi za kufanya mnaanza kusumbua wengine usiku,ni ujinga badala ya kulala unaanza kutembea kwenye majumba ya Watu na kuanza kuwasumbua na haupati faid yoyote,huo muda bora ungeutumia kufanya mambo mengine yenye faida...kama wewe huko juu ni Mtu na siyo ndege kama unavyotaka kuaminisha Watu(akanyamaza kimya),nyie ndiyo mnajitafutia taabu(mkwara tu) na ipo siku yako,tangu siku hiyo mpaka leo huo upuuz ulikomaa