Ndugu zangu, katika maisha kuna wakati tunapitia changamoto mbalimbali za kimaisha ikiwa pamoja na mapenzi.Nilimpenda dada mmoja kwa dhati kabisa, lakini upendo toka kwake ulikuwa kama wakulazimisha hivi, maana wakati mwingine unamuona online ukimtumia msg hajibu au anachelewa sana ukiona anajibu haraka ujuwe ana lake. Niliendelea nae hivyo hivyo kwa kipindi cha mwaka mzima kwa uhusiano wa kuvuta na kamba.
Mwaka jana mwezi desemba tarehe 23 niliamua kwa dhati kabisa kuachana nae. Hatua ya kwanza niliacha kabisa kumtafuta kwa mwezi mzima huku akichungulia whatsapp status zangu na mimi kwa roho ngumu nikiangalia zake, ilipofika Janauari mwishoni mwaka huu nika m-block kabisa na kudelete number zake.
Feb alinitafuta kupitia namba ya mdogo wake nikapokea kwa vile nilikuwa siijuwi kisha yeye aliongea kwa kuomba msaaada wa kumpeleka mdogo wake Aghakhan Hospl, nilikubali kwa maana niliona siyo vita acha nitoe tu msaada, nilipofika kuwachukua sikuongea nae sana ukiondoa kumpa salaam na kisha kumpeleka huko hospital tulipofika sikuongea chochote kitu ambacho si kawaida yangu mbali ya kuwaacha na mimi kusepa zangu jambo si lakawaida.
Siku iliyofuata nikapokea simu toka kwa rafiki yake kuwa yule dada nae amewekwa mapumziko hospital ya jirani lakini hawaoni ana tatizo gani, nikamwahidi nitampigia kumjulia hali lakni sikufanya hivyo kwani nilihisi ni usongo tuuu wa mawazo hana lolote.
Jana jioni dada kapiga tena simu kupitia namba nyingine kwa sababu ya mdogo wake nayo nime block toka siku ile, na nilivyosikia tu sauti yake nilimwambia nitampgia maana nipo kikaoni, sijapiga na sitompigia maana nikianza kuwasiliana tutarudi kwenye mahusiano ambayo yeye mwenyewe aliyaletea mzaha. Tutanatimiza miezi mitano kuelekea wa sita bila mawasiliano rasmi, nimezuia mawasiliano na nimezuia kuonana naye ili iwe funzo kama mtu anakupenda usifanye mzaha na aweke nidhamu.
Nawakilisha kwenu wapendwa.
Mwaka jana mwezi desemba tarehe 23 niliamua kwa dhati kabisa kuachana nae. Hatua ya kwanza niliacha kabisa kumtafuta kwa mwezi mzima huku akichungulia whatsapp status zangu na mimi kwa roho ngumu nikiangalia zake, ilipofika Janauari mwishoni mwaka huu nika m-block kabisa na kudelete number zake.
Feb alinitafuta kupitia namba ya mdogo wake nikapokea kwa vile nilikuwa siijuwi kisha yeye aliongea kwa kuomba msaaada wa kumpeleka mdogo wake Aghakhan Hospl, nilikubali kwa maana niliona siyo vita acha nitoe tu msaada, nilipofika kuwachukua sikuongea nae sana ukiondoa kumpa salaam na kisha kumpeleka huko hospital tulipofika sikuongea chochote kitu ambacho si kawaida yangu mbali ya kuwaacha na mimi kusepa zangu jambo si lakawaida.
Siku iliyofuata nikapokea simu toka kwa rafiki yake kuwa yule dada nae amewekwa mapumziko hospital ya jirani lakini hawaoni ana tatizo gani, nikamwahidi nitampigia kumjulia hali lakni sikufanya hivyo kwani nilihisi ni usongo tuuu wa mawazo hana lolote.
Jana jioni dada kapiga tena simu kupitia namba nyingine kwa sababu ya mdogo wake nayo nime block toka siku ile, na nilivyosikia tu sauti yake nilimwambia nitampgia maana nipo kikaoni, sijapiga na sitompigia maana nikianza kuwasiliana tutarudi kwenye mahusiano ambayo yeye mwenyewe aliyaletea mzaha. Tutanatimiza miezi mitano kuelekea wa sita bila mawasiliano rasmi, nimezuia mawasiliano na nimezuia kuonana naye ili iwe funzo kama mtu anakupenda usifanye mzaha na aweke nidhamu.
Nawakilisha kwenu wapendwa.