Nilienda kwa lengo la kushauriwa nikaishia kusimangwa

Nilienda kwa lengo la kushauriwa nikaishia kusimangwa

Kalaga Baho Nongwa

JF-Expert Member
Joined
Sep 27, 2020
Posts
9,953
Reaction score
23,150
Kwa niliyokutana nayo kalaga baho niseme tu safari ya maisha ni ndefu sna. Mikasa, visa na vibweka kwa akili za watanzania ndo mahala pake. Umaskini nao ndo umefika

Juzi wazee nilishikwa kwelikweli, maisha magumu sana Dira haioneshi wapi ni kaskazini. Basi nikajikoki kutafuta watu wazima kidogo wanipe neno la busara na maneno yanaleta hisia mpya na matumaini. Nikamcheki Shangazi yangu mmoja hiv akasema "njoo tujadili"

Basi wakuu kufika pale niko nje nimegonga hodi akauliza "nani?" Nikajibu "mm kalaga baho" nikasikia kawasha redio taarabu "siiina mda huooo , siiina! Wa kukaa vipembeni kudiskasi na mtu". Nikajua anatania
Kuingia ndani nimesalimia kukaa chini nikasikia karopoka "kula chuma hicho". Heeeh, kumbe mm wakati namueleza shida nije anishaur Ali furaha sana.

Nikaa chini ndugu zangu yule mama nilijuta!. Ushaur uliotoka pale ulisisitiza kujikaza kiume na maisha yakizid kuwa magum sana kanishauri nilie. Neno "ndo ukubwa huo! na ndo umekuwa uyaone ndo hayo!" Yalijirudia katika kila sentensi aliyoizungumza. Bas wakuu nikaona leo nimeyamunya nikajifanya napokea simu iliyoita nikatoka mpaka stendi nikakwea daladala nikarudi geto.

Kanipigia simu niko wapi mbona sijaaga. Nikamwambia nilipigiwa simu ya dharura sikutakiwa kubaki tuendelee na mazingumzo. Kama hakuwa na ushauri si angesema tu.

Yule mama mwehu nini?
 
Halafu mbaya ukisema matatizo shida ,usipo sema pia unaonekana una madharau😅😅 ishi maisha yako waswahili tupo tupo tu hatujui hata tunaishi ili iweje😅😅😅
Ah kuna watu wana roho za kichwai sana. Ndugu gani kama yule mkuu? Ndugu ukimwambia hujala anafurahi sana ukimfata kumuomba ushaur una milioni nane unataka kufanya biahsra akushauri ukiondoka analia inamuuma kunako mtima. Huu si uchawi
 
Hakunaga ushauri wa bure.

Kwanza washauri hawajazaliwa bado

KILA MTU ANA STRESS ZAKE

Unakuta Mshangazi hauna mbele wala nyuma halafu unaweka shida zako anapata cha kusimulia akiwa na Mshangazi baadae
Kwa hiyo mishangazi ndo mifumo yenu ya maisha sio?

Ndo mana mashangazi (madada wa baba) mnakuwaga na matiti makubwa kama matikiti maji na makalio madogo kama skonsi
 
Kwenye haya maisha watu ambao wanaweza kuwa wanakupenda Kwa dhati na kukuombea ufanikiwe ni Wazazi wako na Watoto wako tu

Hawa Ndugu na jamaa wengine tuishie kunywa nao beer tu na Kuchoma nao Kuku, kamwe usidhani wanaweza kukupenda na kutamani ufanikiwe

Mchekeshaji kutoka Nchini Kenya, Profesa Hamo huwa anasema "kwanini tubebe mizigo yako wakati Kila mtu ako na yake"
 
Kwenye haya maisha watu ambao wanaweza kuwa wanakupenda Kwa dhati na kukuombea ufanikiwe ni Wazazi wako na Watoto wako tu

Hawa Ndugu na jamaa wengine tuishie kunywa nao beer tu na Kuchoma nao Kuku, kamwe usidhani wanaweza kukupenda na kutamani ufanikiwe

Mchekeshaji kutoka Nchini Kenya, Profesa Hamo huwa anasema "kwanini tubebe mizigo yako wakati Kila mtu ako na yake"
Babu ukinywa nao beer pia siwanaweza hata kukuwekea sumu🤔
 
Kwenye haya maisha watu ambao wanaweza kuwa wanakupenda Kwa dhati na kukuombea ufanikiwe ni Wazazi wako na Watoto wako tu

Hawa Ndugu na jamaa wengine tuishie kunywa nao beer tu na Kuchoma nao Kuku, kamwe usidhani wanaweza kukupenda na kutamani ufanikiwe

Mchekeshaji kutoka Nchini Kenya, Profesa Hamo huwa anasema "kwanini tubebe mizigo yako wakati Kila mtu ako na yake"
Sasa mkuu ushauri unakugharimu nn? Ushauri ni maneno tu.. sasa mpaka maneno ya kuongea kama huna si unasema tu. Mtu anapewa dhamana ashaur anaongea pumba tukimchapa makofi tunamuonea
 
Babu ukinywa nao beer pia siwanaweza hata kukuwekea sumu🤔
Kwa kweli, unatakiwa kabla hujaenda toilet na kuacha kinywani chako hakikisha umekunywa chote ndiyo uondoke

Ama ukirudi unakimwaga Chini kisha unafungua kinywaji kingine

JK aliwahi kusema hata kule Chamani "hawaachiani Maji ya kunywa mezani"

Imagine 😜
 
Kuna watu wanafurahia kusikia unapata shida, mafaniko aaah..inawachoma roho. Upimage basi wapi pa kutoa madukuduku yako, sio kila mtu yupo upande wako. Saa nyingine bora mtu baki au rafiki kuliko ndugu
Yani ndo nimejionea mama yangu. Huyu mama nimemjaza kwenye saiti zangu atakutwa na shida tu.. bora kiumane tu
 
Kuna mambo mawili nimejifunza, kumwambia mtu hustles zangu na kumwambia shida zangu. Pipo zipo bitter sana kwa sasa.

Wife kila mara nilimuonya tabia yake ya kujiexpose kwa watu, siku lilipomkuta alikuja akalia mbele yangu. They're happy, very happy wakiona yule aliyeongea mafanikio yake sasa ameanguka.
 
Kuna mambo mawili nimejifunza, kumwambia mtu hustles zangu na kumwambia shida zangu. Pipo zipo bitter sana kwa sasa.

Wife kila mara nilimuonya tabia yake ya kujiexpose kwa watu, siku lilipomkuta alikuja akalia mbele yangu. They're happy, very happy wakiona yule aliyeongea mafanikio yake sasa ameanguka.
Dah! Watu wana mbaya sana.. sio wazur hata kidogo. Mengi ukiyaongea yanabuma. Binafsi nimejionea na hili la huyu mama aliyejichanganya limenikimbiza kabisaaa. Tutaonana misibani tu
 
Back
Top Bottom