Nilifanya kosa la kununua mipira ya kiume, (condoms), njiani kwa matumizi ya nyumbani na mke, imekuwa ugomvi sana, nyumba haikaliki

dimaa

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2016
Posts
4,174
Reaction score
5,658
Za siku wakuu.


Kosa nililofanya, niko njiani natokea likizo nyumbani naelekea kazini, ninakoishi pamoja na familia nikasema nichukue mipira ya kiume (condoms), ili nikifika nyumbani kwa mke tuweze kutumia kwa ajili ya kuzuia mimba.

Wakuu nimefika nyumbani wife kageuza kibao, anasema hizi condoms ulichukua za kufanyia nini?, namwelewesha hanielewi, ndani hapakaliki.

Anasema ulikuwa unafanyia mambo yako afu unasema umeleta tutumie. Haelewi kabisa.

Wakuu hii shida inatatulikaje, najuta ningeacha tu kufanya ivo.
 
Mimba unataka kuzuia mwenyewe au mnazuia wote?
 
Mimi ndo maana ntachelewa kuoa!

Yaani kwenye ndoa huwezi kufanya maamuzi Binafsi na kufikia muafaka pasipo kumshirikisha mwenzio.

Ulitakiwa kumueleza Hilo jambo mapema ! Kwa akili ya kawaida fikiria wewe unarudi safarini Kisha unakuta ndani kwa mkeo Kuna condom!

Yaani alinunua pasipo kukushirikisha wewe! Muelewe ni binadamu pia.

Cha kufanya muoneshe huu uzi au kajisalimishe kwa kiongozi wa Kiroho akusaidie
 
Awamu hii utakoma ubishi wako, tulikusihi ujiunge na kundi la wakataa ndoa wewe ukaivagaa ndoa kwa pupa ukidhani ni tamu mithili ya sukari.
 
Hahahaaa jamani familia izi ni noma.

Mkuu kweli ni kosa,endapo ulinunua izo kinga bila majadiliano na mkeo.

Pia kwani mnalea kwa sasa?kama mnalea,uke jadiliana na mkeo mtumie njia ipi ili kuepuka mimba.

May be kuna mmoja wenu ana changa moto ya kiafya,such as sexual diseases?
 
Nani alianza kuzipata ? Kama yeye ndio aliyeaanza kuziona hapo usitafanye sisi na huyo mke wako watoto wadogo 😂😂
 
Kama ni utaratibu mpya ambao uliamua kuuanzisha bila kumshurikisha mwenzio itabidi ujipange sana kwenye kunyoosha maelezo.

Ila kama huwa mko na utaratibu huo basi atakuelewa tu mkuu, just mpe muda tu
 

Mke wako anakufaham kuliko sisi, wewe ni mwongo na yeye sio kichaaa, pambana na Umalaya wako
 
Wakuu nimefika nyumbani wife kageuza kibao, anasema hizi condoms ulichukua za kufanyia nini?, namwelewesha hanielewi, ndani hapakaliki.
Mwambie yuko sahihi, halafu sikiliza atasema nini next, atakachoamua kubali pia usipinge. Endelea na maisha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…