GoldDhahabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2023
- 7,189
- 10,375
Mwishoni mwa mwaka Jana, nilienda nchini Kenya kupitia mpaka wa Sirari.
Kwa sababu nilifika "border" Usiku, niliamua kulala gesti ili niendelee na safari Asubuhi yake.
Nilimka vizuri, na nikatafuta wanakotoa huduma ya vyakula, nikaagiza supu ya kuku, ndizi mchesmsho na Pepsi.
Baada ya hapo, nilibadilisha hela ili kupata ya Kenya kabla ya kuvuka mpaka.
Kwa sababu nilikuwa na muda mrefu kidogo sijafika Tarime, niliamua kutembea tembea kabla ya kuvuka mpaka. Nilipotosheka, nilirejea tayari kuingia Kenya.
Lakini mita chache kabla ya kufika kwenye ofisi za Uhamiaji, mtu mmoja alinifuata na kunipigisha stori kidogo kabla ya kujitambulisha kuwa yeye anatoa huduma ya kubadilisha fedha, na kuniomba aniuzie fedha za Kenya.
Nilivutiwa na uwezo wake wa kujieleza, alionekana ana "skills" za "customer care".
Ingawa nilikuwa nimeshabadilisha fedha, niliamua kutunuku jitihada zake japo kwa kwa kiduchu. Nilikubali kubadilisha tena Tsh 100,000/= kupata Ksh.
Alinipeleka kwenye alichokiita ofisi yake, ambayo ilikuwa jirani na barabara.
Shangao la kwanza: akampigia mwenzake na kumjulisha kuwa kuna mtu anataka kubadilisha hela hivyo aje na "cash". Nikawa najiuliza, huyu ndiye mwenye ofisi au ni dalali?
Mshangao wa pili: aliyeambiwa aje na hela, hakuja peke yake. Alikuja na watu wengine kama watatu. Nilipoona hivyo, nilisogea karibu na mlangoni, muamala tukaufanyia hapo. Sikutaka "kuzama" ofisini kwao.
Mstuko wa kwanza: nilipohesabu hela ya Kenya niliyoinunua kwa Tsh 100,000/=, niligundua nilipunjwa pesa ya Kenya sawa na kama Tsh 6,000/=.
Nilipolieleza hilo, mfanya muamala akaomba azihesabu tena. Alifanya hivyo na akajiridhisha kuwa ni kweli alikuwa amenipunja, na kuongeza kiasi kilichokuwa kimepelea. Wakati wote hayo yakifanyika, nilikuwa nimemkodolea macho ili asinipunje tena.
Nilipokabidhiwa hela, nikaanza kuzihesabu kwa lengo la kuhakikisha kwa mara nyingine. Zilikuwa noti za sh Ksh 50, 100, 200, n.k. Muda nafanya uhakiki, nilikuwa nimesimama nje ya "ofisi" yao. Mmoja wao akanitahadharisha kuwa si vizuri kuzihesabu pesa hadharani maeneo hayo, kwa sababu kuna watu wasio wema. (Wakati inawezekana wao ndiyo hawakuwa wema)
Sikumtilia mashaka.
Hawakuridhika na hicho kiasi nilichobadilisha. Waliendelea kunishawishi ili nibadili hela nyingine nyingi zaidi ili nisiende kupungukiwa huko niendako. Ni mpaka pale nilupowaambia kuwa hiyo 100,000/= niliyobadili kwao ndiyo iliyokuwa hela pekee ya Tanzania niliyokuwa nimebakiwa nayo.
Jibu hilo liliwafanya waje na ushauri mwingine, safari hii, wakijifanya kunipa ushauri utakaonisaidia kufika haraka niendako. Sijui walinionaje?
Waliniambia wanitafutie bodaboda wa kuniptisha njia ya "short cut" ili nisipite kwenye ofisi za Uhamiaji! Hapo ndipo kengele ya tahadhari ilupoanza kugonga.
Kwa nini nipite njia ya panya wakati nina vibali vya kupita njia sahihi?
Hata bei ya bodaboda waliyonitajia ilikuwa ni ndogo sana, ukilinganisha na nauli ya magari ya abiria.
Nadhani, walifikiri mimi ni mgeni sana Kenya. Isingewezekana kwenda kwa bodaboda umbali wa zaidi ya "counties" mbili, tena kwa nauli waliyonitajia. Huenda, walikuwa na agenda yao ovu.
Hata kwa usafiri wa gari, sikuweza kufika siku hiyo. Nililazimika kulala mji fulani na nikaendelea na safari kesho yake Asubuhi.
Nilichohisi ni kuwa walifikiri begi nilikuwa nalo lina "mali", hivyo, huenda walikuwa wanatengeneza amazingira ya kwenda kuniteka. Au, walitaka niingie Kenya kwa njia ya panya ili wakanikitanishe na Askari Polisi au Afisa Uhamiaji wa mchongo. Inawezekana hawakuwa watu wazuri.
Mara tu baada ya kuingia upande wa Kenya, nilihitaji kupata huduma fulani iliyohitaji kutumia hela. Ndipo nilipogundua
kuwa katika ile Tsh 100,000/= niliyoibadilisha mwishoni, shilingi elfu kama ishirini za Kitanzania zilikuwa zinamisi.
Sina uthibitisho, lakini mwenendo waliouonesha unanishawishi kuamini kuwa wao ndiyo walioniibia. Sijajua walitumia mbinu gani kwa sababu walipokuwa walionibadilishia, nilikuwa nikiwakodolea sana macho ili kuepuka kupunjwa, lakini bado nilipunjwa.
Japo ni hela kidogo lakini iliniuma sana. Ni bora kama ningekuwa nimempa alau mtu, lakini siyo kuibiwa "kizembe" vile. Ninachukiansana kuibiwa. Ninachukia mno kupunjwa.
Nipo tayari nimsaidie mtu (bure) sh 10,000/= lakini sikubali nipunjwe sh 100/=.
Nilienda Kenya salama, na nikarudi salama kwa kuzungukia Kampala, lakini hiyo Tsh 20,000/= bado ilikuwa ikiniuma.
Sina uhakika kama ni hao Watanzania wenzangu ndiyo walioniibia, lakini ushahidi wa kimazingira unanishuhudia kuwa huenda ni wao, na walitamani kuiba zaidi ya hiyo sh 20,000/=, sema tu hawakufanikiwa kupata hiyo fursa.
Inawezekana ni Watanzania wenzangu ndiyo walioniibia(ingawa sina uhakika kama ni Watanzania kweli. Pale ni mpakani, ni kawaida kwa watu wa mpakani kuchangamana na wa upande wa pili bila kubwaghudhiwa).
Kama si Watanzania wenzangu ndiyo walioniibia, hela yangu ilipoteaje?
Kwa sababu nilifika "border" Usiku, niliamua kulala gesti ili niendelee na safari Asubuhi yake.
Nilimka vizuri, na nikatafuta wanakotoa huduma ya vyakula, nikaagiza supu ya kuku, ndizi mchesmsho na Pepsi.
Baada ya hapo, nilibadilisha hela ili kupata ya Kenya kabla ya kuvuka mpaka.
Kwa sababu nilikuwa na muda mrefu kidogo sijafika Tarime, niliamua kutembea tembea kabla ya kuvuka mpaka. Nilipotosheka, nilirejea tayari kuingia Kenya.
Lakini mita chache kabla ya kufika kwenye ofisi za Uhamiaji, mtu mmoja alinifuata na kunipigisha stori kidogo kabla ya kujitambulisha kuwa yeye anatoa huduma ya kubadilisha fedha, na kuniomba aniuzie fedha za Kenya.
Nilivutiwa na uwezo wake wa kujieleza, alionekana ana "skills" za "customer care".
Ingawa nilikuwa nimeshabadilisha fedha, niliamua kutunuku jitihada zake japo kwa kwa kiduchu. Nilikubali kubadilisha tena Tsh 100,000/= kupata Ksh.
Alinipeleka kwenye alichokiita ofisi yake, ambayo ilikuwa jirani na barabara.
Shangao la kwanza: akampigia mwenzake na kumjulisha kuwa kuna mtu anataka kubadilisha hela hivyo aje na "cash". Nikawa najiuliza, huyu ndiye mwenye ofisi au ni dalali?
Mshangao wa pili: aliyeambiwa aje na hela, hakuja peke yake. Alikuja na watu wengine kama watatu. Nilipoona hivyo, nilisogea karibu na mlangoni, muamala tukaufanyia hapo. Sikutaka "kuzama" ofisini kwao.
Mstuko wa kwanza: nilipohesabu hela ya Kenya niliyoinunua kwa Tsh 100,000/=, niligundua nilipunjwa pesa ya Kenya sawa na kama Tsh 6,000/=.
Nilipolieleza hilo, mfanya muamala akaomba azihesabu tena. Alifanya hivyo na akajiridhisha kuwa ni kweli alikuwa amenipunja, na kuongeza kiasi kilichokuwa kimepelea. Wakati wote hayo yakifanyika, nilikuwa nimemkodolea macho ili asinipunje tena.
Nilipokabidhiwa hela, nikaanza kuzihesabu kwa lengo la kuhakikisha kwa mara nyingine. Zilikuwa noti za sh Ksh 50, 100, 200, n.k. Muda nafanya uhakiki, nilikuwa nimesimama nje ya "ofisi" yao. Mmoja wao akanitahadharisha kuwa si vizuri kuzihesabu pesa hadharani maeneo hayo, kwa sababu kuna watu wasio wema. (Wakati inawezekana wao ndiyo hawakuwa wema)
Sikumtilia mashaka.
Hawakuridhika na hicho kiasi nilichobadilisha. Waliendelea kunishawishi ili nibadili hela nyingine nyingi zaidi ili nisiende kupungukiwa huko niendako. Ni mpaka pale nilupowaambia kuwa hiyo 100,000/= niliyobadili kwao ndiyo iliyokuwa hela pekee ya Tanzania niliyokuwa nimebakiwa nayo.
Jibu hilo liliwafanya waje na ushauri mwingine, safari hii, wakijifanya kunipa ushauri utakaonisaidia kufika haraka niendako. Sijui walinionaje?
Waliniambia wanitafutie bodaboda wa kuniptisha njia ya "short cut" ili nisipite kwenye ofisi za Uhamiaji! Hapo ndipo kengele ya tahadhari ilupoanza kugonga.
Kwa nini nipite njia ya panya wakati nina vibali vya kupita njia sahihi?
Hata bei ya bodaboda waliyonitajia ilikuwa ni ndogo sana, ukilinganisha na nauli ya magari ya abiria.
Nadhani, walifikiri mimi ni mgeni sana Kenya. Isingewezekana kwenda kwa bodaboda umbali wa zaidi ya "counties" mbili, tena kwa nauli waliyonitajia. Huenda, walikuwa na agenda yao ovu.
Hata kwa usafiri wa gari, sikuweza kufika siku hiyo. Nililazimika kulala mji fulani na nikaendelea na safari kesho yake Asubuhi.
Nilichohisi ni kuwa walifikiri begi nilikuwa nalo lina "mali", hivyo, huenda walikuwa wanatengeneza amazingira ya kwenda kuniteka. Au, walitaka niingie Kenya kwa njia ya panya ili wakanikitanishe na Askari Polisi au Afisa Uhamiaji wa mchongo. Inawezekana hawakuwa watu wazuri.
Mara tu baada ya kuingia upande wa Kenya, nilihitaji kupata huduma fulani iliyohitaji kutumia hela. Ndipo nilipogundua
kuwa katika ile Tsh 100,000/= niliyoibadilisha mwishoni, shilingi elfu kama ishirini za Kitanzania zilikuwa zinamisi.
Sina uthibitisho, lakini mwenendo waliouonesha unanishawishi kuamini kuwa wao ndiyo walioniibia. Sijajua walitumia mbinu gani kwa sababu walipokuwa walionibadilishia, nilikuwa nikiwakodolea sana macho ili kuepuka kupunjwa, lakini bado nilipunjwa.
Japo ni hela kidogo lakini iliniuma sana. Ni bora kama ningekuwa nimempa alau mtu, lakini siyo kuibiwa "kizembe" vile. Ninachukiansana kuibiwa. Ninachukia mno kupunjwa.
Nipo tayari nimsaidie mtu (bure) sh 10,000/= lakini sikubali nipunjwe sh 100/=.
Nilienda Kenya salama, na nikarudi salama kwa kuzungukia Kampala, lakini hiyo Tsh 20,000/= bado ilikuwa ikiniuma.
Sina uhakika kama ni hao Watanzania wenzangu ndiyo walioniibia, lakini ushahidi wa kimazingira unanishuhudia kuwa huenda ni wao, na walitamani kuiba zaidi ya hiyo sh 20,000/=, sema tu hawakufanikiwa kupata hiyo fursa.
Inawezekana ni Watanzania wenzangu ndiyo walioniibia(ingawa sina uhakika kama ni Watanzania kweli. Pale ni mpakani, ni kawaida kwa watu wa mpakani kuchangamana na wa upande wa pili bila kubwaghudhiwa).
Kama si Watanzania wenzangu ndiyo walioniibia, hela yangu ilipoteaje?