Nilijojifunza katika mazishi ya mama yake Halima Mdee - namimi nikifate

Nilijojifunza katika mazishi ya mama yake Halima Mdee - namimi nikifate

Malaria 2

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2023
Posts
6,846
Reaction score
10,288
Mzee Dee katika hotuba yake alisema Mkewe alikuwa na tabia ya kuweka 10% ya kipato chake kwa ajili ya kutoa Zaka ikiwemo kuwasaidia Maskini na wanaohitaji kusomeshwa. Aliyasema hayo wakati wa shughuli ya kumuaga mkewe abayo tuliohudhuria tulisikia hayo

Hili ni jambo zuri sana na limezungumzwa sana katika Quran na hadithi za Mtume.
Tunatakiwa kwa pamoja tufanye hivyo. Mimi binafsi nimejifunza kitu kikubwa hapo. napanga kufanya hivyo. wengine tuige

Hadithi kuhusu Sadaka na Kuondoa Dhambi:
  • Mtume Muhammad (SAW) alisema: "Sadaka inafuta dhambi kama maji yanavyofuta moto." (Tirmidhi)
Kutoa sadaka ni tendo lenye umuhimu mkubwa katika dini ya Kiislamu, na linafaida nyingi kwa muislamu. Hapa kuna baadhi ya faida za kutoa sadaka:

  1. Kuongeza Baraka na Riziki: Sadaka inasaidia kuongeza baraka katika maisha ya muislamu na kuimarisha riziki. Ni sehemu ya wema na hukumu ya Allah kwa wale wanaotoa sadaka kwa nia ya dhati.
  2. Kutakasa Mali: Kutoa sadaka ni njia ya kutakasa mali na kuondoa dhambi zinazoweza kuathiri baraka na mafanikio ya mtu.
  3. Kuimarisha Mahusiano: Sadaka inaweza kuboresha mahusiano ya kijamii kwa kusaidia wale walioko katika hali ngumu. Inakuza mshikamano na upendo ndani ya jamii.
  4. Kupata Thawabu: Kutoa sadaka ni moja ya matendo ya kheri yaliyoagizwa na Allah, na muislamu anapata thawabu (malipo ya Allah) kwa kila kiasi anachotoa.
  5. Kufungua Milango ya Baraka: Sadaka inafungua milango ya baraka na neema kutoka kwa Allah. Ni njia ya kuomba msamaha na kuonesha shukrani kwa yale aliyopewa.
  6. Kuzuia Dhambi: Kutoa sadaka ni njia ya kuondoa dhambi na kutakasa roho. Inasaidia kupunguza athari za dhambi na kuimarisha imani.
  7. Kuongeza Utu na Utu Uzuri: Sadaka inasaidia kuimarisha utu na utu uzuri wa muislamu. Ni njia ya kuonyesha huruma na upendo kwa wengine.
 
Mzee Dee katika hotuba yake alisema Mkewe alikuwa na tabia ya kuweka 10% ya kipato chake kwa ajili ya kutoa Zaka ikiwemo kuwasaidia Maskini na wanaohitaji kusomeshwa. Aliyasema hayo wakati wa shughuli ya kumuaga mkewe abayo tuliohudhuria tulisikia hayo
maiti yoyote haijawahi tenda dhambi kwenye risala
 
maiti yoyote haijawahi tenda dhambi kwenye risala
Mtume Muhammad (SAW) alisema: "Msiwaseme vibaya wafu, kwani wao wamekwishamaliza mambo yao." (Bukhari)
Mtume Muhammad (SAW) alisema: "Mtu anayemsema vibaya maiti atajikuta amepata madhara kwa matendo yake, na akiwachukia wafu, inakuwa kama kumchukia mwenyewe." (Tirmidhi)
 
Mtume Muhammad (SAW) alisema: "Msiwaseme vibaya wafu, kwani wao wamekwishamaliza mambo yao." (Bukhari)
Mtume Muhammad (SAW) alisema: "Mtu anayemsema vibaya maiti atajikuta amepata madhara kwa matendo yake, na akiwachukia wafu, inakuwa kama kumchukia mwenyewe." (Tirmidhi)
ibada ya wafu haijawahi mwacha mtu salama
 
Mkewe alikuwa na tabia ya kuweka 10% ya kipato chake kwa ajili ya kutoa Zaka ikiwemo kuwasaidia Maskini na wanaohitaji kusomeshwa.
Ndiyo matumizi sahihi ya fungu la 10 ila hawa Matapeli wanataka fungu la 10 tuwape wao waendelee kunua V8 ,kufungua maviwanda ,kununua maHUMMER ,kupiga SHOW na MKONO WA BAUNSA etc Fungu la 10 ni kwenda kusaidia wajane ,yatima,masikini ,wasiojiweza etc na si kwenda kumpa Mzee wa Upako aendelee kupiga Konyagi ,au Gwajima aende kula kondoo au mwamposa aende kuongezea mtaji wa kiwanda chake cha maji.
 
Mzee Dee katika hotuba yake alisema Mkewe alikuwa na tabia ya kuweka 10% ya kipato chake kwa ajili ya kutoa Zaka ikiwemo kuwasaidia Maskini na wanaohitaji kusomeshwa...
Sadaka bila matendo mema ni bure kabisa. Mungu (kwenye dini zote) hahongeki. Ukiwa mtenda mabaya kama kufisadi, kuua, kuteka, kuiba, kuzini nk, hata utoe mabilioni ya dola ni bure. Unatakiwa uache dhambi kwanza ndiyo utoe sadaka.
 
Back
Top Bottom