Daisy Llilies
JF-Expert Member
- Apr 19, 2019
- 1,017
- 2,158
Nilipigwa pin ya kutokwenda kazini kwa siku 14. Baba chanja alinipa pesa ya kutumia maana nililalamika mno akaona isiwe shida.
Siku kumi na nne zilivyokwisha tu nilipiga simu ban yangu ikaondolewa. Baada ya kufika kibaruani nilikuta Dettol Antibacterial wipes za kumwaga. Kwakweli kama ni kupambana na corona virus wenzetu wamejitahidi sana.
Kumbe kirusi cha corona kina uwezo wa kukaa nyuma ya mlango au kwenye kitasa na juu ya meza kwa siku tatu na kuendeleza libeneke kwa host mpya. System mpya kazini ni kuwa chumba unachofanyia kazi kila baada ya lisaa moja unalangusa vitu vyote vilivyomo kwa antibacterial wipes.
Kuanzia mipango, vitasa, meza na hata walivyokalia wagonjwa na wageni wao inabidi vioshwe kila siku.
Siku kumi na nne zilivyokwisha tu nilipiga simu ban yangu ikaondolewa. Baada ya kufika kibaruani nilikuta Dettol Antibacterial wipes za kumwaga. Kwakweli kama ni kupambana na corona virus wenzetu wamejitahidi sana.
Kumbe kirusi cha corona kina uwezo wa kukaa nyuma ya mlango au kwenye kitasa na juu ya meza kwa siku tatu na kuendeleza libeneke kwa host mpya. System mpya kazini ni kuwa chumba unachofanyia kazi kila baada ya lisaa moja unalangusa vitu vyote vilivyomo kwa antibacterial wipes.
Kuanzia mipango, vitasa, meza na hata walivyokalia wagonjwa na wageni wao inabidi vioshwe kila siku.