Nilime Nini Zaidi Ya Hivi?

one cater

JF-Expert Member
Joined
Jun 10, 2014
Posts
368
Reaction score
153
Habari Za Mchana Wana Jamvi, Nina Shamba Langu La Hekari 2 Kule VIGWAZA, Nataka Nilime, Nilimuuliza Mtu Nini Kizuri Cha Kulima Kule Akaniambia Ardhi Yake Ni Nzuri Kwa Kwa Kulima Mihogo Na Mahindi, Sasa Nilikuwa Nahitaji Mawazo/Maoni Zaidi Kwa Wenye Uzoefu Na Ardhi Ya VIGWAZA Kama Inafaa Kwa Kilimo Kingine Zaidi Ya Mihogo Na Mahindi, Nawasilisha..
 
Ushauri mzuri ni wa mtu aliyeliona hilo shamba, mtafute mtaalam wa kilimo
 

Jaribu pia kuangalia na msimu tuliopo. Sidhani kama ukipanda mahindi this time yataota hata kama hiyo ardhi ni nzuri kwa mahindi!!
 
Jaribu pia kuangalia na msimu tuliopo. Sidhani kama ukipanda mahindi this time yataota hata kama hiyo ardhi ni nzuri kwa mahindi!!

Vipi akimwagilia, si anauza mabichi kwa ajili ya kuchoma.
 

Njia ya uhakika zaidi ni kumchukua afisa ugani na kuenda naye shambani mkuu, pia unaweza kuchukua sample za udongo.
 
Vipi akimwagilia, si anauza mabichi kwa ajili ya kuchoma.


Mkuu,

Maji sio kigezo pekee cha kulima, hata majira ya mwaka nayo yana mchango mkubwa. Anaweza kuotesha mahindi kuanzia July na akamwagilia kila siku na yasiote sababu ya setting za jua, mvua, joto, baridi vya kipindi hiki visiwe rafiki.

Labda aangalie matikiti kama kuna vyanzo vya maji.
 

ni kweli mkuu, lakini maeneo aliyosema hakuna baridi ya kutishia uhai wa mahindi na kama ana uwezo wa kumwagilia kushindana na jua linavyochukua maji basi lazima avune. btw, wazo la tikiti maji huenda ni zuri zaidi kwa sababu zina soko zaidi, lakini ndiyo ajiandae kuzinywesha maji ya kutosha maana zina kiu hizo!
 

Hapo Kisima, Bwawa au Mto vinahusika!!
 
Jaribu pia kuangalia na msimu tuliopo. Sidhani kama ukipanda mahindi this time yataota hata kama hiyo ardhi ni nzuri kwa mahindi!!

Ahsante Kwa Ushauri Mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…